CCM Zanzibar impe heshima yake John Gideon Okello

CCM Zanzibar impe heshima yake John Gideon Okello

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2011
Posts
25,770
Reaction score
50,247
Inajulikana kuwa aliyeongoza mapinduzi ya Zanzibar mwaka 1964 ni mganda aliyejulikana kwa jina la John Gideon Okello, lakini CCM Zanzibar haitaki kumtambua wala kumpa heshima yake.

CCM tunawajua ni wabinafsi lakini hili la kutokumpa heshima yake aliyeongoza mapinduzi ya Zanzibar litawagharimu.

Kila siku mnayaita ni mapinduzi matukufu wakati aliyeyaongoza hamtaki kumpa heshima yake inayostahili.

Lazima Zanzibar kuwe na mtaa, jengo, uwanja wa michezo, chuo kikuu au alama yoyote kama kumbukumbu kwa ajili ya Okello.

Mtu aliyefanya yale mapinduzi huku kina Karume na wenzake wakiwa wamejificha anawezaje kudharauliwa kiasi hiki?
 
Hawawezi

Watasema aliwaua waarab wao

Pia wataishia kumuita kafir.
Unaweza kupotosha historia lakini huwezi kuifuta.

Mpaka leo ukiwaambia mashabiki wa Mzee Karume waseme huyo kiongozi wao alikuwa wapi siku ya mapinduzi hawana jibu.

Inakuwaje Karume isemwe ndiye aliyeongoza mapinduzi wakati siku yenyewe ya mapinduzi haijulikani alikuwa wapi?
 
hakika

Hata okello mwenyewe amekuja kugundulika after some time baada ya watu kuchimba wenyewe na sylabas za nje kuonesha jamaa huyu
Hili nalo wale wanaotafuta shahada za Uzamili ama Uzamivu ama wanaotaka kuwa wabobevu wa historia ya Zanzibar wanatakiwa wachimbue.

Vichogo ndiyo walioongoza mapinduzi ya Zanzibar lakini leo wanakashfiwa na waliowakomboa.
 
Hii yote ni kutoka na umasikini mkuu.

Haswa pale unapokuwa wa kifikra.

Na haswa pale watu wachache wanapo force umasikini huo ukae ndanj yenu ili wafaidike wao
Kabisa... Mwalimu alisema maadui wetu ni watatu. Ujinga, Umaskini na maradhi.

Bahati mbaya sana watawala wetu wanausheherehesha Umaskini.
 
Kwa nini Watu weusi wa ASP wakisaidiwa na Tanganyika waliipindua serikali ya Sultan?

Kulikuwa na shida gani mpaka serikali ya Sultan na Mohamed Shamte iliyochaguliwa kwa kura halali ikapinduliwa na maelfu ya watu kuuwawa kiholela??
 
Inajulikana kuwa aliyeongoza mapinduzi wa Zanzibar mwaka 1964 ni mganda aliyejulikana kwa jina la John Gideon Okello, lakini CCM Zanzibar haitaki kimtambua wala kumpa heshima yake.

CCM tunawajua ni wabinafsi lakini hila la kutokumpa heshima yake aliyeongoza mapinduzi ya Zanzibar litawagharimu.

Kila siku mnayaita ni mapinduzi matukufu wakati aliyeyaongoza hamtaki kumpa heshima yake inayostahili.

Lazima Zanzibar kuwe na mtaa, jengo, uwanja wa michezo, chuo kikuu au alama yoyote kama kumbukumbu kwa ajili ya Okello.

Mtu aliyefanya yale mapinduzi huku kina Karume na wenzake wakiwa wamejificha anawezaje kudharauliwa kiasi hiki?
ccm imebemenda historia kubwa sana ya Tanzania.
Ya Tanganyika ndo yanasiginwa kabisa...
ccm iliyozaliwa kiharakati na mapinduzi eti leo ina viongozi wanaoona harakati na maandamano ni uhaini!
What goes around comes around.
Kama Zanzibar, Tanganyika itakombolewa na kina Okelo part II
 
Inajulikana kuwa aliyeongoza mapinduzi wa Zanzibar mwaka 1964 ni mganda aliyejulikana kwa jina la John Gideon Okello, lakini CCM Zanzibar haitaki kimtambua wala kumpa heshima yake.

CCM tunawajua ni wabinafsi lakini hila la kutokumpa heshima yake aliyeongoza mapinduzi ya Zanzibar litawagharimu.

Kila siku mnayaita ni mapinduzi matukufu wakati aliyeyaongoza hamtaki kumpa heshima yake inayostahili.

Lazima Zanzibar kuwe na mtaa, jengo, uwanja wa michezo, chuo kikuu au alama yoyote kama kumbukumbu kwa ajili ya Okello.

Mtu aliyefanya yale mapinduzi huku kina Karume na wenzake wakiwa wamejificha anawezaje kudharauliwa kiasi hiki?
Wanasema ni mgalatia. Wabaguzi sana hao jamaa
 
Unaweza kupotosha historia lakini huwezi kuifuta.

Mpaka leo ukiwaambia mashabiki wa Mzee Karume waseme huyo kiongozi wao alikuwa wapi siku ya mapinduzi hawana jibu.

Inakuwaje Karume isemwe ndiye aliyeongoza mapinduzi wakati siku yenyewe ya mapinduzi haijulikani alikuwa wapi?
Kudanganya juu ya aliyeongoza mapinduzi kunaondoa sifa ya kuwa mapinduzi tukufu. Ccm ni malaghai na hayana aibu
 
Kwa nini Watu weusi wa ASP wakisaidiwa na Tanganyika waliipindua serikali ya Sultan?

Kulikuwa na shida gani mpaka serikali ya Sultan na Mohamed Shamte iliyochaguliwa kwa kura halali ikapinduliwa na maelfu ya watu kuuwawa kiholela??
Sasa ndiyo ujue ni kwa nini CCM ya sasa wanayaita maandamano kama ni nia ya mapinduzi.

Jibu la swali lako ni hili: ASP ( Muungano wa waafrika na washirazi) walipata kura nyingi kuliko muungano wa vyama vya Zanzibar Nationalist Party (ZNP) na Zanzibar and Pemba People's Party (ZPPP)

Huo muungano wa hivyo vyama viwili vya ZNP na ZPPP ulipata viti vya ubunge 18 na ASP walipata viti 13 kati ya viti 31 vilivyokuwa vinagombewa.

Lakini kwenye kura moja moja ASP ilipata 54% ya kura zote. Na hapo ikagundulika kule hivyo vyama vingine vinapoungwa mkono kulikuwa na majimbo mengi kuliko maeneo ambako ASP ilishinda.

Kwa nini kulikuwa na umwagikaji mkubwa wa damu. Ni Kwa sababu mapinduzi yenyewe yalijengwa juu ya msingi wa visasi!
 
Inajulikana kuwa aliyeongoza mapinduzi wa Zanzibar mwaka 1964 ni mganda aliyejulikana kwa jina la John Gideon Okello, lakini CCM Zanzibar haitaki kimtambua wala kumpa heshima yake.

CCM tunawajua ni wabinafsi lakini hila la kutokumpa heshima yake aliyeongoza mapinduzi ya Zanzibar litawagharimu.

Kila siku mnayaita ni mapinduzi matukufu wakati aliyeyaongoza hamtaki kumpa heshima yake inayostahili.

Lazima Zanzibar kuwe na mtaa, jengo, uwanja wa michezo, chuo kikuu au alama yoyote kama kumbukumbu kwa ajili ya Okello.

Mtu aliyefanya yale mapinduzi huku kina Karume na wenzake wakiwa wamejificha anawezaje kudharauliwa kiasi hiki?
Hii mzee Mohamed Said hajawai kuandika kuhusu Okello na Zanzibar au yeye anajua Tanganyika tu
 
Sasa ndiyo ujue ni kwa nini CCM ya sasa wanayaita maandamano kama ni nia ya mapinduzi.

Jibu la swali lako ni hili: ASP ( Muungano wa waafrika na washirazi) walipata kura nyingi kuliko muungano wa vyama vya Zanzibar Nationalist Party (ZNP) na Zanzibar and Pemba People's Party (ZPPP)

Huo muungano wa hivyo vyama viwili vya ZNP na ZPPP ulipata viti vya ubunge 18 na ASP walipata viti 13 kati ya viti 31 vilivyokuwa vinagombewa.

Lakini kwenye kura moja moja ASP ilipata 54% ya kura zote. Na hapo ikagundulika kule hivyo vyama vingine vinapoungwa mkono kulikuwa na majimbo mengi kuliko maeneo ambako ASP ilishinda.

Kwa nini kulikuwa na umwagikaji mkubwa wa damu. Ni Kwa sababu mapinduzi yenyewe yalijengwa juu ya msingi wa visasi!
Katiba iliyokuwepo iliyoridhiwa na vyama vyote ikiwemo ASP ilikuwa inatambua wingi idadi ya viti vya ubunge katika kupewa ushindi na kuunda serikali na sio wingi wa idadi ya watu, kama vile tu leo Marekani rais anavyoweza kushinda kwa electoral votes/ college bila wingi wa kura "popular vote".

Jambo lingine kulikuwa na tuhuma za ASP kuvusha watu kutoka bara kuwenda kupiga kura Zanzibar.
 
Inajulikana kuwa aliyeongoza mapinduzi ya Zanzibar mwaka 1964 ni mganda aliyejulikana kwa jina la John Gideon Okello, lakini CCM Zanzibar haitaki kumtambua wala kumpa heshima yake.

CCM tunawajua ni wabinafsi lakini hili la kutokumpa heshima yake aliyeongoza mapinduzi ya Zanzibar litawagharimu.

Kila siku mnayaita ni mapinduzi matukufu wakati aliyeyaongoza hamtaki kumpa heshima yake inayostahili.

Lazima Zanzibar kuwe na mtaa, jengo, uwanja wa michezo, chuo kikuu au alama yoyote kama kumbukumbu kwa ajili ya Okello.

Mtu aliyefanya yale mapinduzi huku kina Karume na wenzake wakiwa wamejificha anawezaje kudharauliwa kiasi hiki?
Huyo walimtumia kufanya mapinduzi Kisha baadae kumfukuza na kumfuta kwenye historia.
 
Hii mzee Mohamed Said hajawai kuandika kuhusu Okello na Zanzibar au yeye anajua Tanganyika tu
Amewahi... Kwa melengo hasi. Ila ukiwauliza walete ushahidi kama Okello na Karume walikuwa wanajuana kabla ya mapinduzi huwa wanakuwa hawana jibu.

Wao husema kuwa Okello alitumwa tu kuongoza yale mapinduzi, ila hawana ushahidi wowote kuonesha kuwa kuna wakati Okello alikuwa ni sehemu ya hivyo "vikao" vya kupanga mapinduzi.
 
Amewahi... Kwa melengo hasi. Ila ukiwauliza walete ushahidi kama Okello na Karume walikuwa wanajuana kabla ya mapinduzi huwa wanakuwa hawana jibu.

Wa husema kuwa Okello alitumwa tu kuongoza yale mapinduzi, ila hawana ushahidi wowote kuonesha kuwa kuna wakati Okello alikuwa ni sehemu ya hivyo "vikao" vya kupanga mapinduzi.
Tafuta kitabu cha "kwa heri Ukoloni, kwaheri Uhuru, Zanzibar na mapinduzi ya Afrabia"....Kina mengi.
 
Hili nalo wale wanaotafuta shahada za Uzamili ama Uzamivu ama wanaotaka kuwa wabobevu wa historia ya Zanzibar wanatakiwa wachimbue.

Vichogo ndiyo walioongoza mapinduzi ya Zanzibar lakini leo wanakashfiwa na waliowakomboa.
Hao vichogo wanatajwa kama wavamizi kutoka nchi jirani..

JokaKuu zitto junior
 
Katiba iliyokuwepo iliyoridhiwa na vyama vyote ikiwemo ASP ilikuwa inatambua wingi idadi ya viti vya ubunge katika kupewa ushindi na kuunda serikali na sio wingi wa idadi ya watu...
Kama nimekuelewa vizuri ni kwa nini ASP walipinga ushindi ambao upo kikatiba?

Hili ukiunganisha na hali iliyopo Sasa Tanzania utawaelewa CHADEMA kugomea uchaguzi wa 2025.

Katiba ni ramani ya nchi, kama Katiba haipo sawa nchi pia haiwezi kuwa sawa.
 
Tafuta kitabu cha "kwa heri Ukoloni, kwaheri Uhuru, Zanzibar na mapinduzi ya Afrabia"....Kina mengi.
Nimekisoma... Kile kitabu ukikiangalia kwa makini ni kitabu kilichoandikwa na watu wanaoamini kuwa "walipinduliwa. Zipo Zanzibar mbili zinazoyaangalia yale mapinduzi Kwa mitazamo miwili tofauti kabisa.
 
Inajulikana kuwa aliyeongoza mapinduzi ya Zanzibar mwaka 1964 ni mganda aliyejulikana kwa jina la John Gideon Okello, lakini CCM Zanzibar haitaki kumtambua wala kumpa heshima yake.

CCM tunawajua ni wabinafsi lakini hili la kutokumpa heshima yake aliyeongoza mapinduzi ya Zanzibar litawagharimu.

Kila siku mnayaita ni mapinduzi matukufu wakati aliyeyaongoza hamtaki kumpa heshima yake inayostahili.

Lazima Zanzibar kuwe na mtaa, jengo, uwanja wa michezo, chuo kikuu au alama yoyote kama kumbukumbu kwa ajili ya Okello.

Mtu aliyefanya yale mapinduzi huku kina Karume na wenzake wakiwa wamejificha anawezaje kudharauliwa kiasi hiki?
Sio Okello pekee bali kuna Wamakonde waliokuwa shamba la mkonge Sakura, Tanga walivuka maji usiku wa kuamkia mapinduzi na kutia nguvu kubwa ambazo Waunguja hawakuwa nao.
Doa kubwa hawa ndio walitekeleza mauaji ya kimbari kwa Waarabu bila kujali nani ni nani.
 
Back
Top Bottom