CCM yanguruma Busanda; Wapinzani chali!

CCM yanguruma Busanda; Wapinzani chali!

Tathmini ya Mchungaji kuhusu uchaguzi wa Busanda:

  1. Operesheni Sangara haijasaidia kitu. Ukizingatia kuwa Operesheni hii ilianzia kanda ya Ziwa Magharibi, ungetarajia iwe ni msukumo fulani ambao ungeleta mabadiliko. Lakini mpaka sasa ni wazi ama Maudhui ya Operesheni Sangara ni dhaifu au Operesheni nzima ni dhaifu na haina mantiki ya kisayansi.
  2. Hotuba ya Zitto na Vita vya Ufisadi. Pamoja na kuwa hotuba hiyo ilikuwa ni murwa, lakini ilitolewa kwenye wakati mbovu. Kauli nyingi za Upinzani na hata humu ndani hazileti mvuto wa mtu kufikiria kwa makini kuwa akichagua kingine, kuna ubora na ataona unafuu wa kuboresha maisha yake. Upinzani umeegemea nguvu zake kuulaani Ufisadi kama ndiyo njia pekee ya kuing'oa CCM na si kuonyesha Mtanzania ni vipianaweza jitegemea kuondokana na CCM au kutegemea chama cha Siasa. Hotuba ya Zitto ilipaswa iwe ndiyo mhimili wa kuhubiriwa kila siku kuonyesha kwa kunyu,bulisha jinsi gani Wananchi wanavyokosa mapato ya rasilimali zao na kupungua kwa maendeleo kutokana na uongozi dhaifu wa CCM, na si kegemea nguvu zote kuwa CHADEMA ndio waliovumbua Ufisadi wa EPA na Kagoda!
  3. Umoja ni Nguvu; Upinzani unaendelea kushindwa kujifunza kuwa kuna umuhimu wa kuwa na umoja. Hebu fikirieni, Mama Killango pamoja na kuchoshwa na Ufisadi na Udhaifu ndani ya CCM, bado alisimama kidete kwenda kuiuza CCM Busanda. Aliacha tofauti zake na Rostam na kufanyia kazi na kuhakikisha Ushindi CCM. Je upinzani uko tayari kuachana na migogoro na mivutano kila siku na kuunda umoja wa kweli na wenye nguvu?
  4. Nguzo na Mizizi iko vijijini: Nilipoandika Chadema must Reform na Focus 2010, nilitoa ushauri kwa Upinzani kujiandaa kwa kujijenga kupitia Serikali za Mitaa na kuachana na pilika za majukwaa makubwa. Nafahamu hizi chaguzi za Kiteto, Mbeya Vijijini, Tarime, Busanda na Magogoni ni namna ya kujipatia Ruzuku, lakini ukweli ni kuwa Upinzani umepoteza nguvu, muda na fedha kujiingiza kwenye Chaguzi ambazo ilikuwa wazi kwamba CCM ingeshinda. Badala ya kuekeza kwenye Ubunge na Uraisi, ka nini Upinzani usiwekeze kwenye Uchaguzi wa Serikali za Mitaa mwaka huu? Hivi hawaoni CCM ilivyo mahiri mpaka kumfanya Katibu Mwenezi wake Aggrey Mwnri kuwa Waziri Mdogo TAMISEMI ni mbinu ya kuhakikisha mizizi na nguzo za CCM zinaimarika huku vijijini ambako ndiko kuna 80%?
  5. Upinzani hauna Sera: Mpaka leo hii, sijui CHADEMA, CUF, TLP na hata NCCR wana sera za namna gani! Nilimuuliza Mnyika miezo kadhaa akaniambia niende kwenye webusaiti yao nikasome Ilani na Mwongozo wa CHADEMA. Mpaka kesho CCM inajulikana ni Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea hata kama imefanya mabadiliko, lakini ile imani ya Ujamaa na Kujitegemea haijafutika kwa wananchi. Je Upinzani mna Sera gani za kujiuza zaidi ya vilio vya Ufisadi?
  6. Watanzania si Tatizo. Ingawa majuzi nilihoji iweje 60% y Watanzania wanaridhika na shida na hivyo kuihakikishia CCM ushindi wa 60%, tatizo la kuleta madadiliko si Watanzania na hata kuwaita Wajiinga au Ndivyo Walivyo. Kosa si Watanzania ni wajinga, bali ni sisi ambao ambao tumeshindwa kuwafundisha namna gani wanaweza kuwa jamii huru yenye kujitegemea!
Hili ni somo jingine kwa Upinzani, na sijui ni nini kinahitajika kifanyike kuwasaida wabadilike. Inasikitisha kuwa Dr. Slaa, Zitto na Mnyika ambao tunajua wako humu ndani, wanashindwa kujifunza kutoka hili Darasa la bure la namna gani wanaweza kufanikiwa.

Inaelekea Darasa tunalotoa, anayeelimika na kufaidika ni yule tusiyemtaka; CCM!

Well presentes; wenye macho waone na kujifunza haya sasa kuelekea 2010
 
CCM imeshinda Busanda, hilo halina ubishi. Kwamba nilitarajia Chadema kushinda hilo nalo halina ubishi nalo lilitegemea mambo kadhaa na mazingira fulani ya kisiasa (niliyoyaanisha huko nyuma).

CCM imeshinda Ubunge na kutetea jimbo lake kiukweli na kihalisia ilistahili kushinda jimbo hilo. Hata hivyo ukiangalia vizuri utaona kuwa CCM haijashinda kushawishi mioyo ya yawatu zaidi.

Mwaka 2005, vyama vitatu vilisimamisha wagombea Busanda. CCM iliibuka kwa ushindi wa asilimia 79.2 (61,868) waliofuatia ni CUF asilimia 16.8 (13,094) na Chadema asilimia 4 (3,107). Hii ina maana kuwa wapinzani walipata jumla ya kura 16,161.

Wapiga kura waliojiandikisha ni 125886.

Hii ina maana gani?

a. Katika uchaguzi huu mdogo chama kilicho "gain" ni Chadema. Kama tukichukulia wale walioipigia Chadema mwaka 2005 ndiyo wameipigia tena mwaka huu (3107) basi kura hizi zinasema zaidi. Matokeo yanasema chadema imepata kura 22,799. Hizi kura zimetoka wapi? Kama wale wote wa CUF ndio pia wameipigia Chadema ina maana bado Chadema wangepata kura 16,161 lakini ziko 22,799!

Hii ina maana kuwa kuna kura 6638 ambazo zimetoka mahali pengine.

b. Kwa vile kura za CCM ndiyo zimepungua kutoka 61,868 hadi 29,242 ni wazi kuwa CCM haikugain. Kwa maneno mengine, chama kilichokubalika zaidi ni Chadema na si CCM. Kukubalika huko kunaonekana kwenye takwimu.


c. Nilisema huko nyuma kuwa siri ya ushindi iko kwenye kujiandikisha na wale watakaojitokeza kupiga kura. Kilichotokea Busanda ndicho pia kilichotokea Kiteto. Wakati ule nilifanya observation hii hii. CCM haishindi kwa kukubalika zaidi bali kwa watu kutojitokeza kupiga kura. Kama watu wengi wangejitokeza kupiga kura hata kufikiria asilimia 60 hivi au karibu ya sabini na ongezeko la Chadema lingefuata mtiririko wa ongezeko tuliloliona hakuna shaka hata kidogo Chadema ingeibuka na ushindi.

d. CCM inajua siri hii; wanajua kwa sababu wao ni chama kikongwe kinachojua mikakati na utaalamu wa uchaguzi. CCM haikuhitaji kushawishi watu wengi wajitokeze kupiga kura; ilihitaji kuwashawishi wana CCM kukipigia kura! NI kwa sababu hiyo basi ushindi wa CCM umetokana na wana CCM wenyewe; kama itafanyika tathmini tutaona kuwa karibu asilimia 80 ya waliopigia kura CCM watakuwa ni wana CCM au watu ambao wana mapenzi na CCM (kitu ambacho kina mantiki).

e. Wapinzani bado hawajafika kwenye kutegemea wanachama; wanategemea watu wenye kuichukia CCM; Huu ni mkakati wa kushindwa. Zile kura karibu 6000 za ziada (ukiondoa za CUF na Chadema) ni kura za wana CCM ambao hawajaridhika na hali iliyopo au watu wengine ambao na wenyewe wameona waachague vinginevyo. Binafsi ninaamini Chadema wangekuwa makini wangewekeza mtaji wao kwenye hawa.

Sijui muda wote wa kampeni Chadema imepata wanachama wangapi wapya Busanda. Sijui katika mikutano yao ya kampeni walitoa mara ngapi nafasi kwa mtu kujiunga na chama chao na kwa kiasi gani waliwaalika watu siyo tu kuichagua Chadema wakati wa uchaguzi bali kukichagua kama chama chao. Bila kuwa na base ya wanachama huwezi kushinda chaguzi za namna hii.

Hivyo, ushindi wa CCM si wa kupuuzia wala kubeza hata kidogo; ni ushindi wa mzoefu wa siasa ni ushindi wa mtaalamu wa mikakati. CCM ni chama cha kisiasa na kinaelewa majukumu na malengo yake ambayo ni kutawala. Katika hili hawana shida kutumia mbinu zozote za kisiasa kujihakikishia ushindi.

Mshindi ni mshindi tu hata kama goli lake la ushindi limekuja kwa penati! CCM inastahili pongezi zote na wapinzani hususan Chadema wanastahili pongezi kubwa zaidi kwa kuonesha kuwa wanaweza kushindana. Lakini hilo peke yake halitoshi, anayepewa tuzo ni mshindi tu, kuwa namba mbili siyo sifa ya ushindi.
 
Mie sikuwa na muda wa kupita post zote..Nilisoma za juu kwanza!

Kama ulitoa tathmini kabla ya matokeo,sasa hivi yametoka una maoni ganui?

nilitoa maoni baada ya matokeo; kwani kanzi kalishatoa taarifa tangu jana wakati nyinyi mnasubiri. Sasa kama hukuchukua muda kusoma utaniuliza kitu kile kile.
 
CCM imeshinda Busanda, hilo halina ubishi. Kwamba nilitarajia Chadema kushinda hilo nalo halina ubishi nalo lilitegemea mambo kadhaa na mazingira fulani ya kisiasa (niliyoyaanisha huko nyuma).

CCM imeshinda Ubunge na kutetea jimbo lake kiukweli na kihalisia ilistahili kushinda jimbo hilo. Hata hivyo ukiangalia vizuri utaona kuwa CCM haijashinda kushawishi mioyo ya yawatu zaidi.

Mwaka 2005, vyama vitatu vilisimamisha wagombea Busanda. CCM iliibuka kwa ushindi wa asilimia 79.2 (61,86 waliofuatia ni CUF asilimia 16.8 (13,094) na Chadema asilimia 4 (3,107). Hii ina maana kuwa wapinzani walipata jumla ya kura 16,161.

Wapiga kura waliojiandikisha ni 125886.

Hii ina maana gani?

a. Katika uchaguzi huu mdogo chama kilicho "gain" ni Chadema. Kama tukichukulia wale walioipigia Chadema mwaka 2005 ndiyo wameipigia tena mwaka huu (3107) basi kura hizi zinasema zaidi. Matokeo yanasema chadema imepata kura 22,799. Hizi kura zimetoka wapi? Kama wale wote wa CUF ndio pia wameipigia Chadema ina maana bado Chadema wangepata kura 16,161 lakini ziko 22,799!

Hii ina maana kuwa kuna kura 6638 ambazo zimetoka mahali pengine.

b. Kwa vile kura za CCM ndiyo zimepungua kutoka 61,868 hadi 29,242 ni wazi kuwa CCM haikugain. Kwa maneno mengine, chama kilichokubalika zaidi ni Chadema na si CCM. Kukubalika huko kunaonekana kwenye takwimu.


c. Nilisema huko nyuma kuwa siri ya ushindi iko kwenye kujiandikisha na wale watakaojitokeza kupiga kura. Kilichotokea Busanda ndicho pia kilichotokea Kiteto. Wakati ule nilifanya observation hii hii. CCM haishindi kwa kukubalika zaidi bali kwa watu kutojitokeza kupiga kura. Kama watu wengi wangejitokeza kupiga kura hata kufikiria asilimia 60 hivi au karibu ya sabini na ongezeko la Chadema lingefuata mtiririko wa ongezeko tuliloliona hakuna shaka hata kidogo Chadema ingeibuka na ushindi.

d. CCM inajua siri hii; wanajua kwa sababu wao ni chama kikongwe kinachojua mikakati na utaalamu wa uchaguzi. CCM haikuhitaji kushawishi watu wengi wajitokeze kupiga kura; ilihitaji kuwashawishi wana CCM kukipigia kura! NI kwa sababu hiyo basi ushindi wa CCM umetokana na wana CCM wenyewe; kama itafanyika tathmini tutaona kuwa karibu asilimia 80 ya waliopigia kura CCM watakuwa ni wana CCM au watu ambao wana mapenzi na CCM (kitu ambacho kina mantiki).

e. Wapinzani bado hawajafika kwenye kutegemea wanachama; wanategemea watu wenye kuichukia CCM; Huu ni mkakati wa kushindwa. Zile kura karibu 6000 za ziada (ukiondoa za CUF na Chadema) ni kura za wana CCM ambao hawajaridhika na hali iliyopo au watu wengine ambao na wenyewe wameona waachague vinginevyo. Binafsi ninaamini Chadema wangekuwa makini wangewekeza mtaji wao kwenye hawa.

Sijui muda wote wa kampeni Chadema imepata wanachama wangapi wapya Busanda. Sijui katika mikutano yao ya kampeni walitoa mara ngapi nafasi kwa mtu kujiunga na chama chao na kwa kiasi gani waliwaalika watu siyo tu kuichagua Chadema wakati wa uchaguzi bali kukichagua kama chama chao. Bila kuwa na base ya wanachama huwezi kushinda chaguzi za namna hii.

Hivyo, ushindi wa CCM si wa kupuuzia wala kubeza hata kidogo; ni ushindi wa mzoefu wa siasa ni ushindi wa mtaalamu wa mikakati. CCM ni chama cha kisiasa na kinaelewa majukumu na malengo yake ambayo ni kutawala. Katika hili hawana shida kutumia mbinu zozote za kisiasa kujihakikishia ushindi.

Mshindi ni mshindi tu hata kama goli lake la ushindi limekuja kwa penati! CCM inastahili pongezi zote na wapinzani hususan Chadema wanastahili pongezi kubwa zaidi kwa kuonesha kuwa wanaweza kushindana. Lakini hilo peke yake halitoshi, anayepewa tuzo ni mshindi tu, kuwa namba mbili siyo sifa ya ushindi.

Good Analysis!

Unawashauri nini CHADEMA baada ya kupoteza?Nini kifanyike ili kuhakikisha wanashinda jimbo la biharamuro?

Je hauoni kuna haja ya CHADEMA kuinga mkono TLP?yaani chama kimoja cha upinzani ndiyo kisimame huko?
 
Hakuna kitu kilicho good kwenye hiyo analysis ya Mwanakijiji,
Analysis iliyojaa subjective opinions ambazo haziko supported na evidence yoyote itakuwaje good!
 
Kuna mtu aliniambia siku moja hapendi kwenda JF maana kuna Mashetani; huenda kweli wapo; maana shetani hujifanya ndiye mfalme kumbe anatekeleza malengo yake; wenye nia na mioyo safi hukimbia mashetani; kuna vigezo vingi kujua nani shetani nani si shetani; ila wataalam waliobobea huweza kubaini nawasilisha hili kama angalizo; unaweza kukaa ktk keyboard kumbe unatekeleza mambo yake mwovu; angalia ndg

- Mkulu wangu Malundi, yamekua haya tena ya shetani badala ya siasa na demokrasia at work? Yaani kila mwananchi kuweka mawazo yake bila kujali upande wa pili sasa wote tukiwaza sawa si hata huyo shetani atakimbia mkuu?

Respect.

FMEs!
 
- Mkulu wangu Malundi, yamekua haya tena ya shetani badala ya siasa na demokrasia at work? Yaani kila mwananchi kuweka mawazo yake bila kujali upande wa pili sasa wote tukiwaza sawa si hata huyo shetani atakimbia mkuu?

Respect.

FMEs!

Hayo maneno huw wanaambiwa na wale wakosaji!wanaodhani tunawasababishia Hasara kisiasa...
 
CCM imeshinda Busanda, hilo halina ubishi. Kwamba nilitarajia Chadema kushinda hilo nalo halina ubishi nalo lilitegemea mambo kadhaa na mazingira fulani ya kisiasa (niliyoyaanisha huko nyuma).

CCM imeshinda Ubunge na kutetea jimbo lake kiukweli na kihalisia ilistahili kushinda jimbo hilo. Hata hivyo ukiangalia vizuri utaona kuwa CCM haijashinda kushawishi mioyo ya yawatu zaidi.

Mwaka 2005, vyama vitatu vilisimamisha wagombea Busanda. CCM iliibuka kwa ushindi wa asilimia 79.2 (61,868) waliofuatia ni CUF asilimia 16.8 (13,094) na Chadema asilimia 4 (3,107). Hii ina maana kuwa wapinzani walipata jumla ya kura 16,161.

Wapiga kura waliojiandikisha ni 125886.

Hii ina maana gani?

a. Katika uchaguzi huu mdogo chama kilicho "gain" ni Chadema. Kama tukichukulia wale walioipigia Chadema mwaka 2005 ndiyo wameipigia tena mwaka huu (3107) basi kura hizi zinasema zaidi. Matokeo yanasema chadema imepata kura 22,799. Hizi kura zimetoka wapi? Kama wale wote wa CUF ndio pia wameipigia Chadema ina maana bado Chadema wangepata kura 16,161 lakini ziko 22,799!

Hii ina maana kuwa kuna kura 6638 ambazo zimetoka mahali pengine.

b. Kwa vile kura za CCM ndiyo zimepungua kutoka 61,868 hadi 29,242 ni wazi kuwa CCM haikugain. Kwa maneno mengine, chama kilichokubalika zaidi ni Chadema na si CCM. Kukubalika huko kunaonekana kwenye takwimu.


c. Nilisema huko nyuma kuwa siri ya ushindi iko kwenye kujiandikisha na wale watakaojitokeza kupiga kura. Kilichotokea Busanda ndicho pia kilichotokea Kiteto. Wakati ule nilifanya observation hii hii. CCM haishindi kwa kukubalika zaidi bali kwa watu kutojitokeza kupiga kura. Kama watu wengi wangejitokeza kupiga kura hata kufikiria asilimia 60 hivi au karibu ya sabini na ongezeko la Chadema lingefuata mtiririko wa ongezeko tuliloliona hakuna shaka hata kidogo Chadema ingeibuka na ushindi.

d. CCM inajua siri hii; wanajua kwa sababu wao ni chama kikongwe kinachojua mikakati na utaalamu wa uchaguzi. CCM haikuhitaji kushawishi watu wengi wajitokeze kupiga kura; ilihitaji kuwashawishi wana CCM kukipigia kura! NI kwa sababu hiyo basi ushindi wa CCM umetokana na wana CCM wenyewe; kama itafanyika tathmini tutaona kuwa karibu asilimia 80 ya waliopigia kura CCM watakuwa ni wana CCM au watu ambao wana mapenzi na CCM (kitu ambacho kina mantiki).

e. Wapinzani bado hawajafika kwenye kutegemea wanachama; wanategemea watu wenye kuichukia CCM; Huu ni mkakati wa kushindwa. Zile kura karibu 6000 za ziada (ukiondoa za CUF na Chadema) ni kura za wana CCM ambao hawajaridhika na hali iliyopo au watu wengine ambao na wenyewe wameona waachague vinginevyo. Binafsi ninaamini Chadema wangekuwa makini wangewekeza mtaji wao kwenye hawa.

Sijui muda wote wa kampeni Chadema imepata wanachama wangapi wapya Busanda. Sijui katika mikutano yao ya kampeni walitoa mara ngapi nafasi kwa mtu kujiunga na chama chao na kwa kiasi gani waliwaalika watu siyo tu kuichagua Chadema wakati wa uchaguzi bali kukichagua kama chama chao. Bila kuwa na base ya wanachama huwezi kushinda chaguzi za namna hii.

Hivyo, ushindi wa CCM si wa kupuuzia wala kubeza hata kidogo; ni ushindi wa mzoefu wa siasa ni ushindi wa mtaalamu wa mikakati. CCM ni chama cha kisiasa na kinaelewa majukumu na malengo yake ambayo ni kutawala. Katika hili hawana shida kutumia mbinu zozote za kisiasa kujihakikishia ushindi.

Mshindi ni mshindi tu hata kama goli lake la ushindi limekuja kwa penati! CCM inastahili pongezi zote na wapinzani hususan Chadema wanastahili pongezi kubwa zaidi kwa kuonesha kuwa wanaweza kushindana. Lakini hilo peke yake halitoshi, anayepewa tuzo ni mshindi tu, kuwa namba mbili siyo sifa ya ushindi.

Haya nakubaliana na wewe sasa na hawa wapinzani wafanyenini kuanzia leo ili washinde 2010?
 
Hakuna kitu kilicho good kwenye hiyo analysis ya Mwanakijiji,
Analysis iliyojaa subjective opinions ambazo haziko supported na evidence yoyote itakuwaje good!

Kwa kulinganisha takwimu za kura za 2005 na za sasa huko Busanda, ni chama gani kimekubalika zaidi kwa watu wengi zaidi?
 
e. Wapinzani bado hawajafika kwenye kutegemea wanachama; wanategemea watu wenye kuichukia CCM; Huu ni mkakati wa kushindwa. Zile kura karibu 6000 za ziada (ukiondoa za CUF na Chadema) ni kura za wana CCM ambao hawajaridhika na hali iliyopo au watu wengine ambao na wenyewe wameona waachague vinginevyo. Binafsi ninaamini Chadema wangekuwa makini wangewekeza mtaji wao kwenye hawa.
wanachama wa mpira wa miguu ni tofauti na wa siasa
wanachama wa mpira wa miguu wakifungwa na timu yao ikishuka daraja hawatakiwi kuisaliti timu wanatakiwa wabaki na kuendelea kuishabikia ie uzalendo

mwanachama wa siasa hutakiwi kuwa kama wa mpira wa miguu
mwanachama wa siasa usiporidhisha na sera za chama chako unatakiwa kukihama na kutafuta mbadala
ni sahihi kwa chadema kuchukua watu wanaoichukia ccm na ndio hivyo inavyotakiwa iwe, wanachama wamechoka wanataka alternative

hata obama alipata watu ambao walikua wana vote republican all their live...
kama chadema wanaweza kuwakamata watu wanaoichukia ccm then the party is in a right direction
watu wanavyofikiria humu JF ni tofauti na watu wanavyofikiria uraini
ukitaka kuisulubisha ccm ndani ya jf ni dakika moja lakini bado utapata upinzani
ukitaka kuisulubisha ccm uraini sio mchezo, bado wa TZ upeo wao ni mdogo sana kwa hiyo mimi naona chadema wanafanya kazi ya ziada na ukizingatia siku hizi viongozi wa TLP na CUF wanasafiri na ccm sio mchezo "ccm wamegundua ukitaka kula vizuri lazima ule na mwenzako" viongozi wa upinzani wanasafiri kimya kimya
 
Mzee Zitto,

Kwanza nianze kwa kukupa pole kwa kushindwa katika jimbo la Busanda. Kusema ukweli najua inauma sana pale mtu unapoinvenst muda na energy zako na kupata matokeo tofauti kidogo . Lakini wana Chadema msife moyo kumbuka wahenga walisema ,"A journey of a thousands miles begins with a single step." Chadema imeanza safari hiyo tunajua fika kwamba safari hii ni ngumu na yenye misukosuko mingi .

Binafsi naamini kabisa ili Chadema ishinde ni lazima muwe strategic ...Kusema tuu twenda Biharamulo bila ya kutafuta tatizo ni nini mtakuwa mnapoteza muda. Ni lazima mumtafute mchawi aliyepelekea nyie kushindwa huu uchaguzi. Mzee Zitto mapendekezo yangu kwa Chadema na vyama vingine ni kama ifuatavyo :

1. Kwanza kabisa ni lazima mtambue ya kuwa CCM ni chama kilichopo madarakani . Wazungu wanasema lazima mtambue strength za CCM , kwa kufanya hivi mtaweza kupanga strategy nzuri za kuishinda CCM bila kuialienate. Chadema ina scarce resources compared to CCM kwa hiyo kushindana na hawa watu katika fedha will be plainly wastage of resources. Ni lazima tutambue ya kuwa CCM has cut-throat technique at their disposal...

2. Ni lazima tutengeneze message ambayo itakuwa ina appeal katika broad base na sio continuing preaching to the choir. Message ambayo itakuwa inajali demographics ya jimbo husika . Hapa naamanisha ya kuwa ni lazima mpate wanaojua takwimu wakae chini na wafanye analysis za nguvu ! Mujue katika jimbo kuna wanawake wangapi, vijana wa ngapi na wazee wangapi . Pia mjue kuna shule ngapi , hospitali ngapi ...la msingi mjue matatizo yanayowagusa hawa watu . Message yenu lazima ibadilike kutokana na mahali muda na wakati. Zitto , the point I am trying to make here is simply, Chadema must forges a message which will resonates with the targeted audience.

3. Ni lazima muangalie data za Busanda kwa ndani zaidi, kama walivyosema watu wengine there is something fishy there ! It doesn't make sense for 80,000 people who registered to vote to shun away from the voting booths. Mimi nadhani ni dhahiri ya kuwa kuwa hapa kuna mchezo uliochezwa. Sasa hapa ni muhimu kufuatalia na kujua ni age group gani ambayo ili register lakini they didn't vote. Pendekezo langu ni lazima baada ya hizi chaguzi mtafute solution ya hili jambo. ..

4. Ni lazima mtoe kudos kwa CCM ya Nyerere na mambo waliyoyafanya . Hii ni muhimu sana katika kuappeal kwa wale ambao ni CCM lakini wako katikati . Ni lazima muonyeshe tofauti kati ya CCM ile na hii ya sasa.

5. Zitto lazima mjitahidi kutumia rhetorical devices katika speech zenu especially pathos . Ni lazima speech zenu ziwaguse wahusika on a personal level . Ni lazima mtu aonyeshwe uhusiano wa siasa na yeye kukosa maji, umeme , shule kwa mtoto . . . n.k
Msiamini ya kuwa wapiga kura wanajua kila kitu.

Itaendelea . . .

good analysis kuna kazi kubwa huko mbele na inahitaji akili na uvumilivu. kumbuka ni kazi ya kuwanyanganya watu tonge mdomoni. hivyo si kazi rahisi
 
Inashangaza sana Mkuu. Inawezekana hawakuwa na muda wa kwenda kupiga kura, ama walipata tabu kujua vituo vyao vya kupigia kura, au kuyaona majina yao au sababu nyingine yoyote. Ila ni idadi inayosikitisha sana.



Siamini kuwa idadi ambayo haikupiga kura inaweza kuwa ilishawishiwa kufanya hivyo kwa kununuliwa kwa shahada zao za kupigia kura. NI watu wengi sana. Fikiria, kama ukinunua kila moja kwa kulipia shilingi elfu moja (1000/=), itagharimu zaidi ya shilingi million 60. Sasa sijui unaweza kutumia kiasi gani cha fedha kuzinunua zote hizo na wao wakaridhika. Pia upinzani ulikuwa macho sana kiasi kwamba isingewezekana kununua shahada nyingi kiasi hicho bila kujulikana.

Sababu ya kuogopa vitisho vya dola nalo sioni kama inawezekana kwa baadhi tu ya watu. Maana hata waliojitokeza nao pia waliona kama kulikuwa na vitisho hivyo, nao pia wangeogopa kujitokeza.



Bila kujali takwimu za Tarime, inajulikana kuwa CHADEMA wako imara zaidi kule. Wana uwakilishi mkubwa hata kwenye Halmashauri ya wilaya ya Tarime. Nguvu hiyo ni kubwa na inabidi waitunze. Ila pia kushinda kama walishinda kwa 62% inaelekea ushindani ulikuwa mkubwa sana kwa kuzingatia vigezo vya hapo juu.

Nadhani tatizo lililopo ni nia ya wananchi kusimama kwenye foleni na kupiga kura. Bado watu wanatakiwa kuonyeshwa umuhimu wa kura zao moja moja. Kuna ambao hudhani kuwa wengine wanaweza kupiga kura na kumchagua wanaomtaka wao. Wengine hudhani kuwa, hata wakipiga kura, hakuna tofauti yoyote kwani kura yake ni moja tu kati ya nyingi. Kwa kifupi elimu inahitajika ili kuleta matokeo yanayotakiwa kwa wananchi kushiriki uchaguzi kila wanapopata fursa ya kufanya hivyo.



Kwakweli mwananchi wa kawaida kujua faida ya kura ni kazi kubwa. Kumbuka yeye immediate need yake ni chakula cha siku hiyo na mara nyingi hawawezi ku- associate matatizo yake na mambo ya kupiga kura na viongozi for hawajawahi kuwa na experience ya kusaidiwa mambo yao binafsi. Wakati mwingine democracy is a necessary but not sufficient condition for the peoples welfare.

Inahitaji moyo wa uzalendo na upendo kwa wengine wenye uwezo wa kulink welfare na politics kuwasaidia wale ambao bado wana loyalty ya vyama vilivyoleta uhuru. Naamini watanzania wengi hawapendi kuona haya ila pia siasa za chuki na magomvi ndizo zinazorudisha watu nyuma. Hizo ni mbinu chafu za wachache wanaonufaika na huu mfumo nadhani vijana wengi hawapendi hayo na hii inanipa moyo kwamba mbeleni hii hali itakwisha na tutaamua ku agree to disagree on ideologies bila kumdhania mwenzako vibaya.

Natoa wito kwa viongozi waliopo madarakani wasaidie kukuza upinzani it is also for their well beings. Maendeleo yakipatikana uchumi ukakua haya mambo madogo madogo ya kufuatiliana fulani kala nini ka vaa nini kaenda wapi yataisha. Adui yetu mkubwa ni sisi wenyewe tukubali tumekosea tukijirekebisha hakuna wakupoteza wote tutakuwa washindi. nahapo wengi watatokea kupiga kura bila hata kuelimishwa. Extensionist claim the gud technology is the one which extends itself without extensionist. Waswahili wakasema chema chajiuza chenyewe.........
 
CCM imeshinda Busanda, hilo halina ubishi. Kwamba nilitarajia Chadema kushinda hilo nalo halina ubishi nalo lilitegemea mambo kadhaa na mazingira fulani ya kisiasa (niliyoyaanisha huko nyuma).

CCM imeshinda Ubunge na kutetea jimbo lake kiukweli na kihalisia ilistahili kushinda jimbo hilo. Hata hivyo ukiangalia vizuri utaona kuwa CCM haijashinda kushawishi mioyo ya yawatu zaidi.

Mwaka 2005, vyama vitatu vilisimamisha wagombea Busanda. CCM iliibuka kwa ushindi wa asilimia 79.2 (61,868) waliofuatia ni CUF asilimia 16.8 (13,094) na Chadema asilimia 4 (3,107). Hii ina maana kuwa wapinzani walipata jumla ya kura 16,161.

Wapiga kura waliojiandikisha ni 125886.

Hii ina maana gani?

a. Katika uchaguzi huu mdogo chama kilicho "gain" ni Chadema. Kama tukichukulia wale walioipigia Chadema mwaka 2005 ndiyo wameipigia tena mwaka huu (3107) basi kura hizi zinasema zaidi. Matokeo yanasema chadema imepata kura 22,799. Hizi kura zimetoka wapi? Kama wale wote wa CUF ndio pia wameipigia Chadema ina maana bado Chadema wangepata kura 16,161 lakini ziko 22,799!

Hii ina maana kuwa kuna kura 6638 ambazo zimetoka mahali pengine.

b. Kwa vile kura za CCM ndiyo zimepungua kutoka 61,868 hadi 29,242 ni wazi kuwa CCM haikugain. Kwa maneno mengine, chama kilichokubalika zaidi ni Chadema na si CCM. Kukubalika huko kunaonekana kwenye takwimu.


c. Nilisema huko nyuma kuwa siri ya ushindi iko kwenye kujiandikisha na wale watakaojitokeza kupiga kura. Kilichotokea Busanda ndicho pia kilichotokea Kiteto. Wakati ule nilifanya observation hii hii. CCM haishindi kwa kukubalika zaidi bali kwa watu kutojitokeza kupiga kura. Kama watu wengi wangejitokeza kupiga kura hata kufikiria asilimia 60 hivi au karibu ya sabini na ongezeko la Chadema lingefuata mtiririko wa ongezeko tuliloliona hakuna shaka hata kidogo Chadema ingeibuka na ushindi.

d. CCM inajua siri hii; wanajua kwa sababu wao ni chama kikongwe kinachojua mikakati na utaalamu wa uchaguzi. CCM haikuhitaji kushawishi watu wengi wajitokeze kupiga kura; ilihitaji kuwashawishi wana CCM kukipigia kura! NI kwa sababu hiyo basi ushindi wa CCM umetokana na wana CCM wenyewe; kama itafanyika tathmini tutaona kuwa karibu asilimia 80 ya waliopigia kura CCM watakuwa ni wana CCM au watu ambao wana mapenzi na CCM (kitu ambacho kina mantiki).

e. Wapinzani bado hawajafika kwenye kutegemea wanachama; wanategemea watu wenye kuichukia CCM; Huu ni mkakati wa kushindwa. Zile kura karibu 6000 za ziada (ukiondoa za CUF na Chadema) ni kura za wana CCM ambao hawajaridhika na hali iliyopo au watu wengine ambao na wenyewe wameona waachague vinginevyo. Binafsi ninaamini Chadema wangekuwa makini wangewekeza mtaji wao kwenye hawa.

Sijui muda wote wa kampeni Chadema imepata wanachama wangapi wapya Busanda. Sijui katika mikutano yao ya kampeni walitoa mara ngapi nafasi kwa mtu kujiunga na chama chao na kwa kiasi gani waliwaalika watu siyo tu kuichagua Chadema wakati wa uchaguzi bali kukichagua kama chama chao. Bila kuwa na base ya wanachama huwezi kushinda chaguzi za namna hii.

Hivyo, ushindi wa CCM si wa kupuuzia wala kubeza hata kidogo; ni ushindi wa mzoefu wa siasa ni ushindi wa mtaalamu wa mikakati. CCM ni chama cha kisiasa na kinaelewa majukumu na malengo yake ambayo ni kutawala. Katika hili hawana shida kutumia mbinu zozote za kisiasa kujihakikishia ushindi.

Mshindi ni mshindi tu hata kama goli lake la ushindi limekuja kwa penati! CCM inastahili pongezi zote na wapinzani hususan Chadema wanastahili pongezi kubwa zaidi kwa kuonesha kuwa wanaweza kushindana. Lakini hilo peke yake halitoshi, anayepewa tuzo ni mshindi tu, kuwa namba mbili siyo sifa ya ushindi.

Hapa nimekupata vizuri Mzee Mwanakijiji
badala ya kutumia helkopta (gharama kubwa) hizi gharama zingetumika kutafuta wenyeji vijijini wenye uwezo wa kuzungumza (siasa) waku convice watu (wao kwa wao wanaelewana vizuri zaidi kuliko wazungumzaji wa kutoka "dar" wanaoongelea vitu vikubwa kama ufisadi, nk vitu ambavyo havieleweki kwa vijijini) na kutafuta vikunda mbalimbali mf. NGOs za kuhamasisha watu wapige kura.

tusidanganyane kuwa wanakijiji hawana uelewa. inategemea tunaongelea kitu gani! kwa wale wanaofuatilia kuhusu Indigineous Knowledge (IK) wanavijiji wanaulewa mkubwa sana katika kutatua matatizo yao. ila huenda wasiwe na uelewa wa mambo/ufisadi unaoongelewa kwenye vyombo vya habari (wizi wa kitaalamu) hivyo badala ya kulaumu uelewa wao tunapaswa kuwajue vizuri na tucheze nao kwa step na nyimbo zinazofanana
 
Mabadiliko ya kweli yanahitaji ushiriki wa mimi na wewe ili kuleta maendeleo endelevu,bila upinzani imara chama hiki kitaendelea kutuhadaa kwamba kinatetea maslai ya wengi.Tunajua kwa uhakika kabisa viongozi walio wengi ktk ccm wanapigania maslai yao na hawako tayari kuweka au kujenga demokrasia ya kweli na chaguzi zilizo huru na za haki.
 
Felister,

Kubali ungali mchanga kama unavyosema mwenyewe. Subiri ukomae, bado unanyonya unataka kuwa mjeshi, lo!!!! Wabongo kwa visingizio tunaongoza. Timu zetu zikishindwa utasikia visingizio kibao, sasa tena mumeanza mara oh! Mwantumu Mahiza kaiba kura, mara wanafanya nini baada ya saa 12 jioni nk. Na hayo matusi yenu ya kuita wana CCM wote mafisadi ndiyo hayo hayo yatakayozidi kuwaangusha. Watu wanawaona hamna busara. "HIVI UNGEKAA KIMYA, NANI ANGEJUA HUNA BUSARA?" Zingatia sana usemi huu.

Kupiga watu kwa manati nayo ni udhaifu mwingine uliowaangusha. Nilisema hapa wiki iliyopita akaja mkubwa mmoja akanishambulia utadhani JF ni ya wapinzani wa CCM pekee, mtu mwingine hana haki ya kuweka post yake.
Wewe nani kakuambia kuwa una BUSARA?
 
Back
Top Bottom