Kuna mambo ambayo CHADEMA wanapaswa kuzingatia katika kampeni zao zinazofuata.
1. Matumizi ya Helikopta yawe kwa nia ya kuwafikisha sehemu zisizofikika kwa urahisi/haraka.
Ila, kwa style yao (Ya sasa) ya kufanya vikao vingi kwa siku moja na kukimbia bila kuvifanyia tathmini, wakidhani kuwaeleza tu wapiga kura kuwa CCM haifai inatosha kuwahakikishia ushindi, ni kujidanganya, na kupoteza pesa zao bure.
Inabidi wafahamu kuwa, wananchi huwa wanakusanyika hata kama kuna janga (mfano ni milipuko ya mabomu, ajali n.k.).
Waangalie maana ya mikusanyiko wanayofanikiwa kuipata, wawe na mipango ya jinsi ya kuitumia mikusanyiko hiyo, na walinde kura wanazoahidiwa.
Wajue, kura nyingi nchini ni floating votes (nadhani zaidi ya 70%). Watumie wanachama wapya (kupitia operation zao - Sangara n.k.) kuongeza idadi ya wanachama, nao waelimishwe kupiga kura na kukisaidia chama kwa mambo mbalimbali.
2. Kwa maoni yangu, CCM itaamka kwa kishindo zaidi kuelekea uchaguzi ujao (Biharamulo, serikali za mitaa na 2010). Baada ya kazi kubwa iliyoipata Tarime na Busanda, ni dhahiri kuwa CCM imejifunza.
Nashauri CHADEMA (ambao inaelekea kuanza kukubalika) kuwekeza zaidi katika chaguzi za Serikali za Mitaa. Na kuachana kabisa na Biharamulo (afterall Mbunge huyo wa mwaka mmoja hawezi kuisaida sana).
Baada ya kuanguka Busanda, sidhani kuwa kuweka nguvu zao Biharamulo kutasaidia CHADEMA kushinda. Ni dhahiri kuwa watashindwa tena (kwa anaebisha "lets bet"). CCM wataendelea kutumia uwezo wake wote (kumbuka wako tayari kwa chaguzi hizi -kifedha na resources nyingine). Hivyo CHADEMA kujiingiza Biharamulo kutawapunguzia nguvu za kushinda Serikali za Mitaa (Mwaka huu).
Serikali za mitaa huongeza nguvu kwa chama kuweza kushinda udiwani, na ubunge katika uchaguzi mkuu (endapo itatumika vizuri). Inabidi wao wawe wakifanya kampeni za serikali za mitaa wakati wenzao wakitafuta ubunge Biharamulo. CHADEMA waamue kusaidia chama wanachotaka kishinde. iyo itawapa presence kidogo kwa wananchi Biharamulo ambayo itasaidia kuwapa nguvu kwenye uchaguzi Mkuu ujao.