Ndio matokeo ya siasa za keyboard hayo na kupeana false hope. Kilichobali sasa ni mtuletee vile visingizio vyenu vya kawaida wizi, ubabe, mkono wa serikali nk.
Ukweli utabaki kuwa wapinzania hususan Chadema hawana mikakati, kuna wapiga genge la wazomeaji tu na sikumbuki ni lini mara ya mwisho kuzomea kumeleta mafanikio kwa chama chochote cha kisiasa.
Wananchi wa Busanda wameongea, tena wameongea loud and clear! hii tabia ya akina Pasco na genge lake kututukania wazee wetu ikome hao hao anao waita wasio na elimu ndio waliomfikisha hapo alipo na leo na elimu yake kubwa ya uhandisi habari, inanikumbusha hadithi ya wimbo wa marehem Marijan wa Chakubanga kujiita John Smith.
Zipo wapi zile tambo na majigambo? zimesaidia nini sera za kuchoma moto bendera? kejeli na matusi kuwaita watu wa makamo vibajaji zimewafikisha wapi?
Huu ni wakati muafaka kwa Chadema kurudi kwenye drawing board ba kuanza upya. Hawa pundit wa JF watawadanganya hawa ni arm-chair generals wanapigana kwenye kkeyboards tu kaeni chini muanze upya siasa si tu kungurumisha chopa na kukusanya watoto kwenye mikutano, kunahitajika mikakati endelevu ya muda mrefu na mfupi.