Kama Busanda ingeshinda Chadema ingelikuwa ni mara ya kwanza jimbo lolote la uchaguzi katika mkoa wa Mwanza kuangukia upande wa upinzani.Kama Watanzania wengi tulivyo na tunavyoamini CCM ndiyo baba na mama yetu.
Ni sehemu chache sana ambazo zinaweza zikachagua chama cha upinzani kwa hoja yoyote ile.CCM ni kama imani ya kidini inavyojengeka kwa muumini si rahisi kuiacha bila mbadala unaoridhisha.
Hakuna wa kulaumu kuhusu hali hii ila Mwalimu Nyerere.Alitutawala kifikra na kulifanya taifa kufuata sera za kijamaa zilizodumaza akili za watu.Alipokubali mfumo wa vyama vingi angejiondoa CCM na kuwa Baba wa Taifa wa kweli wa Tanzania,hali isingekuwa kama ilivyo sasa.Kasumba ya mwalimu haijaondoka na haitaondoka hivi karibuni.
Vyama vyetu vya upinzani vina sera nzuri na vina viongozi shupavu,lakini matatizo ya Watanzania ni makubwa mno kuliko tunavyoweza kudhani.Hatujaanza kuondokana na kasumba ya Nyerere na kwa ujumla umma wetu bado kabisa unaishi katika fikra za enzi za Mwalimu kukiwa na mabadilko kidogo sana.Tuna kazi kubwa sana ya kuubadili mfumo uliopo lakini akili zetu bado bado hazijakaa sawa.
Kuna mmoja wetu alilaumu kwamba Wasukuma wana matatizo ya kutoelewa na katoa mifano kadhaa lakini amejisahau kuwa si Wasukuma pekee.Ukiangalia idadi ya viti vya wabuge wa upinzani nchi nzima utaweza kung'amua kuwa akili za Watanzania hazijawa tayari.Tunahitaji mageuzi ya akili za watu kuziondoa kwenye upumbavu wa kulelewa na mawazo ya Mwalimu na kupigania katiba mpya,demokrasia ya kweli na haki za kiraia.Bado safari ni ndefu ndugu zangu.
Iwapo hamtaki kubadilka basi CCM itaendelea kutawala hadi mwisho wa karne.
Hivi mkuu Makalangilo ulitegemea
Mwalimu Nyerere angependa Chama gani kishinde kama si Chama alichokiasisi CCM? Basi baba wa Taifa ni bonge la mtaalam na watu wa CCM waendelee kumpongeza, na Makalangilo aendelee kumlaumu Mwalimu kwa kufanya kazi yake vizuri ya kuhakikisha kuwa chama chake CCM kinaendelea kuchaguliwa. Si ndio wajibu wa kila mtu kujitahidi chama chake kishinde?
Of course asingependa mengi yanayofanywa na viongozi wa Serikali na CCM, kama kuwalinda mafisadi etc.
Mimi nadhani matatizo ni haya:
1. Upinzani bado kujipenyeza vijijini huko ndani kabisa. Huko kuna watu wanaitwa wajumbe (wale wa nyumba kumi) bado wapo hao, na wote ni CCM. So far upinzani haujajipenyeza kihivyo.
2. Upinzani wawaeleze wananchi, hasa wa vijijini kitu watachowafanyia pale wakichaguliwa, zaidi ya kusema tu pale CCM waliposhindwa.
3. Kuna tetesi kuwa baadhi ya mawakala wa vyama vya upinzani huwa wanapewa shinikizo la kupewa pesa ili kukubali matokeo ya kura yageuzwe kwenye baadhi ya vituo. Sijui hii ni kweli?.... Wadau mna info kuhusu hili?
4. Kwenye Uchaguzi uliopita wa Marekani, watu wa kujitolea (volunteers) walikuwa wakipita nyumba hadi nyumba kuulizia kama watu wamejiandikisha kupiga kura na kuwahamasisha kupiga kura kwa wagombea wao. Tz je? hakuna hiyo. Wanasubiri watu wawafuate viongozi kwenye mikutano ya hadhara.
Kusema labda Mwalimu angejitoa CCM siyo issue hapa. Hapa watu waangalie the way forward.
CCM haitaki katiba mpya,na as long as wao ni majority Bungeni hakuna Katiba mpya.
Chadema inaelekea hawataki ushirikiano wa kuachiana majimbo na wenzao. Wao
waliachiwa na CUF kule Kiteto na Tarime, ila wao Chadema
wakagoma kuiachia CUF Mbeya vijijini na hata baada ya mgombea wao kuenguliwa wakawataka wafuasi wao wasiende kupiga kura. Wakaona afadhali jimbo lirudi CCM kuliko kwenda CUf, na ikawa hivyo.