Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
- Thread starter
- #61
Miaka 18 baada ya mfumo wa vyama vingi kuanzishwa bado watu wako busy kujisajili na CCM na sio vyama vingine vya upinzani, kwanini?je kuna dalili za vyama vya upinzani kujirekebisha ili kuondokana na hali hiyo? na je tukate tamaa kwa kuwa hakuna muelekeo wa kuiangusha CCM kwa sasa?...la hasha.
Tusiwasingizie wananchi katika hili, wananchi wapo tayari na wana hamu ya mabadiliko lakini vyama vya upinzani havijafanya vya kutosha kuweza kuchukua matarajio ya wananchi hawa na kuwajengea imani kuwa nchi itakuwa bora zaidi na salama mikononi mwao.
jamani hadi sasa CCJ imeshakusanya wanachama elfu 20! Hii ni kabla ya usajili wa kudumu na kabla ya uhamasishaji mwingine. Baadhi ya hawa wanatoka kwenye vyama vingine na wengine kwa mamia wanakuja wakiwa hawana chama bali sasa hatimaye wamepata chama ambacho kinaendana na hisia na matamanio yako kama Watanzania. Wapo wanaojiunga CCM, wapo wanaojiunga CHadema na CUF na wapo wanaojiunga na watakaojiunga na CCJ. Ndio uzuri wa demokrasia.