Biashara ya samaki

Wakuu, natamani na tayari nimepata mtaji wa kusafirisha samaki toka Mwanza kwenda Arusha ila nahitaji msaada wa jinsi ya kuanza na masoko ya huko Arusha, tafadhali naombeni msaada
 
Ilo mbona rahisi kama una samaki za kutosha pitia migahawa na hotel zote kusanya oda.Pia pitia kwa hakina mama wanaouza samaki kusanya oda.

Usisahau kuacha na kuchukua mawasiliano ili muwe mnatafutana samaki zikifika.

Samaki zinalipa sana ila uwe serious na uwe na lugha nzuri kwa wateja bila kusahau utimize ahadi kwa wakati na usiuze samaki wabovu.

Fata niliyokwambia utafanikiwa
 
NI WAZO ZURI, SONGA MBELE
Ni wazo zuri mkuu songa mbele. Ila jitahidi ujue ni samaki ya aina gani utakuwa unapeleka kutoka Mwanza kwa sababu samaki aina ya sangara ni bei kubwa sana mwanza kwa sababu ya kuwepo kwa viwanda, so wasi wasi wangu usije ukawanunua then ukienda kuuza wananchi wako wakaona ni bei kubwa. Jaribu kuangalia samaki aina ya sato na wengine ila sangala fikiria mala mbili kabla ya kuuza.

Kama utakuwa unanunua Mwanza tafuta ofisi weke frige na kuwa unakusanyia mzigo hapo hata kwa muda mfupi. Jambo lingine jitahidi kujiridhisha na usafiri wa kudumu. Haya malori hayafai kabisa yameisha tia watu hasara. hata samaki wakiwa wamekaushwa gari ikiharibika usababisha hasara sana. Ila hizo ni changamoto ambazo ukizijua mapema ni vyema kuzitafutia ufumbuzi haraka.

Kama utapata soko zuri za sangala uko arusha, kumbuka sangala mwanza anakuwa na thamani kwa vitu vikuu viwili.

Kwanza mnofu kwenye viwanda na pili ndani ya sangala tumboni kuna kitu wanaita bondo sijajua kama ni kiswahili au la ila nimezoea kusikia wanaita hivyo, hii kitu ni hela sana kwa sangala alie mkubwa. watu wa Arusha usiwauzie na hilo bondo litoe na ukaliuze Mwanza kwa Wachina hela nzuri.

Nahisi usingize ngoja nilale nitakupa data kesho tena.
 
ni wazo zuri mkuu songa mbele. ila jitahidi ujue ni samaki ya aina gani utakuwa unapeleka kutoka mwanza. kwa sababu samaki aina ya sangala ni bei kubwa sana mwanza kwa sababu ya kuwepo kwa viwanda. so wasi wasi wangu usije ukawanunua then ukienda kuuza wananchi wako wakaona ni bei kubwa. jaribu kuangalia samak aina ya sato na wengine ila sangala fikiria mala mbili kabla ya kuuza.

Kama utakuwa unanunua mwanza tafuta ofisi weke frige na kuwa unakusanyia mzigo hapo hata kwa muda mfupi. jambo lingine jitahidi kujiridhisha na usafiri wa kudumu. haya malori hayafai kabisa yameisha tia watu hasara. hata samaki wakiwa wamekaushwa gari ikiharibika usababisha hasara sana. ila hizo ni changa moto ambazo ukizijua mapema ni vyema kuzitafutia ufumbuzi haraka.

Kama utapata soko zuri za sangala uko arusha, kumbuka sangala mwanza anakuwa na thamani kwa na vitu vikuu viwili.
kwanza mnofu kwenye viwanda na pili ndani ya sangala tumboni kuna kitu wanaita bondo sijajua kama ni kiswahili au la ila nimezoea kusikia wanaita hivyo, hii kitu ni hela sana kwa sangala alie mkubwa. watu wa arusha usiwauzie na hilo bondo litoe na ukaliuze mwanza kwa wachina hela nzuri.

nahisi usingize ngoja nilale nitakupa data kesho tena

Well said mkuu...
 
Wakuu, nashukuru kwa michango yenu ila samaki ninaotaka kupeleka ni sangara wakuu maana hao sato ni ghali sana
 
Wakuu, nashukuru kwa michango yenu ila samaki ninaotaka kupeleka ni sangara wakuu maana hao sato ni ghali sana

Sangara hasa ndo wanatoka sana kwa A twn lakini ni vizuri ukasafiri na kufanya japo utafiti usio rasmi ili kwenda kujionea hali ya namna wanavyokutana wauzaji(kama utakavyokuwa wewe) na wanunuaji (wateja wanaochukua mzigo toka kwako ).Binafsi nimekuwa nikiona hamna utaratibu wa kuwa na order wala nini,huwa naona inaingia gari na mzigo inazungukwa na kinamama (wanunuzi) wanachukua mzigo kadiri ya uwezo wao then wanasambaa kwenda mtaani ambapo kila mtu anachuuza kwa watu wake maisha yanaendelea.(Hii hasa ipo soko la Kirombero )
Cha msingi ni kupata connection na wanaofanya biashara hiyo ili msiingize mzigo kwa pamoja na hasa unapokuwa mgeni.

Kwa sato nafikiri ndo wanaenda kwa Order kwa wenye hoteli na mabucha ya samaki(Hasa Soko Kuu ).
 
PACKAGE NZURI NA MTINDO WA DELIVERY NI MUHIMU
Wazo zuri ndugu, kama walivyopita washauri wengine. Kwanza unatakiwa utembelee eneo husika na kuangalia uhitaji gharama za usambazaji, pia kwa ushauri wangu kwa kuwa arusha ni jiji kubwa package yako na deliver transit inabidi iendane na mandhari ya sehemu unayopeleka, e.g serena hotel uki delivery kwa head hiyo ni soo. Usafi ni kitu muhimu katika biashara ya chakula. ili ufanye biashara yenye tija obseve this.

1. Tafuta sare yako ili uonekane uko serious na kazi yako
2. Kama una usafiri hata (pikipiki yenye refrigerator) kwa ajiri ya ku distribute orders
3. Kumbuka utahitaji watu wa kukusaidia ili kuendana na mda wa order husika
4. Je, utakuwa unauza kwa jumla au reja reja

All the best.
 
Wakuu, natamani na tayari nimepata mtaji wa kusafirisha samaki toka Mwanza kwenda Arusha ila nahitaji msaada wa jinsi ya kuanza na masoko ya huko Arusha, tafadhali naombeni msaada

ulishaanza kusafirisha?. ntafute kwa 0767 465147 nko arusha nafanya biashara ya SATO kwa saidi ya miaka 5, na nahitaji mtu wa kuniletea
 
Habari wana jf

mimi ni mwenyeji wa mwanza ambaye kwa sasa naishi Singida, biashara ya samaki kutoka mwanza nimeona ni biashara inayoweza kufanya vizuri kulingana na maeneo ninayokaa, naomba kufahamishwa , ni kwanamna gani naweza kusafirisha samaki aina ya sangara na sato wabichi tokea mwanza hadi singida!! naombeni pia wazoefu wa kada hii mnipe uzoefu! Naomba kuwasilisha.
 
Mkuu ni bonge la idea ila fuata ushahuri wa wadau hapo juu utafanikiwa mnooo,

Binafsi nina wazo kama hilo ila nataraji kuifanya Dar es Salaam, nimeplan iwe formal business, kwa maana ya kusajiri kabisa company ya general supply pamoja na business licence, na kutafuta order kwenye big hotels & supermarkets hapa town, changamoto niliyonayo ni kwenye vifungashio bado sijajua ni wapi nitaweza pata vifungashio murua kabisa maana kwenye hii biashara packaging ni swala la msingi sana... nimependa pia wazo la mdau mmoja hapo juu la kuwa na sare kabisa....
kwa wenye uzoefu kwenye hili swala la packaging au value addition technique yoyote please unaweza share nasi...

Natanguliza shukrani.
 
Pamoja na maelezo mhimu ya King, na kwakuwa nipo kwenye mchakato wa kuanzisha hii biashara naomba niongezee kidogo. Mimi nategemea kuifanya katika kwa kiwango cha kati na hivyo wateja wangu wakuu nitategemea mahotel na watu wa kipato cha kati na siyo mama lishe. Mambo makuu ninayoyafikiria ni haya
  • Jina la kampuni linalofanana fanana na chakula-nitakuwa na matawi mikoa mitatu (Dodoma, Arusha, Dar)
  • Location ya biashara-nafikiria iwe kwenye junction kama mwenge kwa Dar
  • Means of Transportation-Nitakuwa na gari kubwa ya freezer kwaajiri ya kusafirishia kutoka Lake zone na kupeleka Arusha, Dar then Dodoma kabla haijageuza kurudi Lake Zone.
  • Nitakuwa na Gari ndogo kila centre kwaajili ya kusambaza kwa wateja wa kudumu kama wenye hotel na mashule.n.k
  • Nitakuwa na Deep freezer kwa kila kituo.
  • Nitakuwa na standby Generator kukabiliana na changamoto za TANESCO kwa kila kituo
  • Nitatengeneza machinjio ya kisasa-hii ni plan ya baadae baada ya kupata shamba la kutunzia mifugo
  • Nitakuwa na shamba la mifugo ambayo ndiyo malighafi yangu
  • Nitakuwa na kituo cha kukusanyia samaki hapo Mwanza-Natafuta mtaalam wa kutengeneza Coldroom
  • Bidhaa nitakazoanza nazo ni-Nyama ya Ng'ombe, Mbuzi, Kondoo. Kuku wa kisasa na kienyeji, Samaki aina ya Sato na Sangara, Lakini pia nitakuja na mchele kwa Arusha na Dodoma......tayari nina 100bags za kuanzia na nipo nafunga mshine ya kisasa ya kukoboa na kubangua mchele na kufunga 5, 10. 15, 20kg
  • Project to start in June 2014.

Tafadhali mawazo yenu. Nipo tayari kulipa gharama za Busness Plan ila kwa mtu mwenye input ya maana.
Habari mkuu, ulishaanza Biashara yako?
 
Nahitaji kufanya biashara ya kuuza samaki in large scale.

Yaani mfano kama kusafirisha kilo 100 hadi 1000 kutoka Mwanza hadi Dar,

Mwenye ujuzi na hii biashara anishauri
 
Haya watu wanaspea kuleta mrejesho.

Hembu mliopo Mwanza.
Niambieni kunasifisha SATO na SANGARA kwa ufupi samaki kuja huku Zanzibar kwa Ndege,ita cost kiasi gani.

Yaani nipeni mchanganuo wa gharama kwa kilo,na pia gharama za usafiri kwa ujumla wake.

Nafikiria kuanzisha hii biashara ila bado nasita kwanza,maana Direct flight kutoka Mwanza Kuja Zanzibar ni issue.Ila wazoefu mnajua hizi connections na gharama zake.

Haya tujuzane
 
Haya watu wanaspea kuleta mrejesho.

Hembu mliopo Mwanza.
Niambieni kunasifisha SATO na SANGARA kwa ufupi samaki kuja huku Zanzibar kwa Ndege,ita cost kiasi gani.

Yaani nipeni mchanganuo wa gharama kwa kilo,na pia gharama za usafiri kwa ujumla wake.

Nafikiria kuanzisha hii biashara ila bado nasita kwanza,maana Direct flight kutoka Mwanza Kuja Zanzibar ni issue.Ila wazoefu mnajua hizi connections na gharama zake.

Haya tujuzane

Samahani hivi wewe unajishughulisha na nini?maana kila kitu wakitaka weye..
Samahani nahisi kama weye janjajanja tu kupoga stori humu
 
Wana forums,

Naomba msaada wa taratibu na kanuni za kuanzisha biashara ya samaki wabichi ukiacha wale wa kutembeza.
 
Back
Top Bottom