Tujifunze na Kuanza Utamaduni Huu Mpya wa Ufugaji Samaki

Madear

Member
Feb 13, 2020
45
107
Ni kawaida sana kuona watu wakifuga kuku, ng'ombe, mbuzi, nguruwe, n.k. Lakini ni nadra sana kuona watu wakifuga samaki licha ya kuwa mazingira yetu yanafaa sana kwa shughuli za ufugaji samaki kutokana na kuwepo kwa maeneo yenye maji ya kutosha na hali nzuri ya hewa. Baadhi ya mataifa kama China na Misri kufuga samaki imekuwa utamaduni wao na hadi leo wamefanikiwa sana kwenye hii sector.

Kadri miaka inavyozidi kwenda samaki wanazidi kupungua kwenye vyanzo vya asili (ziwani, baharini na mitoni) Hii ni kutokana na ongezeko la watu hali inayopelekea samaki kuvuliwa kupita kiasi ili kukidhi mahitaji ya watu bila kutoa muda wa kutosha wa samaki kuzaliana.

Matokeo yake ni upungunguvu mkubwa wa samaki kwenye vyanzo vya asili na ufugaji wa samaki ndio unaonekana kama njia mbadala ya kuzalisha samaki wengi ili kukidhi mahitaji ya watu.

Haya mazingira yanafanya tuone ufugaji wa samaki ni fursa nzuri sana ya kujiinua kiuchumi, rafiki kwa mazingira na ianaweza kumaliza/kutatua tatizo la uhaba wa samaki hususani samaki wa maji baridi, hapa naongelea samaki pendwa Sato.

Huu ni wakati sahihi kwa mtu mmoja mmoja na jamii kwa ujumla kujifunza utamaduni huu mpya wa kufuga samaki kwenye mazingira yetu kama njia ya kujiongezea kipato, kutunza mazingira, kutumia resources zetu vizuri na pia ufugaji wa samaki ni njia nzuri ya kupunguza msongo wa mawazo kuona tu samaki wanavyofanya manuvering ni burudani tosha

Kunanjia nyingi rahisi za kufanya ufugaji samaki kama vile kwa kutumia mabwawa, matanki au vizimba. Sio raziama ufanye uwekezaji mkubwa unaweza kujenga kibwawa kidogo tu au ukafugia kwenye tanki hapo kwako na ukawa unajipatia kitoweo (Sato fresh kabisa) au unaweza kufuga samaki na kulima bustani kwa wakati mmoja, badala ya kumwaga maji yaliyochafuka wakati wa kufuga samaki wewe unaweza kuyatumia maji hayo yenye mbolea kumwagilia bustani, ukaboresha kilimo chakona kikawa chenye tija





 
Naomba kufahamu gharama za kawaida za kuseti tank la kufugia pamoja
122862C3-439B-48F6-A7ED-DCE7360FAE82.jpeg
 
Gharama kwa system kama hii haipo constant inategemea na mazingia unapochukulia materials ila wastani ni Tsh 300,000 hadi 500,000. Hii inajumlisha gharama zote kuanzia tank, pvc pipe, filter n.k
Asante, vipi hilo dumu moja linafuga samaki wa ngapi?
 
Asante, vipi hilo dumu moja linafuga samaki wa ngapi?
Hapa unaweza kuweka samaki 100.
Kiasi/idadi ya samaki sio constant, idadi ya samaki inategemea vitu viwili ujazo wa maji na inategemea na uwezo wako wa kudhibiti ubora wa maji, hivi kwa pamoja ndio vita determine uweke idadi gani ya samaki

Sishauri sana matumizi ya tank, nashauri zaidi njia ya bwawa ndio nzuri kwa sababu inakupa nafasi ya kuweka samaki wengi. Lakini kwa tank ili uweke samaki wengi zaidi itakulazimu uwe na filter kwa ajili ya kukusaidia kudhibiti ubora wa maji
 
Hapa unaweza kuweka samaki 100.
Kiasi/idadi ya samaki sio constant, idadi ya samaki inategemea vitu viwili ujazo wa maji na inategemea na uwezo wako wa kudhibiti ubora wa maji, hivi kwa pamoja ndio vita determine uweke idadi gani ya samaki

Sishauri sana matumizi ya tank, nashauri zaidi njia ya bwawa ndio nzuri kwa sababu inakupa nafasi ya kuweka samaki wengi. Lakini kwa tank ili uweke samaki wengi zaidi itakulazimu uwe na filter kwa ajili ya kukusaidia kudhibiti ubora wa maji
tatizo ni eneo la kuchimba bwawa huku mjini ni shida, mimi nyumbani kwangu kuna space kubwa tuu ya kuweka hizo mobile fish pond.
Naomba kuuliza kwa mfano nikaagiza kila kitu kwa ajili ya hizo mobile fish pond kila kinachohitajika kutoka china je installation unaweza kufanya?, na vipi samaki hawana changamoto za magonjwa kama kuku?
A17B3F08-E941-483B-8E7F-65E2AE6379C6.jpeg
 
Ni kawaida sana kuona watu wakifuga kuku, ng'ombe, mbuzi, nguruwe, n.k. Lakini ni nadra sana kuona watu wakifuga samaki licha ya kuwa mazingira yetu yanafaa sana kwa shughuli za ufugaji samaki kutokana na kuwepo kwa maeneo yenye maji ya kutosha na hali nzuri ya hewa. Baadhi ya mataifa kama China na Misri kufuga samaki imekuwa utamaduni wao na hadi leo wamefanikiwa sana kwenye hii sector.

Kadri miaka inavyozidi kwenda samaki wanazidi kupungua kwenye vyanzo vya asili (ziwani, baharini na mitoni) Hii ni kutokana na ongezeko la watu hali inayopelekea samaki kuvuliwa kupita kiasi ili kukidhi mahitaji ya watu bila kutoa muda wa kutosha wa samaki kuzaliana.

Matokeo yake ni upungunguvu mkubwa wa samaki kwenye vyanzo vya asili na ufugaji wa samaki ndio unaonekana kama njia mbadala ya kuzalisha samaki wengi ili kukidhi mahitaji ya watu.

Haya mazingira yanafanya tuone ufugaji wa samaki ni fursa nzuri sana ya kujiinua kiuchumi, rafiki kwa mazingira na ianaweza kumaliza/kutatua tatizo la uhaba wa samaki hususani samaki wa maji baridi, hapa naongelea samaki pendwa Sato.

Huu ni wakati sahihi kwa mtu mmoja mmoja na jamii kwa ujumla kujifunza utamaduni huu mpya wa kufuga samaki kwenye mazingira yetu kama njia ya kujiongezea kipato, kutunza mazingira, kutumia resources zetu vizuri na pia ufugaji wa samaki ni njia nzuri ya kupunguza msongo wa mawazo kuona tu samaki wanavyofanya manuvering ni burudani tosha

Kunanjia nyingi rahisi za kufanya ufugaji samaki kama vile kwa kutumia mabwawa, matanki au vizimba. Sio raziama ufanye uwekezaji mkubwa unaweza kujenga kibwawa kidogo tu au ukafugia kwenye tanki hapo kwako na ukawa unajipatia kitoweo (Sato fresh kabisa) au unaweza kufuga samaki na kulima bustani kwa wakati mmoja, badala ya kumwaga maji yaliyochafuka wakati wa kufuga samaki wewe unaweza kuyatumia maji hayo yenye mbolea kumwagilia bustani, ukaboresha kilimo chakona kikawa chenye tija


View attachment 2771187
View attachment 2771188
View attachment 2771189
View attachment 2771190
Aisee hivi,utengenezaji wa bwawa la kawaida unaweza kugharimu tsh ngapi?

Na vipi kuhusu yale mabwawa yanayowekwa ksratasi yanadumu kwa mda gani?
 
tatizo ni eneo la kuchimba bwawa huku mjini ni shida, mimi nyumbani kwangu kuna space kubwa tuu ya kuweka hizo mobile fish pond.
Naomba kuuliza kwa mfano nikaagiza kila kitu kwa ajili ya hizo mobile fish pond kila kinachohitajika kutoka china je installation unaweza kufanya?, na vipi samaki hawana changamoto za magonjwa kama kuku?View attachment 2772003
Ndio kufanya installation inawezekana, samaki awahitaji chanjo kama kuku ni nadra sana kuona samaki wameugua
 
Aisee hivi,utengenezaji wa bwawa la kawaida unaweza kugharimu tsh ngapi?

Na vipi kuhusu yale mabwawa yanayowekwa ksratasi yanadumu kwa mda gani?
Gharama inategemea na size, ulitaka bwawa lenye mita za mraba ngapi Mkuu?

Ukitunza vizuri lina uwezo wa kudumu zaidi ya miaka 5, uimara unategemea na thinkness ya hiyo nylon, kuna 0.5mm, 1mm na 1.5mm

Bei yake ni Tsh 7,500/m²
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom