Elungata
JF-Expert Member
- Jan 28, 2011
- 40,205
- 33,224
Maswali haya hayajajibika, kabisa.Team Watafutaji
Kama title inavyosema hapo juu, naomba kufahamu hii biashara kwa undani kidogo, yaani recently tuliambiwa kuwa kwa kipindi hiki cha miaka mitano samaki wetu wameongezeka urefu/ukubwa.
Sasa basi nikawa interested kufahamu kama mtu anaweza kununua samaki (Sato/Sangara) kutoka kwa Wavuvi in bulk na kuziuza kwa makampuni ambayo tumeambiwa wanasafirisha kwenda nje ya nchi moja kwa moja.
Au kuanza kuvua na kuuza moja kwa moja kwa haya makampuni badala ya kununua kama middleman.
Moja, je ni changamoto gani kubwa zipo kwenye hii sekta?
Pili, upatikanaji wa vibali ukoje!?
Tatu, je hivi viwanda vinanunua hao samaki kwa mfumo gani? Cash on delivery au on credit?
Nne, je mtu anaweza kuingia mkataba na hivi viwanda ili kuwa-supply mzigo?
Tano, ni fursa gani (fursa ndani ya fursa) zinaweza kupatikana kwenye hii biashara?
Sita, modality yao (kama ipo), ipoje? Je wanaweza kukudhamini vifaa ili mzigo uwapelekee wao na kukatana kidogo kidogo?
Saba, ni viwanda (kwa majina) vipo kati ya Mwanza, Bukoba na Musoma au around maeneo hayo ambao wanaweza kupokea mzigo?
Nane, je upatikanaji wa samaki una msimu? High season na low seasons?
Maswali yangu hayajakaa kwa mtiririko maalum hivyo tusaidiane tu kadiri tutakavyoona inafaa.
Kwa hili tutaweza kusaidiana na kuwasaidia vijana wetu/wenzetu pia