Biashara ya samaki

Team Watafutaji
Kama title inavyosema hapo juu, naomba kufahamu hii biashara kwa undani kidogo, yaani recently tuliambiwa kuwa kwa kipindi hiki cha miaka mitano samaki wetu wameongezeka urefu/ukubwa.

Sasa basi nikawa interested kufahamu kama mtu anaweza kununua samaki (Sato/Sangara) kutoka kwa Wavuvi in bulk na kuziuza kwa makampuni ambayo tumeambiwa wanasafirisha kwenda nje ya nchi moja kwa moja.

Au kuanza kuvua na kuuza moja kwa moja kwa haya makampuni badala ya kununua kama middleman.

Moja, je ni changamoto gani kubwa zipo kwenye hii sekta?

Pili, upatikanaji wa vibali ukoje!?

Tatu, je hivi viwanda vinanunua hao samaki kwa mfumo gani? Cash on delivery au on credit?

Nne, je mtu anaweza kuingia mkataba na hivi viwanda ili kuwa-supply mzigo?

Tano, ni fursa gani (fursa ndani ya fursa) zinaweza kupatikana kwenye hii biashara?

Sita, modality yao (kama ipo), ipoje? Je wanaweza kukudhamini vifaa ili mzigo uwapelekee wao na kukatana kidogo kidogo?

Saba, ni viwanda (kwa majina) vipo kati ya Mwanza, Bukoba na Musoma au around maeneo hayo ambao wanaweza kupokea mzigo?

Nane, je upatikanaji wa samaki una msimu? High season na low seasons?

Maswali yangu hayajakaa kwa mtiririko maalum hivyo tusaidiane tu kadiri tutakavyoona inafaa.

Kwa hili tutaweza kusaidiana na kuwasaidia vijana wetu/wenzetu pia
Maswali haya hayajajibika, kabisa.
 
Wakuu,
Mimi ninafikilia kuanzisha Kampuni yangu, nataka kununua samaki Mwanza kutoka kwa wavuvi, niwakaushe kwa Oven na kuwakaanga kwa kutumia Air fryer alafu niwa pack kwenye package moja moja ,kwa mfano, Sato mmoja awe kwenye package yake na dagaa fungu la Tsh 5000, 2000 nk alafu nipeleke super market na madukani

Swali langu sasa kwenu, je biashara hii italipa ? Je mna ushauri wowote wa kuborosha hili wazo langu ? .kwa kifupi ni mnanishauri nini juu ya hili wazo ?

Oven na Air fryer naweza kununua,
N.B
Target yangu ni mkoa wa Arusha, Singida, Dodoma na wilaya ya Moshi
 
Wakuu,
Mimi ninafikilia kuanzisha Kampuni yangu, nataka kununua samaki Mwanza kutoka kwa wavuvi, niwakaushe kwa Oven na kuwakaanga kwa kutumia Air fryer alafu niwa pack kwenye package moja moja ,kwa mfano, Sato mmoja awe kwenye package yake na dagaa fungu la Tsh 5000, 2000 nk alafu nipeleke super market na madukani

Swali langu sasa kwenu, je biashara hii italipa ? Je mna ushauri wowote wa kuborosha hili wazo langu ? .kwa kifupi ni mnanishauri nini juu ya hili wazo ?

Oven na Air fryer naweza kununua,
N.B
Target yangu ni mkoa wa Arusha, Singida, Dodoma na wilaya ya Moshi
Umeambiwa hiyo mikoa haiwezi fanya hivyo?

Samaki pelekea mbichi akiwa kaganda
 
Umeambiwa hiyo mikoa haiwezi fanya hivyo?

Samaki pelekea mbichi akiwa kaganda
Kwa utafiti wangu niliofanya, hapa Tanzania kuna watu wachache wanaofanya hiyo biashara na wanauza dagaa tu kwenye package, hakuna kampuni / mtu anauza samaki wa kukaanga kwenye supermarket mikoa hiyo.

Asante pia kwa ushauri kuhusu kuuza samaki fresh, nimeifikilia pia hii, lakini mimi nilivowaza ni kuwauza hao samaki walioganda wakiwa kwenye package na wateja wangu wawe ni Hotels na supermarket

Je, wewe katika wazo ulilonipa la kupeleka samaki walioganda unadhani Targeted customers ni wapi ?
 
Kwa utafiti wangu niliofanya, hapa Tanzania kuna watu wachache wanaofanya hiyo biashara na wanauza dagaa tu kwenye package, hakuna kampuni / mtu anauza samaki wa kukaanga kwenye supermarket mikoa hiyo.

Asante pia kwa ushauri kuhusu kuuza samaki fresh, nimeifikilia pia hii, lakini mimi nilivowaza ni kuwauza hao samaki walioganda wakiwa kwenye package na wateja wangu wawe ni Hotels na supermarket

Je, wewe katika wazo ulilonipa la kupeleka samaki walioganda unadhani Targeted customers ni wapi ?
Samaki sio Dagaa
 
Kwanza inatakiwa ujue ni aina gani ya samaki (kuna sangara na sato kanda ya ziwa bila kusahau kamongo na kambale) Kuhusu pwani sijui sana

Soko umeshasema ni uhakika sasa kazi imebaki ni wapi utawapata hao samaki, mimi pia najihusisha na hii biashara kiukweli inalipa

Kama upo kanda ya ziwa unaweza kunicheki tukabadilishana ujuzi
@mjusi kafiri
 
Back
Top Bottom