Biashara ya Kuuza Nyama (Butcher's Shop): Mambo Mbalimbali ya Kujifunza

1.Nikupe hongera kwanza kwa kutaka kujiajiri ila nikupe dokezo na Tahadhari hapo kwa usimamizi lazima mwenyewe uwepo nikimaanisha uwe na usimamizi wa karibu zaidi.

2. Kuhusu nyama nunua tu vingunguti ama ukonga km unaishi Dar es salaam kg machinjion 4,500 mpaka 5,000 unaweza pata connection na gari yaan wasambazaji nyama kwa gari wakakuletea mpaka ulipo.

Kwa upande wa samaki nenda ubungo River side sato kg 8,000 na sangara 4,500 kwa kg km ukizoea utapata connection ya wauzaji wanaoleta mojakwamoja huwa wanauza Sato 5,500 sangara 4,000 note hizi bei ni za jumla rejareja Sato 10,000 kwa kg na Sangara 8,000 nyama rejareja 6,000 sehemu zengine 7,000

3. Ushindani sio mkubwa ila vyema ukawa na Machine ya kukatia nyama, ofisi layout iwe nzuri, Muuzaji awe mchangamfu hapo utakuwa umewapa pigo washindani wako

4. Faida nafikiri ushajua kwa nyama faida 1,000 kwa kg kwa samaki Sato ni 2,000 km unanunua riverside sangara 3,500 kwa kg Hasara zipo nazinakuja kutokana na miundo mbinu ukikatika umeme jua nimaafa

5. Changamoto zipo nyingi sana kwanza ukikosea kuchagua eneo yaani ukifail kuchagua location ya ofisi yahiyo butcher basi jua ni hasara kwenda mbele, Pili wauzaji sipendi kuongelea vibaya watani wangu wagogo ila usije kumueka Mgogo buchani kwako kama huna usimamizi wa karibu atakufilisi nasema tena atakufilisi kuepuka hilo tafuta machine unaweza weka yoyote akauza. Usinambie kama nafanya lahasha namuona Kaka angu anavoendesha

Kama wewe ni mgogo utanisemehe jamani
Samahani mkuu kama hutojali.Hao Samaki Kwa bei ya jumla ni river side maeneo gani!wanauza kuanzia kg ngapi mi nataka Kwa matumizi ya nyumbani.
 
Samahani mkuu kama hutojali.Hao Samaki Kwa bei ya jumla ni river side maeneo gani!wanauza kuanzia kg ngapi mi nataka Kwa matumizi ya nyumbani.
Ubungo External kuanzia kg 5 Sangara 4,500 Sato ni 8,000 ila kuanzia kg 5 ndo utaweza nunua ukishuka kituoni ulizia na River side ile barabara km yaendea Mabibo.
 
Nimeanza biashara hiyo mwez uliopita,mm nipo mkoani huku unachinja Ng 'ombe mzima peke yako kikubwa unakua na bucha zaidi ya moja za kuuzia,unatundika kiasi kiasi unatunza kwny friza mapema kabla haijakaa muda mrefu, unamalizia siku ya pili kuuza nyama inakua km ya leo.kikubwa usikosee kwny bei ya kununulia mnyama. Faida laki au 80 baada ya siku mbili ni kawaida

Habari,

Mkuu samahani kuna text nimekutumia inbox kama utakuwa na uelewa nayo naomba unisaidie please.
 
Hii biashara intofautiana mkoa kwa mkoa, na hali ya kipato kwa wananchi wa eneo husika unalouzia
 
Ubungo External kuanzia kg 5 Sangara 4,500 Sato ni 8,000 ila kuanzia kg 5 ndo utaweza nunua ukishuka kituoni ulizia na River side ile barabara km yaendea Mabibo.
Mwambie pemben yake kuna pub flan jina nimesahau afu kuna shule kwa upande kama ukiwa unatokea mabibo hapo wauzapo samaki kwa mbele yake zaman kuna vifaa vya matrecta vilikuepo sjiu kwa sasa niko mkoani.
 
We utawasafilisha kwa njia gani wasihalibike kutoka huko na utanzià kwa kiasi gani
 
Mwambie pemben yake kuna pub flan jina nimesahau afu kuna shule kwa upande kama ukiwa unatokea mabibo hapo wauzapo samaki kwa mbele yake zaman kuna vifaa vya matrecta vilikuepo sjiu kwa sasa niko mkoan
Shule ni atlas, opposite na azania kiwanda cha unga
 
Habari zenu wadau, kwa wajuzi na wataalam wa biashara ya bucha naombeni kujuzwa bei ya vifaa vifuatavyo.

1. Mashine ya kisasa ya kukatia nyama
2. Vyuma vya kuning'inizia nyama
3. Mizani ya kisasa
4. Freezer kubwa

Kama kutakuwa na vifaa vingine vinavyohitajika naomba mnijuze na gharama zake nataka nianze rasmi mwakani hii biashara.

Naombeni ushirikiano wenu
 
Back
Top Bottom