Chamoto
Platinum Member
- Dec 7, 2007
- 9,856
- 22,191
Nilikuambia huyu Captain nimemuonea Youtube, sasa nitaongea nini kwa kitu ambacho sina taarifa?Kaka nimekupatia code nyingi sana ili uweze kuzielewa. Nilikuuliza swali, umewahi kuwaza kuwa Captain Tesha yupo wapi? Nikauliza kwanini hatufikirii kuhusu huyo jamaa?
Nililiongea jana hili.Sikumbuki kama ni wewe ulisema Serikali ipo na wajibu wa kulinda raia. Sikutaka tena kuendelea na ku decode encryption. Maana vitu vyote vipo wazi na ushahidi.
Kuhusu huyu msaidizi, mi sina ishu, na nilielewa toka jana kuhusu hayo mambo ya satellite images na hata ulinzi wa kimtandao.Ndio maana kiongozi wa juu kabisa yaani msaidizi wa Putin alitumwa kuja Tanzania.
Urusi wapo na satellites angani wanaona movements zote zinazoendelea.
Ukisoma comments zangu za juzi utaona nimegusia kuhusu Kagame, na sababu za wao kutumia fursa ya tensions zetu za ndani.Jana CDF wa Kenya wamekutana na CDF wa Rwanda baada ya mimi kuweka uzi kuhusu PAKA na ujio wa Russia.
Unganisha dots kaka, we are in war with Kenya and Rwanda. Hizi kwenye media ni prompts to kutengeneza sababu.
Kenyan media wanapiga kelele kuhusu raia wao wameuawa nchini Tanzania, na wengine wamekamatwa, so wanataka kutengeneza vikundi vya kigaidi kwa kisingizio kuwa wanakuja kuwaokoa ndugu zao.
Hili la media za Kenya nilishalisoma, nguvu inayotumika ni kubwa mno (it's unnatural), lina footprints zote za the usual suspect, hata kipindi cha Magufuli waliongea sana negatively about him, tofauti na sasa wametumika "independent media" zaidi kuliko legacy media.
Kuhusu Gwajima kufanya hivyo sijui ila ukiangalia yeye na CCM mtandao unaweza kuona Rostam anauwezo mkubwa na sababu ya kuweza kufanya hivyo zaidi ya Gwajima.Kaa mkao huo huo.
Minong'ono inasema Askofu Gwajima kipindi cha Lowassa (UKAWA) walipeleka mafunzo ya kijeshi vijana zaidi ya 200, walirudi nchini baadae. Vijana hao juzi kati walichukuliwa na inasemekana yalifanyika mafunzo ya vijana kama 500 huko kenya wakiungana na vijana hawa. Vijana hawa 200 wengine walikuwa kwenye vyombo vya ulinzi na usalama.
Katika maelezo yako yote hapa hujawahi kusema chochote kuhusu CCM mtandao, wala Kikwete na genge lake la kina Rostam, kwa nini huwa husemi chochote kuhusu hawa? Kwa nini huoni tatizo lao? Kikwete yupo kwenye serikali sasa kwa maslahi ya nani? Uhusiano wake na genge la akina George Soros pamoja na Klaus Schwab huoni kuna tatizo?Kuna rafiki yangu mmoja ambaye anauza sana kahawa pale magomeni mwembe chai alikuwa akitusimulia kwenye kijiwe cha kahawa, akasema kabla ya uchaguzi miamba hao 200 walipotea wengine hawaonekani kwenye vyombo vya ulinzi na usalama.
Mange kimambi na Maria Sarungi ni kama vichaa lakini wamekusanya taarifa nyingi mno maana adui zetu wamewaamini.
Uzuri hawa watu tumewazidi hatua nyingi sana kwenye mambo ya Intelligece.
Wao wanatumia Art of Deal Methodoloy sisi tunatumia Art of War Methodology
Art of Deal iliundwa na Trump yenye mbinu zake ni kupiga kelele sana na kujionesha wewe unanguvu, kumtisha adui yako ili aje kwenye meza ya mazungumzo na uweze dictate conditions.
But art of War unahakikisha adui yako unamjua zaidi na unajijua zaidi. Adui yako aone uko mbali kumbe wewe upo karibu mno, na aone upo karibu kumbe wewe upo mbali mno.
Ni hayo tu kaka yangu.
Mwaka jana kila nilipokuwa nagusia kifo cha Magufuli, ulikuwa unapotezea kana kwamba Magufuli alikuwa trator wa nchi ila hujawahi kuwasema vibaya Kikwete na CCM mtandano, kwa nini?