joto la jiwe
JF-Expert Member
- Sep 4, 2017
- 26,111
- 46,621
Mkuu, kuhusu mateja kukatazwa inatokana na kwamba biashara ya madawa ya Kulevya imepigwa marufuku duniani. Kabla ya hapo ilikua inafanyika Kama kawaida na watu walitumia, lakini baadae Dunia ilikubaliana kwamba kuuza na matumizi ya madawa ya Kulevya Kuna athari mbaya duniani(Usiniuliza ubaya gani kwasababu sikuwepo enzi hizo).Huo ni mfano halisia kabisa, lengo la kukataa uteja ni kutokana na athari zinazopatikana kwenye tabia hiyo, vivyo hivyo ushoga una athari kubwa kwa afya ya mwanadamu na ndiyo maana tunapinga ushoga, pia hata kimaadili sio sawa mwanaume kuingiliwa kinyume na maumbile sio tu mwanaume bali hata mwanamke sio vizuri kiafya.
Mkuu ngoja nikuulize swali la kizushi, hivi wewe uko ladhi mwanao aingiliwe kinyume na maumbile? Unajua tusiweke mijadala kwa minajili ya kuonekana tunashinda au kuonekana wazuri kwenye kujenga na kutetea hoja, je wewe ungefurahi mwanao kufanyiwa hivyo? Na kama hutofurahi kwnn usikemee japo kupunguza tabia hiyo?
Hatuwezi kumaliza tatizo lkn pia hatuwezi kukaa kimya tatizo linapotokea, ni lazima kupambana kulipunguza, Tanzania hairuhusu ushoga na ndiyo maana yule askari alipogundulika ni shoga alifukuzwa.
Kuhusu ushoga, ukiachana na maneno ya mitaani na Imani za kidini, hakuna ushahidi wowote wa kisayansi(Medical), unaotaja athari za ushoga ulkiacha athari za kawaida zitokanazo na tendo la "sex" ambazo pia hutokea kwa njia zingine(Vaginal).
Kwamba Mimi ninakubali au sikubali kuwa na mtoto au ndugu wa aina hiyo?. Sijui Kama jibu langu litakua na maana yoyote, kwasababu ninaweza Mimi nikawa sikubali, lakini kunao wale ambao wanakubali. Tunapaswa kuweka mazingira ambayo ni rafiki kwa Kila mtu, mwenye kukubali na asiyekubali ushoga
Sent from my itel L5007 using JamiiForums mobile app