tuusan
JF-Expert Member
- Jun 30, 2016
- 17,973
- 20,222
Pesa inayotengwa kwa ajili ya kukarabati na kujenga barabara kwa kiwango cha lami ni kweli kwa mwaka mkoja haitoshi, izo 500km ni mfuko wa barabara tu,lakini kuna miradi ya mikopo kama ule wa barabara ya masasi mtwara kipande cha mvinata 160Km ambazo walichukua pesa Bank ya maendeleo africa,Siridhidhwi na uwekezaji mdogo wa pesa kwenye barabara.Hii Nchi ni kubwa na Kila sehemu Kuna uhitaji mkubwa sana wa barabara lakini Kasi ni ndogo.
Nguvu inayotumika ku push sgr na bwawa la Nyerere ingetumika kwenye barabara Leo hii tungekuwa tunazungumzia uchumi unaokua kwa zaidi ya 10%.
But unfortunately kwa mwaka zinajengwa km chini ya 500 za lami za barabara kuu,za Tarura hasa Vijijini hata km 30 hazifiki.
Kuna miradi kama ya Tengeru moshi holili upanuzi wa barabara kua njia nne hela za mjapan,kuna miradi ya mwendokasi kutoka washirika,outer ring ya dodoma na miradi kadhaa ambayo haijatengewa fedha za ndani...
Ukijumlisha miradi inayoendelea kutekelezwa ni zaidi ya 1700Kms znajengwa kwa sasa kwa kiwango cha lami
