Wewe sidhani hata unaelewa ninachokisema, ni hivi nilikuwa naongelea double standard.
Hayo waliyokuwa wanawashutumu wachina, google wamekuwa wakifanya toka 1998. Google toka ilipoanza imekuwa wakiweka cookies kwenye computer zetu kwa miaka 30.
Hawakuishia hapo, wakawa wanagawa analytics codes kwa websites mbalimbali (ikiwemo JamiiForums) ili kutrack mienendo ya watu dunia nzima.
Bado hawakutosheka, wakaanzisha browser yao (chrome) ili kuwakamata wengi zaidi, mwisho fungakazi wakanunua android ili waweze kuwa na full control ya identity ya watumiaji (finger print, facial recognition, voice id, contacts and just about everything at their disposal).
Kama hujui, Google, Youtube, Facebook, Instagram, whatsapp vyote hivyo ni vyombo ya kiupelelezi. Ndiyo maana baadhi ya nchi makini wamezizuia hizi huduma.