Wakuu,
Wakati ndugu zetu wa Kenya wakimaliza uchaguzi kwa amani na kutoa funzo la hali ya juu sana kwa kuendesha uchaguzi kitaalamu sana huku kila mtu akijipakulia matokeo na kujumlisha bila shida hali ni hivyo hivyo kwenye miundombinu yao.
Kwakweli Nairobi iko mbali sana. Flyovers zao ni za kibabe sana! Huwezi fananisha na kale kadaraja ka kijazi tunakojitapa nako kila siku, Kule Thika superhighway ni balaa, miundombinu ya Nairobi ni kiwango cha Ulaya au China kabisa.
Hapa Dar zaidi ya vidaraja hakuna superhighway yoyote. Hivi tunakwama wapi?