Ukweli ni kwamba, Tanzania ndio chimbuko la SADC, bila Tanzania kusingekuwepo na SADC. SADC ni mtoto wa "Front line states", ambayo ndiyo iliyoongoza mapambano ya kuzikomboa nchi zote zinazounda SADC, ukiacha Lesotho, Zambia, Malawi na DRC, kiongozi wa hiyo "Front line states" alikua ni Nyerere na makao makua ni Dar.
Baada ya ukombozi kukamilika, Nyerere akasema nchi zote zilizokua zikipigania uhuru wa kisiasa ziungane kwa pamoja na kupigana uhuru wa kiuchumi, ndio ikazaliwa SADCC, ambayo baadae ikazaliwa SADC. Makao makua yalipendekezwa yabaki Tanzania, lakini Nyerere akasema yahamishiwe katika ya nchi wanachama wa SADC, ndio yakahamishiwa Botswana.
Kama ambavyo chimbuko la EAC ni Nyerere, hata chimbuko la SADC ni Nyerere (Tanzania). Tanzania ipo karibu zaidi na EAC "Geographically", lakini ni SADC by birth, spiritually, Faith, and Mentally.
Tatizo ni ninyi wakenya mnajaribu kutulazimisha tubaki EAC wakati Kenya na Tanzania hatuna historia yoyote ya mashirikiano zaidi ya mivutano na tofauti za kiitikadi, Kenya mnalazimisha Tanzania iegemee zaidi EAC kwasababu kuu mbili
1)Uchumi wa Kenya unategemea Sana "EAC"
2)Kenya Haina uwezekano wa kuomba kujiunga SADC kutokana na usaliti wenu kipindi cha Ukombozi kusini mwa Afrika
Summary;
Tanzania 80% SADC, and 20% EAC
Sent from my itel L5007 using
JamiiForums mobile app