Kuna siku nilikuwa Nairobi, nikaita uber kuelekea Airport, ikaja na dereva alikuwa dada mmoja, akanisalimia vizuri then baada ya kuketi kwenye gari, akaniuliza kwa Kiingereza chao chenye accent mbovu, you don’t look Kenyan, where do you come from? Nikamjibu kwa kiswahili, unahisi unaweza pata wapi accent nzuri kama hii ya Kiingereza na Kiswahili……?? Akacheka sana, kumbe wewe ni mTZ? Unatoka where all of our foods come from? Nikamwambia kwa utani “naam, na siku mkituletea za kuleta mtakuwa hamli hapa” huu utani ukamuingia alafu akaanza kufunguka namna Kenya imeoza na jinsi ambavyo land yao kidogo yenye rutuba badala ya kuzalisha chakula inazalisha maua na makorolokolo mengine ikiwaacha wakenya kibao na njaa sababu pia inamilikiwa na watu wachache.
Kiukweli niliwaonea sana huruma Wakenya hasa yule dada alivyoongea kwa uchungu, kidogo tu nimlipie nauli nimlete Bongo sababu alikuwa kaishakubali kuja kufanya hustles zake huku kama nikim-guarantee makazi ya muda na pa kuanzia. Tatizo hakuwa mzuri sana na haya mambo ya hisani wabongo tuliishaachana nayo baada ya ukombozi wa Afrika…….


Wakenya wako desperate sana aisee.