LDC kuna nn lakini
😀😀😀😀😀
26 billionares from different parts of the world visit Serengeti NP, Tanzania.
Jana tarehe 23.07.2017 Waziri wa Maliasili na Utalii Prof. Jumanne Maghembe aliwapokea Mbugani Serengeti Mabilionea 26 wakifuatana na wenzi wao (26) katika ziara yao ya siku 3 nchini Tanzania.
Mabilionea hao wa Club ya YPO (Young Presidents Organisation) wanatoka mabara yote duniani na wako katika ziara ya nchi 8, Uingereza, Rwanda, Tanzania, Maldeves, Nepal, Bhutan, Rajastan na nchi moja nyingine.
Katika hafla ya Chakula cha jioni alicho waandalia Wageni wake Prof. Maghembe aliwakaribisha Tanzania na Maajabu ya Dunia yaliyobebwa na hifadhi ya Taifa ya Serengeti. Alisisitiza "hakuna eneo lolote katika uso wa Dunia lenye mkusanyiko wa wanyama wanaokula majani (herbivores) na wale wanaokula nyama (canivores) kama Serengeti.
Aidha, Prof. Maghembe aliwaeleza Wageni wake kuwa kuhifadhi ni gharama kubwa inayobebwa na Tamzania kwa niaba ya Dunia. Hivyo akawaomba wageni wawe Mabalozi wa kuitangaza Tanzania kama Destinatiom ya amani yenye vivutio vyenye ubora wa pekee. Hatua hiyo italeta watalii wengi nakuiongezea Tanzania mapato.
Aidha, aliwaomba warudi tena kuwekeza nchini ili washiriki kwenye uchumi unaokuwa kwa wastani wa 7% kwa kipindi cha miaka 15 sasa.
View attachment 549391 View attachment 549392 View attachment 549393 View attachment 549394 View attachment 549395