Battle ya uzuri na wingi wa mabasi mgeipotezea tu maana tunawagaragaza. Mabasi yetu bongo ni more beautiful than yours. Pia ni mengi sana ikilinganishwa na ya kwenu. Hii ni kwa kuwa uchumi wa Tanzania umesambaa kila kona ya nchi hivyo miji ni mingi. Wingi wa miji unapelekea demand kubwa ya inter-city/upcountry transportation.
Ila; nasema ila!
Sisi wabongo tunalo somo kubwa sana la kijifunza kwenye hii battle ya mabasi. Wingi wa mabasi kutoka nje (Chinese buses) una madhara hasi kwenye sekta ndogo ya bus manufacturing/assembly.
Tuko chini sana kwenye uundaji mabasi in both terms of quality and quantity. Najua wapo producers wazuri wachache kama Dar Coach na JN Coaches ila tuwe macho na haya mabasi ya hawa rafiki zetu wa China.
Automobile assembling and manufacturing haihitaji mtaji kubwa sana bali ambition and planning. Mfano ni huyo mkali wa JFA assemblers aliyeanzisha assembling plant kwa tune ya below TZS 5bn na itagharimu 12bn mpaka kukamilika.
Hayati Reginald Mengi naye alikuwa kwenye mchakato na Foton Motors kabla ya umauti kumfika.
Kuna watu wetu kama akina Hanspaul wakiwezeshwa vizuri watatutoa kimasomaso.
Iko hivi. Viwanda vingi vya China "havizalishi" hayo mabasi bali vinafanya tu assembling. Mfano mzuri ni yale mabasi yetu ya mwendokasi. Golden Dragon kwa sehemu kubwa ni body makers. Engine zilitengenezwa na Kemix ya Marekani. Gear box na Diff zilitengenezwa Germany.
Tukiamua tunaweza. "Matatu" za Kenya hazivutii lakini ile kwamba ziko manufactured Kenya inawapa benefits nyingi ambazo ziko wazi.
Pia kwenye eneo la mini-bus tunapigwa na wajapani. Mimi nimekua kwenye biashara ya "macoaster na vi-hiece". Pale kinachofanyika ni dumping ya magari chakavu na mabovi ya Japan ambayo hayako designed kufanya kazi kwenye miundombinu kama ya kwetu.
Pia mengi kule yanafanya shughuli binafsi ila huku tunayatwisha mzigo wa commercial transportation. Hivyo yanachoka haraka.
Jana PM aliahidi kuwatembelea JN Coach tar 26. Alinikosha sana.