Chamoto
Platinum Member
- Dec 7, 2007
- 9,856
- 22,191
Falsafa yetu ilikuwa kupinga unyonyaji popote pale duniani, ndiyo sababu ya kuwasaidia hao wapalestina. Majirani zao waarabu huwa ni wanafiki sana hivyo walipoomba msaada kwa non aligned movement (NAM) Tanzania ikiwa mjumbe, walipewa. Tanzania imekuwa ikipokea wakimbizi wa Rwanda na Burundi toka 50's huko na imekuwa ikiwapa hifadhi wasomali na hata wasudani kusini.Kama kweli aliwaruhusu kuingiza bidhaa bila kulipa kodi nae alikosea sana sababu moja, anawaweka wageni kuwa na advantage sokoni kuliko wazawa lakini pili hatukutakiwa kuwachukua watu kutoka bara jingine sababu wana majirani ambao ni waarabu wenzao sasa kama majirani hawawataki sisi hatukutakiwa kuwa watakatifu sana, tatu hatuna mahusiano nao yoyote ya kiutamaduni(kama hawa wamarekani weusi)
Miaka ya sitini huo uhalifu unaousema haukuwepo ila kuna mfumo uliwekwa uliosababisha huo uhalifu kuongezeka. Ulianza katika kuharibu misingi ya familia kwa ku - promote single motherhood.Haya mambo ya kusaidia watu yametuchelewesha pia kwenye maendeleo sasa hivi waje ni offer mezani kama wengine tu mambo ya systemic racism yapo kweli lakini pia huko kwao ndio wanaongoza kwa uhalifu, utumiaji wa madawa, kukosa malezi ya wazazi wote na kukosa maarifa ya uwekezaji sasa kaka upo tayari kubeba hayo matatizo yao mengine pia uyalete huku?
Fikiria, mke/demu wako anakujibu ovyo, mnaanza kubishana kidogo anapiga simu polisi, jamaa wakija hata hawaulizi wanakubeba wewe kukupeleka jela, teyari hapo unapata record mbaya ya kuwa jela. Ukitoka unakuwa umeshafukuzwa kazi, kutafuta nyingine inakuwa ishu kwa kuwa unarekodi ya kuwa convicted with domestic violence.
Demu yeye anaamua ku file for child support, hata ukipata kazi pesa yako inakatwa juu kwa juu, huku akikuzuia kuona wanao. Wakati huo huo mjinga mmoja anajimegea kimasihara huku akiendesha gari uliyomnunulia mkeo. Aisee, we acha tuu.
Kutokana na kukosa mapato, demu anaweza akaenda kuomba kuishi kwenye section 8 (nyumba za kulipiwa na serikali) na kupata benefits kem kem za EBT card (electronic Benefits Transfer) ili kununua chakula bure. Mwanamke anapata faida zote hizi, kwa mwanaume kukandamizwa.
Sasa unakuta kwa kukosa sifa za kupata ajira wanaume wengi wanaishia kufanya uhalifu, na watu wengi wakiwa nje ya Marekani hudhani hawa watu ni wakorofi tuu kumbe ni mfumo ndiyo uliotengenza hayo.
Watoto wanaokulia kwenye jamaii hizo wanakuwa wanalelewa na hisia za kike toka kwa mama zao na hivyo kutoelewa mwanaume anatakiwa awe vipi. Hii husababisha cycle ya wanaume kuwa jela na watoto kulelewa na mama zao pekee kujirudia, kizazi hadi kizazi. Hivyo baadhi ya hao wanaokuja Afrika wanataka kuiondoa hiyo cycle ili kizazi kijacho kisiharibike.
Naomba nieleweke, sisemi wapewe kila kitu bure ila siyo mbaya wakifikiriwa.


tunawombea Somalia ushindi 