Hawa wanaharakati wa twitter wamechangia pakubwa upinzani kushindwa kwenye huu uchaguzi wa mwaka huu,
Viongozi wapinzani ikiwezekana kujitenga na hao wanaharakati uchwara fanyeni hivo,
Wanaharakati uchwara wa twitter wanapotosha na unakuta nao viongozi wa upinzani wanaingia mkenge kwenye huo upotoshaji unaofanywa na hao wanaharakati uchwara,
Binafsi nilikuwa ni mwanachama wa chama kimojawapo cha upinzani tena na kadi nilikuwa nayo kabisa na ulikuwa huniambii chochote kuhusu hicho chama [emoji23][emoji23][emoji23]
Lakini upinzani walipoanza kujihusha na hawa wanaharakati uchwara waongo na wapotoshaji rasmi nilijitoa upinzani na sio mimi tu...wapo wengi kama mimi,
Sasa hivi sina chama ila namkubali JPM na ndio maana nilipiga kura ya urais tu [emoji23][emoji23][emoji23]
Upinzani achaneni na hawa wanaharakati uchwara waongo na wapotoshaji.