Bastola ya Aden Rage na CCM

Bastola ya Aden Rage na CCM

tatizo sio yeye ila ni mikogo yake ndio inamsumbua nahisi ita mla na yeye..


 
Angalia picha hii halafu uipe maneno.

ragebastola.jpg
 
mara huyu anamwagiwa tindikali, yule nyumba yaungua karatasi inapona, huku katibu anasema kuna magaidi anawajua lakini polisi haiwajui, na huyu naye anapanda na siraha jukwaa la siasa kana kwamba ni vitan, mpaka kuisha kampen hizi tutasikia na kuona mengi pengine kuliko kampen zozote zile.

Yah kwa kweli hadi siku ya mwisho, naimani mabomu yatapigwa tu hapo Igunga, mana naona wenzetu wa magamba maji yameshawafika shingoni na sasa wanategemea zaidi vitisho. Ukimsikiliza Mukama utajua tu amelenga kutisha wananchi na kuwajengea hofu wananchi kuwa CHADEMA ni hatari. Nlitegemea chama kilichoshika Dora kisingekuwa na wasiwasi lakin Hofu ya kina Mukama ni dhahiri jahazi linazama. So hata Rage hajiamini kama wenzake ndo mana anajihami na Bastola.
 
Hakukuwa na haja ya Rage kupanda jukwaani na bastola kwa sababu kama mbili;
  1. Pamoja na kwamba bastola ni kwa usalama wake lakini pia ni hatari kwa usalama wake kwani bastola zinatafutwa sana na majambazi hivyo kujiweka target bila kujua kwa sababu ya ujinga wake
  2. Kwenye mikutano ya siasa kama ile ya Igunga kuna usalama wa kutosha hivyo hakukuwa na haja ya kuonyesha bastola hadharani.
 
Mkuu tayari waSomali wapo kibao Tanzania wamefanikiwa kuingiza fedha za uharamia [utekaji meli ipo thread hapa jamvini] kwenye uchumi wetu faida na hasara wanauchumi wanazijua lakini kisiasa tukilala hakika uchaguzi wa mwaka 2015 tutawashuhudia zaidi ya wasomali kumi mjengoni.Zipo jitihada za kuijumuisha Somalia kwenye EAC bila kujali hali ya ulinzi na usalama siku wakifanikiwa tutegemee instability ndani ya jumuiya.

Rage kafanikiwa kupenya ndani ya mifumo yetu ya uongozi kwakuwa iko weak sana majambazi wakiwa na fedha wanaingia halafu tuanategemea maendeleo.


Jamii za kisomali kama hizi zitatuletea matatizo sana hapa tz,maana wameshindwa kuishi kwao somalia,sasa wanataka kuleta instability huku kwetu,
huyu nae hashindwi kuleta mercenaries kutoka hapo somalia
 
nadhan picha hii iko clear zaidi
 

Attachments

  • 309011_10150296565636143_512646142_8314679_439906274_n.jpg
    309011_10150296565636143_512646142_8314679_439906274_n.jpg
    19.7 KB · Views: 46
Mkuu tayari waSomali wapo kibao Tanzania wamefanikiwa kuingiza fedha za uharamia [utekaji meli ipo thread hapa jamvini] kwenye uchumi wetu faida na hasara wanauchumi wanazijua lakini kisiasa tukilala hakika uchaguzi wa mwaka 2015 tutawashuhudia zaidi ya wasomali kumi mjengoni.Zipo jitihada za kuijumuisha Somalia kwenye EAC bila kujali hali ya ulinzi na usalama siku wakifanikiwa tutegemee instability ndani ya jumuiya.

Rage kafanikiwa kupenya ndani ya mifumo yetu ya uongozi kwakuwa iko weak sana majambazi wakiwa na fedha wanaingia halafu tuanategemea maendeleo.

hiyo thread nilishaisoma mkuu,ilikuwa thread nzuri,
tatzo la viongozi wa hii nchi,mtu ukiwa na hela,hata kama ni jambazi wa kiwango gani,wanakukumbatiia na kukuingiza kwenye system bila kuangalia effects zozote,mwisho wa siku hakuna maendeleo na viongozi majambazi wanaendeleza uajambazi wao
 
Rage hakusoma vizuri na hivyo JKT hakuiona. Silaha amejifunzia nyumbani kama alivyojifunza udereva wa gari. Hali hii inawakumba WATANZANIA wengi tu sasa baada ya mafunzo haya muhimu ya JKT kuelekea kufutika huku umuhimu wa kumiliki silaha kama hizi ukiongezeka miongoni mwetu.
 
Hayo mambo ya kupanda na Bastola jukwaani yangefanywa na kiongozi au mbunge wa CHADEMA wangewaambia wananchi kuwa oneni jinsi vyama vya upinzani vinavyotaka kuvunja amani nchini. Kwa kweli wangeongea mengi hadi povu lingewatoka, Sasa wamefanya wao ngoja tuone wataongea nini katika hili.
 
Msomali huyu hakupaswa kupanda jukwaani na bastola hata kama anaimiliki kihalali,after all hairuhusiwi kuonyesha hadharani. Nashindwa kuelewa ni kwa vipi Polisi haijamhoji/kumkanya kwa hilo. Sipati picha ingekuwa aliyefanya hivyo ni mwana CDM ingekuwaje
 
Hayo mambo ya kupanda na Bastola jukwaani yangefanywa na kiongozi au mbunge wa CHADEMA wangewaambia wananchi kuwa oneni jinsi vyama vya upinzani vinavyotaka kuvunja amani nchini. Kwa kweli wangeongea mengi hadi povu lingewatoka, Sasa wamefanya wao ngoja tuone wataongea nini katika hili.
Hofu yangu mimi ni jinsi alivyoivaa kishamba namna ile kiasi kwamba unampiga ngwala kidogo tu unamnyang'anya na kuleta madhara makubwa kwenye watu wengi namna ile. Watoa leseni za kumiliki silaha toeni na mafunzo pia. JKT na mafunzo ya mgambo vimekufa.
 
Mkuu kama kwenye kitabu cha animal farm." All animals are equal but some are more equal than others"

Kweli mkuu,
Najaribu ku-imagine hiyo bastola angekua amebeba Mh. Mbowe,
Kwanza ingekua mtaji wa kisiasa kwa Magamba,
Pili leo angekua "ndani" tayari.
Ila kwakua ni "mwenzao", anadunda tu bila tabu
 
Huyo ni mamluki wa Al-shabab kutoka somalia, madai ya kiongozi wa Ccm aliyevamia siasa uzeeni ndio hayo.
 
Kabla ya kumshambulia Rage tungepaswa kwanza kufahamu sheria za umuliki wa silaha hapa Tanzania. Kwa mfano:
  1. Je mtu anaruhusiwa kutembea na silaha anayoimiliki kihalali?
  2. Je ni makosa kuonesha silaha unayoimiliki kihalali hadharani?
Tukishazijua sheria za umiliki wa silaha tutakuwa na uwezo mzuri sana wa kuchangia hii mada. Naomba wataalm wa sheria watujuze zaidi.

As for me, sizijui hizo sheria ndio maana siwezi kusema kama Rage ana makosa au hapana.
Hayo maswali ni sawa kabisa, lakini kwa kufikiri kwa haraka haraka, NI KOSA ISIPOKUWA KWA WATU WA VYOMBO VYA ULINZI WANAPOKUWA KAZINI.
Ikiwa si kosa kutembea na na kuonesha hadharani silaha unayomiliki, maana yake ni kuwa, kila anayemiliki silaha kutembea na kuionesha hadharani, hii nchi ingelikuwa haikaliki.

Pia tuzingatie kuwa SILAHA si bastola wala bunduki tu. Mapanga, shoka, mikuki, mawe...pia ni silaha na watu wanazimiliki hizi kihalali. Je, ni ruhusa kwa anayemiliki silaha hizo kuingia nazo katika hadhara ya watu? Nafikiri wanaoelewa sheria wangelitufafanulia hili, iwapo ni kosa ni juu ya viongozi wa vyama vya upinzani kuchukua hatua zinazohusika. Ikiwa si kosa, poa. Sisi tusiomiliki mitutu, tunayo mapanga.

Kidokezo tu, huyu muechimiwa alibeba bastola kwa hofu ya kubakwa!
 
eti ulinzi binafsi, nani akuue wewe Rage, ushaboraro wa uzeeni ndiyo faida zake hizo.
 
Back
Top Bottom