Bastola ya Aden Rage na CCM

Bastola ya Aden Rage na CCM

hawa ndio waleta fujo
ila kuna siku tutawakomesha
07ragekam.jpg
 
usharobaro wa uzeeni ndiyo faida zake hizi.

attachment.php
 
CCM imeishiwa makada kiasi hiki? Vile vyuo vyao vyote vimefungwa au kubadilishwa matumizi? Hata Rage??
 
Kuna mtu hapa alikua anadai eti hio ni simu ya mchina, mie nikasema haya, kama kweli simu za kichina siku hizi ziko hivyo, haya, hadi siku waje kutuuua ndio tutajua kuwa sio simu ya kichina bali ni bastola ya kichina....
 
Usiposhangaa ya CCM utayaona ya CUF.... wao watakuwa na SMG Teh teh magamba wameshikwa pabaya!
 
sheria haikatazi mtu kumiliki silaha, ila hili la kuionyesha hadharani kama simu ya bb ni kosa kubwa tena ni kuwatisha wananchi. Watu kama hawa ndio wanaoendelea kutia doa kampeni za ccm. Yaani ccm imekosa watu wote mpaka inaenda kumchukua rage...ananikumbishia alivyokuwa fat ya zamani alikuwa mbishi sana..
nakubali ccm wamejua kuwa mambo magumu sasa wanaanza kuwatisha wapigakura hata mimi nimeona kwenye gazeti naomba mu m foadie john tedwa na mzee makame mapema
 
Kwa kuwa ni magamba polisi watajifanya hawajona,Ila ktk kibali cha kumiliki silaha bastola ni "concealed weapon",haitakiwi kuachiwa wazi kama alivyofanyakwa kuiachia wazi hivyo amekiuka taratibu za umiliki wa silaha, inatakiwa anyang'anywe kibali na silaha kukabidhi polisi.Jambo ambalo sidhani kama wahusika watalifanya.
 
Dalili za kuzama kwa Meli CCM ni makada wake kama aki na Rage kutembea na siraha kama ishara ya woga.
Tukumbuke Rage sio Gamba wa kwanza kudharau sheria ya kumiliki na kutembea na siraha ya moto kwani Gamba wa kwanza allitishia kumshugulikia mtu na Bastola yake huko mwanza ndani ya Club; na mwingine kesi yake sijui imekwisha vp huko Arusha walipotishiana magamba kwa magamba wenyewe kutwangana risasi kwa bastola zao. Jamani la kuvunda halina dawa.!!!
 
Hii ni hatari sana. ndo CDM inatakiwa wawaeleze wananchi wa Igunga kuwa CCM ni chama cha kuogopwa sana, na wasiende kwenye mikutano yao maana risasi ziko nje nje watauwawa. km mtu anadiriki kutembea na silaha hadharani kiasi hiki ataona ajabu gani kumshuti mtu wakati wowote?

Hebu wana JF ni waulize, je sheria inasemaje kuhusu matumizi na handling ya hizi silaha jamani?

Naomba kutoa hoja wadaU.
 
Hawa ndiyo watanzania wanaojiita great thinkers kweli? matusi ya nini sasa ? ebu tujenge taifa kwa kutoa michango yenye "matinki" , wewe bora utoke hautufai humu

sasa hapo tusi ni nn? BWANA ni tusi? Pole sana! Kwa hiyo ukisema Mungu ni bwana wa mabwana unakuwa unakufuru? na hyo 'MATINKI' ndiyo nn?
 
Nilipokuwa nasoma gazeti la MWANANCHI asubuhi nilishtuka sana kuona picha ya RAGE akiwa na MGUU WA KUKU kiunoni as if kaning'iniza simu vile!!! CCM wanayo kazi sana jamani.....mpaka tukifika 2015 watakuwa wanabeba mabomu viunoni
 
Hayo maswali ni sawa kabisa, lakini kwa kufikiri kwa haraka haraka, NI KOSA ISIPOKUWA KWA WATU WA VYOMBO VYA ULINZI WANAPOKUWA KAZINI.
Ikiwa si kosa kutembea na na kuonesha hadharani silaha unayomiliki, maana yake ni kuwa, kila anayemiliki silaha kutembea na kuionesha hadharani, hii nchi ingelikuwa haikaliki.

Pia tuzingatie kuwa SILAHA si bastola wala bunduki tu. Mapanga, shoka, mikuki, mawe...pia ni silaha na watu wanazimiliki hizi kihalali. Je, ni ruhusa kwa anayemiliki silaha hizo kuingia nazo katika hadhara ya watu? Nafikiri wanaoelewa sheria wangelitufafanulia hili, iwapo ni kosa ni juu ya viongozi wa vyama vya upinzani kuchukua hatua zinazohusika. Ikiwa si kosa, poa. Sisi tusiomiliki mitutu, tunayo mapanga.

Kidokezo tu, huyu muechimiwa alibeba bastola kwa hofu ya kubakwa!

Kisheria ukiwa na nguo za kawaida huruhusiwe kuonyesha silaha za nguvu hata kama unamiliki. Haya ni makosa makubwa sana, watu wanaoweza kuonyesha silaha hadharani ni watu ambao wanajulukana kama walinzi nao wanasheria zao, polisi akitoka kazini lazima akabidhi na jeshi.

Sasa tujue ccm inatuletea mambo ya somalia, irak, na bangladesh. Kwenye umati wa watu wengi hairuhusiwi hata panga, kisu nk. CCM mnatupeleka wapi? Sasa ifike mwisho kama Nyerere alivyoikana na kusema sisiem sio mama yangu. Hii ni kauli mbiu alianzisha mwasisi wa ccm na sisi tunaunga mkono. Yeye RAGGE jana alikuwa na silaha yake mimi kesho nitamwona Mburundi Mrwanda Mkongo au sisi watanzania wenyewe nk wakiwa na silaha nitaweza kuhoji au maskari wataweza kumhojii. Askari kwa ccm wanakazi kubwa sana muoombe mungu watanzania wachukue uamuzi wa haraka iondoke madarakani.

Tatizo letu watanzania unafiki umezidi.
 
Nafikiri sheria imekupiga chenga.

Sasa na wale polisi wanaotembea na silaha khadharani kwenye mabenk na mitaani ni magaidi?

Kifupi kinachokatazwa na Sheria ni kumtishia mtu silaha au kumlenga (kumuonyeshea kuelekea ulipo mwili wake) ni kosa. lakini kuihifadhi kiunoni na watu wakaioana hakuna kosa llolote.

nikuulize shehe anapotoa hutba na kutuelekeza kwamba nyama ya nguruwe haramu, huku ana banda la kufugia nguruwe na bucha ya kuuzia nyama ya nguruwe! ccm wanahubiri amani huku makada wanabeba silaha, huoni ni kinyume na mahubiri yao? Anzeni tu!
 
kitu kimoja nimekuja kunote ni kuwa either rage ni MPENDA VITA au LIMBUKENI! wengi wanazo bastola na kimsingi hutakiwa KUFICHWA!!!!!! ukitazama hiyo picha kimsingi lijamaa liko proud kuwa na bastola kiunomi!!! kimsingi amepandisha shati ili ionekane!!!
 
Back
Top Bottom