Balozi Juma Mwapachu atangaza kurejea CCM...

Balozi Juma Mwapachu atangaza kurejea CCM...

Misemo ya Kiswahili inakuwa na maana inapotumiwa inavyotakiwa.

Mtu anayehama CCM na kurudi back CCM, kama ana akili timamu, anatakiwa kutosema habari hiyo. Wanaompokea CCM ndio wanaotakiwa kusema kama yaliyopita ni ndwele au si ndwele.

Alichosema Mwapachu ni kama mtu kakuzaba kibao wakati anafikiri wewe mtoto, halafu anapoona kumbe wewe ndiye baba mwenye nyumba akwambie yaliyopita si ndwele.

Kama kuna mtu wa kusema yaliyopita si ndwele hapa, ni yule anayesamehe.

Anayesamehewa hawezi kuchagua tu kwamba nini ni ndwele na nini si ndwele.

Ataambiwa "Mla ndizi husahau, lakini mtupa maganda hasahau".

Tunajua asiyekubali kushindwa si mpinzani lakini kujirudi huku kwa baniani mbaya, kiatu chake dawa na kumtukana mamba kabla ya kuvuka mto ni ishara ya bendera kufuata upepo iliyo katika chombo kinachozama kisicho usukani.

Fumbo mfumbe mjinga, mwerevu huligangua na kanga hazai ugenini kama jogoo la shamba haliwiki mjini.

Maneno mema humtoa nyoka pangoni, lakini la kuvunda halina ubani na maji yakimwagika hayazoleki.
Hii dhana ya kuhama hama kwa mtu mwenye umri wake na heshima zake ni kujidhalilisha.

Wazee kama Jaji Warioba au Butiku wako CCM sio kwa sababu CCM inafanya mambo mazuri sana, La hasha. Wameendelea kuwa wanaCCM kwa sababu heshima yao wameipata ndani ya CCM.

Halafu huyu Mzee ametoa rushwa ya shilingi milioni moja kwenye tawi ili zitumike kukarabati jengo la ofisi ya tawi.

Mwangalie kwenye hii video wakati akitoa rushwa baada ya kukaribishwa tena ndani ya CCM.

Labda hii rushwa ya shilingi milioni moja ndiyo imepelekea kusema maneno kama Yaliyopita si ndwele...

 
Mbaya zaidi mtu mwenyewe alishafika level ya ubalozi wa nchi nje ya nchi....Mungu atunusuru viongozi hawa vinasaba vya kina Mangungo bado vipo nao siyo ajabu tupo jinsi tulivyo; huko East Africa Community atakuwa amepitisha mangapi kwakushawishiwa kama kwa ushawishi mdogo wa mtu mmoja aliweza sahau nafasi yake katika taifa hili?
Huyo mzee nimemshangaa mpaka nashangaa. Hard to believe what he has done. Yani na kuiponda kote kule ccm na bado amerudi?.... kaamua kula matapishi yake bila hata aibu.
Kuna watu na viatu. Huyu ni mfano was viatu.
 
Yaani, mnawafundisha hawa vijana vitu gani nyinyi? Mnataka Taifa liwakumbuke kwa yepi hasa? Majina yenu tu? Mnataka tutakapoandika historia tuseme na wao walikuwepo? Binafsi sina tatizo kabisa na wewe kurudi CCM au kuachana na CCM kabisa au kujiunga na chama kingine chochote kwani hilo ni suala la hiari ya mtu. Sikusema lolote ulipoondoka kwani sikuwa shahidi ulipoingia ilikuwaje.

Kujiunga na chama cha siasa ni hiari ya mtu na ni sehemu ya demokrasia ndio maana sijali sana watu kutoka au kujiunga na chama chochote.
Kitu ambacho kimenitibua sana ni maelezo ya kwanini umeamua kurejea! Maelezo yako yanaonesha kitu kimoja cha hatari kabisa; wewe si mtu wa kanuni na mwenye kusimamia unachosimamia.

Maelezo yako yanaonesha pia kuwa wewe si mtu wa tafakari makini na mwenye kupima matokeo ya maamuzi yako mbalimbali. Umejionesha tu ni mtu wa kuongozwa na hisia na kufuata upepo; ni kama kijana mdogo ambaye anahitai kuendelea kufunzwa. Hili naona ni la kuudhi na kutisha zaidi.

Hata sasa swali kubwa linalobakia ni kuwa je tunaweza kukuamini; je tunaweza kuamini kuwa unasema kweli sasa? Je umejionesha kuwa unaweza kuaminika; mtu yeyote anayekuita rafiki anaweza kukuamini sasa na akaingia mapatano nawe?

Binafsi naamini – na inaonekana mwenyewe umegundua hilo – umeonesha mfano mbaya kama kiongozi mkongwa; umeonesha ukosefu mkubwa wa hekima na zaidi umeonesha udhaifu mkubwa wa kusimamia mambo uliyoyaamini.

Sidhani kama hadi hivi sasa kuna lolote ambalo CCM kama chama imelifanya ambalo lingekubadili mawazo; na umesema kweli kuwa sasa umerudi kumfuata mtu kama ulivyoondoka kumfuata mtu; hii ni aina mbaya kabisa ya uongozi tunayotaka kujenga nchini.
Watu wasio na kanuni na maadili ya kuaminika wanaweza vipi kusimama na kujionesha kuwa wanaweza kuaminiwa na kuwa wana kanuni?

Binafsi naamini badala ya kujaribu kuzengea nafasi fulani mahali fulani wakati huu ungeamua kujiendeleza na mambo yako na kuachana na siasa ili angalau uonekane umeaminika. Ni matumaini yangu Magufuli hatowazawadia watu wa aina yako kwani taifa letu linahitaji viongozi bora na siyo bora viongozi; tunahitaji watu ambao watasimama kama mifano kwa vijana na vizazi vijavyo badala ya kuja kutajwa kama viongozi waliowahi kuwepo kuwepo na siyo walikuwepo viongozi viongozi!

Kusamehewa najua wengi tutakusamehe; lakini hatuwezi kukuamini hadi ujioneshe unaweza kuaminika kweli. Kwa hayo uliyoyaseme leo kuwa yaliyopita si ‘ndwele’ tugange yajayo; mmh! Tafadhali Balozi Mwapachu!

MMM

Note: Imehaririwa kuakisi maelezo ya Mwapachu kuwa taarifa iliyokuwa inasambaa siyo yake; mantiki ya ukosoaji wa maamuzi yake bado inasimama na hata maelezo yake ambayo yamepatikana hadi hivi sasa bado yanasimama na ukosoaji huu.

Njaa Njaa Njaaa
Njaa ni kitu kibaya sana.
 
Duh! Hii nchi kiboko. Mtu mzima anajiadhiri hadharani bila chembe ya soni. Sad!
Alikuwa na followers wengi sana Facebook hasa ambitious young leaders na vijana wa kaliba mbalimbali, kawaangusha, aliwahamasisha na makala zake murua kuhusu mageuzi...walimpenda sana.....am sure ataifunga hii account la itakuwa imedoda mno
 
Aliyeandika ule waraka feki wa Mwapachu aliwachota wengi, ila mimi nilishtukia kwamba umeandikwa ili kumpaka matope Mwapachu.

Lakini tutajuaje kama hata huo waraka hakuuandika yeye mwenyewe halafu baada ya kuona umebuma akaamua kuukana?

Manake kwa jinsi alivyojidhalilisha huyo mzee siwezi kushindwa kudhani kuwa huenda hata huo waraka aliuandika mwenyewe lakini baadaye akaamua kuukana!
 
Tanzania one huyu wa 1964 Mpaka wakaitwa Ikulu siku ya Muungano na Mwl Nyerere na mpaka leo kaweka kwake hiyo picha ya kumbukumbu lakini akili zimeisha tangu andoke Ndugu yake Harith Bakari Mwapachu aliekuwa Waziri wa katiba wakati wa Mkapa na Usalama wa Raia wakati wa Uwaziri Mkuu wa Lowassa
Kwani huyo ndugu yake alienda wapi?
 
Lakini tutajuaje kama hata huo waraka hakuuandika yeye mwenyewe halafu baada ya kuona umebuma akaamua kuukana?

Manake kwa jinsi alivyojidhalilisha huyo mzee siwezi kushindwa kudhani kuwa huenda hata huo waraka aliuandika mwenyewe lakini baadaye akaamua kuukana!
Mzee Mwapachu namjua personally. Moja ya sababu zilizonifanya niuwekee maswali mengi sana ule waraka.

Kama ambavyo mimi uandishi wangu huwezi kujificha kwa Mimi Mwanakijiji ndivyo uandishi usio wa Mwapachu usivyoweza kujifanya wa Mwapachu kwangu.

The whole thing was just too incoherent.
 
Mzee Mwapachu namjua personally. Moja ya sababu zilizonifanya niuwekee maswali mengi sana ule waraka.

Kama ambavyo mimi uandishi wangu huwezi kujificha kwa Mimi Mwanakijiji ndivyo uandishi usio wa Mwapachu usivyoweza kujifanya wa Mwapachu kwangu.

The whole thing was just too incoherent.

Heck, he himself sounded disjointed and appeared to be out of it!
 
Heck, he himself sounded disjointed and appeared to be out of it!
The mistake they make is thinking this is '69 and there are no smartphones and all kinds of technologies to capture it all.

He looked like he was coming out of a Palm Beach Black Label double double binge contest with Ben Mkapa.

And you know Ben can hold the worst of the Highland single malts, even as he once, on a drunken stupor, delayed Mwinyi on a state visit, to Saudi Arabia no less, because he had had much too much of the stuff.
 
Inawezekana balozi ampandikizwa na chadema asee
unless natakakusema huyu jamaa hajitambui
 
Nimemuona mzee ktk news zilizosomwa usiku, na amekiri kurudi ccm kavaa shati la kitenge green na katoa 1m/- as mchango kwa ajili ya uimarishaji wa hilo tawi! Amejistate kidogo lkn ktk news hawakuonyesha yote alivosema! Tatizo langu ni huu warka! Sifikiri mzee mwapachu kauandika yeye kwa mkono wake! I doubt it!
 
Mwapachu yuko exactly kama walivyo wana CCM walio wengi..
ni kuwaza kupiga dili kutwa
si ajabu na leo kuna fungu kapewa la kurudi CCM
Ili kuweka kumbukumbu sawa hakika EL ni kansa inayotafuna chadema na Ukawa.
 
Yaani, mnawafundisha hawa vijana vitu gani nyinyi? Mnataka Taifa liwakumbuke kwa yepi hasa? Majina yenu tu? Mnataka tutakapoandika historia tuseme na wao walikuwepo? Binafsi sina tatizo kabisa na wewe kurudi CCM au kuachana na CCM kabisa au kujiunga na chama kingine chochote kwani hilo ni suala la hiari ya mtu. Sikusema lolote ulipoondoka kwani sikuwa shahidi ulipoingia ilikuwaje.

Kujiunga na chama cha siasa ni hiari ya mtu na ni sehemu ya demokrasia ndio maana sijali sana watu kutoka au kujiunga na chama chochote.
Kitu ambacho kimenitibua sana ni maelezo ya kwanini umeamua kurejea! Maelezo yako yanaonesha kitu kimoja cha hatari kabisa; wewe si mtu wa kanuni na mwenye kusimamia unachosimamia.

Maelezo yako yanaonesha pia kuwa wewe si mtu wa tafakari makini na mwenye kupima matokeo ya maamuzi yako mbalimbali. Umejionesha tu ni mtu wa kuongozwa na hisia na kufuata upepo; ni kama kijana mdogo ambaye anahitai kuendelea kufunzwa. Hili naona ni la kuudhi na kutisha zaidi.

Hata sasa swali kubwa linalobakia ni kuwa je tunaweza kukuamini; je tunaweza kuamini kuwa unasema kweli sasa? Je umejionesha kuwa unaweza kuaminika; mtu yeyote anayekuita rafiki anaweza kukuamini sasa na akaingia mapatano nawe?

Binafsi naamini – na inaonekana mwenyewe umegundua hilo – umeonesha mfano mbaya kama kiongozi mkongwa; umeonesha ukosefu mkubwa wa hekima na zaidi umeonesha udhaifu mkubwa wa kusimamia mambo uliyoyaamini.

Sidhani kama hadi hivi sasa kuna lolote ambalo CCM kama chama imelifanya ambalo lingekubadili mawazo; na umesema kweli kuwa sasa umerudi kumfuata mtu kama ulivyoondoka kumfuata mtu; hii ni aina mbaya kabisa ya uongozi tunayotaka kujenga nchini.
Watu wasio na kanuni na maadili ya kuaminika wanaweza vipi kusimama na kujionesha kuwa wanaweza kuaminiwa na kuwa wana kanuni?

Binafsi naamini badala ya kujaribu kuzengea nafasi fulani mahali fulani wakati huu ungeamua kujiendeleza na mambo yako na kuachana na siasa ili angalau uonekane umeaminika. Ni matumaini yangu Magufuli hatowazawadia watu wa aina yako kwani taifa letu linahitaji viongozi bora na siyo bora viongozi; tunahitaji watu ambao watasimama kama mifano kwa vijana na vizazi vijavyo badala ya kuja kutajwa kama viongozi waliowahi kuwepo kuwepo na siyo walikuwepo viongozi viongozi!

Kusamehewa najua wengi tutakusamehe; lakini hatuwezi kukuamini hadi ujioneshe unaweza kuaminika kweli. Kwa hayo uliyoyaseme leo kuwa yaliyopita si ‘ndwele’ tugange yajayo; mmh! Tafadhali Balozi Mwapachu!

MMM

Note: Imehaririwa kuakisi maelezo ya Mwapachu kuwa taarifa iliyokuwa inasambaa siyo yake; mantiki ya ukosoaji wa maamuzi yake bado inasimama na hata maelezo yake ambayo yamepatikana hadi hivi sasa bado yanasimama na ukosoaji huu.

Ninadhani ni vizuri, hata katika extension ya mikataba, ni vizuri tusiende mbali sana na notion ya retirement age. Ingawa kuchoka kwa akili hakulingani kati ya mtu na mtu bali inategemeana na mambo mengi sana. But in all ways, ninashauri tujifunze kusoma brain anatomy za watu kutoka zaidi ya umri bali pia matunda ya maisha yao ya kila siku. Anapokuwa amefikia mahala pa kujichanganya kama hivi , tujue tu umri wake umevuka kiwango cha kufanya tunayoyatarajia. Pengine ni kule kuanza kurudi utoto.
Na kwa mantiki hiyo, wazee wetu wanapashwa pia kutambua na kuwa makini na matamshi wanayoyatoa kwa kuwa yanaweza kufuta historia njema waliyoijenga.

Na jamii inapashwa kuelewa yanapotokea ya mwapachu, wajue ni graph ya ukuzi na hivyo kuyaacha kama yaliyvo.
 
Mzee Mwanakijiji kuna hoja sijui watu wameiona katika bandiko. Nilishangaa sana kumsikia Balozi Mwapachu akitangaza kurudi CCM

Suala hapa si kurudi au kubadili vyama. Hilo ni sehemu ya demokrasia na linawezekana bila tatizo. Suala ni 'precedence' wanayoweka hawa wazee kwa next generation.

Mzee Mwapachu anabeba jina zito katika historia ya nchi hii.

Kupitia uwezo wake na fursa, ametengeneza jina kama waziri, balozi na katibu mkuu wa taasisi kubwa ya EAC

Kauli yake kwa wengi ni kama 'sheria' kwasababu ya public trust aliyo nayo.

Wengi wanamuona mzee mwenye maono ambaye mambo rahisi anayaona kabla hayajatokea. Mzee anayeweza kupiga hesabu za miaka 10 ijayo n.k.

Ni mkongwe wa siasa anayepaswa kufundisha vijana siasa maana yake ni nini.
Kuhama kwake ilikuwa sehemu ya siasa kwavile alisimama na alichokiamini

Katika hili, Mwapachu angekuwa na nafasi nzuri kama angestaafu siasa.
Kuhama siasa kila baada ya miezi 6, haaminiki tena katika uso wa jamii.

Kama hana public trust, anahitaji nini katika siasa?

Nilimweleza Dr Slaa aipoachana na Chadema akae kimya au aache siasa abaki na heshima yake kama kiongozi na mfano.

Habari ya kukimbizana na akina Mwakyembe inamdhalilisha.
Sijui kama alinisikia au alisikia, ninachojua aliachana na mambo ya siasa.

Huo ulikuwa uamuzi mzuri ingawa alishajitia majereha pale serena

Mwapachu, kwa hili ningekushauri kesho asubuhi amka na kutangaza kustaafu siasa

Si dhani hata CCM wanakuamini, sidhani umma unamwamini tena.

Jiamini kukaa nje ya siasa ukistaafu na kuwa hazina kwa nchi

Ulichokifanya ni fedheha
 
Back
Top Bottom