Balozi Juma Mwapachu atangaza kurejea CCM...

Balozi Juma Mwapachu atangaza kurejea CCM...

Mzee Mwapachu kaimaliza kisiasa.Hakuna mwanasiasa mbovu kama mwanasiasa kigeugeu.Hata huko CCM ataonekana kama tishu ya msalani.Amejivua nguo.
 
Watu wa aina ya Balozi Mwapachu wanawavuruga sana vijana Watanzania!

Fikiria kuna watu walikuwa wanapiga kelele za kumpongeza sana siku ambalo aliachana na CCM. Leo pia wanapiga kelele ya kumdharau katika maamuzi yake huku wengine wakiachwa na mshangao.

Mbaya zaidi anawaambia yaliyopita si ndwele, tugange yajayo!
 
Mwapachu yuko exactly kama walivyo wana CCM walio wengi..
ni kuwaza kupiga dili kutwa
si ajabu na leo kuna fungu kapewa la kurudi CCM
Vipi alipokuwa akiandika kingereza chake kumsifia lowassa si ulikuwa unamuunga mkono sio?
 
Aliyeandika ule waraka feki wa Mwapachu aliwachota wengi, ila mimi nilishtukia kwamba umeandikwa ili kumpaka matope Mwapachu.
 
Nimesoma bandiko lako kwa makini nimegundua kuna maneno kama unajitukana na wewe hivi ......anyway Watanzania wengi misimamo ni zero kabisa..
Fikiria kama chadema imekula matapishi yake vipi kwa wafuasi wake
 
Mwapachu yuko exactly kama walivyo wana CCM walio wengi..
ni kuwaza kupiga dili kutwa
si ajabu na leo kuna fungu kapewa la kurudi CCM
Nakuheshimu sana mkuu lakini jua kuwa hakuna wakumnunua mwapachu kwa faida gani ccm kwa sasa inauzika
 
Duh! Hii nchi kiboko. Mtu mzima anajiadhiri hadharani bila chembe ya soni. Sad!
Mbaya zaidi mtu mwenyewe alishafika level ya ubalozi wa nchi nje ya nchi....Mungu atunusuru viongozi hawa vinasaba vya kina Mangungo bado vipo nao siyo ajabu tupo jinsi tulivyo; huko East Africa Community atakuwa amepitisha mangapi kwakushawishiwa kama kwa ushawishi mdogo wa mtu mmoja aliweza sahau nafasi yake katika taifa hili?
 
Watu wa aina ya Balozi Mwapachu wanawavuruga sana vijana Watanzania!

Fikiria kuna watu walikuwa wanapiga kelele za kumpongeza sana siku ambalo aliachana na CCM. Leo pia wanapiga kelele ya kumdharau katika maamuzi yake huku wengine wakiachwa na mshangao.

Mbaya zaidi anawaambia yaliyopita si ndwele, tugange yajayo!
Yani UKAWA inapita mapito magumu...

Lakini yote hii ni kutegemea akili za ccm ziwaendeshee vyama vyao
 
Ningejua elimu ya mwapachu ningemzungumzia sana ila kwa kuwa siijui basi.

Nilichobahatika kugundua ni kwamba mwapachu is still young politically na ninadhani hata uwezo wake wa kufikiri. (Ashakum si matusi)

Mwapachu ni M binafsi, ni that kind of a person anayetafuta njia za kulinda maslahi "shughuri zangu na za washirika wangu" rejea hotuba yake.

Ni afadhari ya lowasa kuliko mwapachu, ni afadhari ya kingunge kuliko mwapachu. Jiulize....

Hivi lowasa angeshinda, mwapachu angeongea anayoyaongea?????

Halafu chunguza hotuba yake, amejivua nguo mwenyewe, kuwa he is after vyeo"wenzangu wamebaki ccm na wana vyeo".

He is after chances.

Ashakum si matusi, mwapachu ni mnafki na hapaswi kuaminiwa tena. Kama anatubu lakini kwa kutumia maneno Yale Yale ya"shughuri zangu na za washirika wangu.......wengine wamebaki na wana vyeo" HAKUNA MTU HAPO.


MAGUFULI ALIWEZA AKIWA PEKE YAKE NA WAZIRI MKUU NA MAKAMU TU, HAWEZI KUSHINDWA AKIWA TAYARI NA MAWAZIRI, MAKATIBU WAKUU WATIIFU, NA SAFU NZIMA YA WAKUU WA MIKOA.

Ashakum si matusi, MWAPACHU is TOO LATE.

Don san tan
 
Watu wa aina ya Balozi Mwapachu wanawavuruga sana vijana Watanzania!

Fikiria kuna watu walikuwa wanapiga kelele za kumpongeza sana siku ambalo aliachana na CCM. Leo pia wanapiga kelele ya kumdharau katika maamuzi yake huku wengine wakiachwa na mshangao.

Mbaya zaidi anawaambia yaliyopita si ndwele, tugange yajayo!
Misemo ya Kiswahili inakuwa na maana inapotumiwa inavyotakiwa.

Mtu anayehama CCM na kurudi back CCM, kama ana akili timamu, anatakiwa kutosema habari hiyo. Wanaompokea CCM ndio wanaotakiwa kusema kama yaliyopita ni ndwele au si ndwele.

Alichosema Mwapachu ni kama mtu kakuzaba kibao wakati anafikiri wewe mtoto, halafu anapoona kumbe wewe ndiye baba mwenye nyumba akwambie yaliyopita si ndwele.

Kama kuna mtu wa kusema yaliyopita si ndwele hapa, ni yule anayesamehe.

Anayesamehewa hawezi kuchagua tu kwamba nini ni ndwele na nini si ndwele.

Ataambiwa "Mla ndizi husahau, lakini mtupa maganda hasahau".

Tunajua asiyekubali kushindwa si mpinzani lakini kujirudi huku kwa baniani mbaya, kiatu chake dawa na kumtukana mamba kabla ya kuvuka mto ni ishara ya bendera kufuata upepo iliyo katika chombo kinachozama kisicho usukani.

Fumbo mfumbe mjinga, mwerevu huligangua na kanga hazai ugenini kama jogoo la shamba haliwiki mjini.

Maneno mema humtoa nyoka pangoni, lakini la kuvunda halina ubani na maji yakimwagika hayazoleki.
 
Matope yapi aliyopakwa mapachu
Kwenye waraka feki uliosambazwa kwamba umeandikwa naye ambao Mwanakijiji kautaja katika Nota Bene yake.

Umesambaa mtandaoni na ndio msingi wa Mwanakijiji kuandika alichoandika, ingawa ame edit na kusema kwamba licha ya waraka huo kuwa feki, msingi wa critique yake uko pale pale.
 
Kwenye uzi kama huu Chadema utawaonea huruma
 
2020 ajisndae kwenda ACT maana hatopokelewa cdm ajiunge na akina yuda mapema
 
Mzee mzima hajiamini hata aliyoongea kajizalilisha tu. Hivi kuna watu waiona ccm mungu eeh so shame
 
Imebidi atoe rushwa ya milioni moja kwa ki local branch cha CCM ili wamkubali na kumtayarishia ki noise cha kurudi chamani. Eti ku renovate ki ofisi cha chama!

Ki spichi chake cha sababu za kurudi CCM kiko shaloooow! Eti nimejiuliza nikatafakari nawezaje kukaa nje ya chama kilichonilea, kilichonikuza, kilichonifikisha hapa.... such light weight justifications...

Imagine hivi vichwa vya type hii ndio vimekuwa vinatawala hii nchi....
 
Back
Top Bottom