Bakwata, Basuta Walaani DC Kuvuliwa Hijabu

Bakwata, Basuta Walaani DC Kuvuliwa Hijabu

Status
Not open for further replies.
CCM inacheza sana na akili za waisilamu maana ni rahisi sana kuwanasa. Wao ukitaka kuwateka tumia dini tu hata kama jana uliwatoa ngeo kama ni mwenzao mtapatana. Nadhani pengine ndivyo wananavyo fundishwa(ubinafisi wa kidini mpendelee mwisilami mwenzako)
Cha ajabu ni kwamba hawaamini kwamba CCM kamwe hawataweza kutimiza matakwa ya waisilamu yaliyo kinyume na katiba ya nchi hii hata kama mwenyekiti wake ni mwiisilamu. Atawandanganya tu na mwisho wa siku atawaambia hayo ni mambo yenu fanyeni wenyewe na huo ndo ukweli.

Hakuna Raisi nchi hii hata kama atakuwa shehe,padre au mchungaji atakayekubali kuvunja katiba ya nchi kwa ajili ya kuipendelea dini moja dhidi ya nyingine. Wenzetu waisilamu hawataki kukubaliana na hili wanadhani Raisi akiwa mwisilamu basi anaweza kupendelea uisilamu kitu ambacho hakitakaa kitokee nchi hii!

Kama Raisi wa Tanzania anataka asimalize hata mwezi Ikulu basi apendelee dini yake kwa uwazi aone kama kundi la pili litaogopa na kukaa kimya.

Kama kuna waisilamu wanaona CDM haimtendei haki (japo haijawahi kuwa na mamlaka ya kutenda au kutowatendea haki watanzania) aendelee kubaki ccm kama anaona kwake issue ni dini zaidi kuliko vita vya ufisadi na maisha magumu tuliyonayo watanzania kwa sasa. Hakuna anayemlazimisha mtu kuwaunga mkono chadema ila ni watu wenyewe wameua kutoka mioyoni mwao.

Hatuwadharau wenzetu waisilamu ila Imekuwa too much utafikiri wao ni yule mtoto kitinda mimba ambaye hagusi hata kidogo analia 'mamaaaaaa eti ....... ananishikakichwani'! Ndugu zetu lazima wajiamini waondokane na ile inferiority comprex na kudhani kuwa kuna mtu anawdharau.

Inashangaza sana kwanini kunakuwa na watu wao hujihisi kunyanyaswa tu kila wakati bila hata kuyaona manyanyaso yenyewe.
But nina marafiki zangu tumesoma nao ni waisilamu lakini wanajiamini sana na ni wapenzi wa chadema wa kufa mtu.

ndugu zetu jiaminini kwanza bila hivyo itasumbua sana na hatutakaa tutatue matatizo ya msingi ya nchi yetu. Kumbukeni mtaendelea kutumiwa tu na ccm kama toilet paper wakati wa uchaguzi wakishapata mnabaki palepale labda na nyie muwe mafisadi wakati dini hairusu.

Tuweni kitu kimoja bila kujali dini zetu tumshughulikie adui wa watanzania wote ambaye ni ccm. Hata Kama baadhi yenu mtakataa bado Mungu akisema ndiyo hakuna atakayezuia.

Mungu ibariki Tanzania!
we ugonini wacha kuwatukana waislam,maneno yako niyakuwadhalilisha waislam na imani yao,je waislam wangemvamia sister wakamvua kilemba na kumburuza ungekaa kimya?cheza na mtu usicheze na imani yake.
 
CHADEMA wawaombe radhi waislam na mama fatuma kimario kwani kumvua hijabu ni udhalilishaji tunaona ulaya wanavyofanya juu ya waislam kuwadhalilisha, je? na chadema wanaiga hao wazungu?

Nyie ni moja ya watu ambao ni janga kwa taifa, kama unavyojitambulisha kwa jina lako hapo, inavyoonekana wewe ni mfuasi mzuri wa CUF nilijua wewe utakuwa wa kwanza kuwa na kumbukumbu ya alivyofanyiwa mbunge wenu kule Tabora aliposwekwa mahabusu chumba kimoja na wanaume, tena mama huyu ni muislam mbona hatukusikia hawa wanaojiita bakwata wakipiga kelele au hilo limehalalishwa na uislam, au kwa sababu tu ni chadema ambayo mnaamini ndo adui wa uislam, mbona mkulu kawachana laivu bila chenga kuhusu mahakama ya kazi hatujasikia mkipanga maandamano nchi nzima kuishinikiza serikali kuwapatia hiyo mahakama au ndo mmeamua kuingia kwa gia hii ili mkulu awaonee huruma na kuwapa hiyo mahakama
 
Poleni sana ndugu zangu waislamu maana hapa ninachokiona ni dini yenu kupoteza maana mbele ya jamii kupitia hawa viongozi wenu wa bakwata wanaotulizwa njaa zao na ccm na kuonekana kuwa ndo msimamo wa waislamu wote
 
Hizo taasisi zilizolalamikia Chadema hawajawahi kufurahishwa lolote na Chadema. Mimi nadhani ni vizuri wavue vilemba na hijabu wajitumbukize kwenye siasa maana hakuna asiyejua kuwa hawa watu wako nyuma ya mgongo wa ccm kitu ambacho ni haki yao lakini wasijifiche nyuma ya pazia la dini pia. Ni ujinga uliotukuka.

Nawashangaa wajinga wote wanaoshabikia ujinga huu wa kidini katika siasa wakidhani watashinda. Kwa hakika wataangukia pua tu maana shida wanazozalisha ccm kwa wananchi zitafika mahali pa kuchosha watu wa dini zote, kabila zote na rangi zote na hapo propaganda za kijinga kama hizi zitakuwa zimefikia kikomo.

Leo matatizo yetu yote hayana uchaguzi wa dini. Kila mtu kwa dini yake kaathirika. Tusiendeleze na kuendekeza ujinga wa kidini. MNASIKIA NYIE WADINI?
 
Kwa kweli Bakwata wamekurupuka kwa kauli hz na pia inaonekana ni kama kutaka kuwachonganisha waislam na CDM....waislam ni watu wana akili timamu sana na hata siku moja hawawezi kukubali utumbo unaoongelewa na viongozi wao kwani wao wanajua kipi ni pumba na mchele....! Hakuna haya ya kuihukumu CDM kabla ya ushahd, ngoja tusubr na kama ikidhihirika kwamba CDM walikosea basi hapo ndipo wanapotakiwa kuomba radhi na si vinginevyo!
 
Inshu ya kisiasa inabadilishwa muelekeo wa kidini na kupandikiza subsitances hewa kwa manufaa ya wachache, mbinu zile zile za ccm. haitazamwi outside the box
 
Baraza kuu la waislam Tanzania(BAKWATA), na Baraza kuu la Answar suna Tanzania(BASUTA), kwa pamoja wamelaani kitendo cha viongozi wa CDM Kumvua hijabu DC Fatuma kimario wamesema kitendo hicho walichofanya chadema kwa mujibu wa uislam ni kama wamewadhalilisha waislam wote Duniani kwa hiyo amewataka viongozi wa CHADEMA kuwaomba radhi waislamu.

Naibu mufti akiwa mjini Tabora alisema Fatuma ana imani yake japo ni DC, heshimuni imani yake kwani waliomchagua wanajua kuwa imani yake inamtaka avae hijab alisema sheikh mohamed issa wa Answar Sunna.

CHANZO: Taarifa ya habari Radio Imaan

Mimi sioni sababu ya kuwabembeleza watu ambao hawajui waumini wao wanamaisha gani. Tunaomba kama vijana wa kiislamu mko humu vitu vingine muwe mnakataa na kuwaonyesha nia yenu sio kila kitu matamko tu, kunasiku mtabanwa na mtatoa tamko nalo litadharauliwa, tutaona ni kawaida yao.

Achaneni nao kila mtu anatetea ugali wake nyumbani kwake sisi tupambane kuikomboa nchi yetu mikononi mwa hawa wakoloni weusi. Vijana wengi waislamu walishaelewa tunakokwenda na tulikotoka. Hao wanaoendelea kuomba chumvi mpaka leo waache waendelee kutembeza bakuli kwa majirani sisi vijana tusonge mbele. Lazima tutambue dini zote tumeletewa tusidanganyane na hakuna mtu ambaye alisha lala kanisani au msikitini akaletewa chakula huko ni lazima ufanye kazi ndio ushibe.

Na ndio maana mungu alisema wewe kiumbe nimekupa utajiri wangu wote ukautumie upate kuishi, akamwacha huru, sasa nyinyi mnatuambia mambo ya hijabu labda tuwaulize huko Pakistani, Libya, Misri wanakovuliwa kila kukicha wanafanywa nini? Nyinyi wazee wa matamko tumesha wachoka. Tutumie akili tulizopewa kwa kutafuta maendeleo na rasilimali zetu mungu alizo tupa kwa amani bila kuingiza mambo ya dini na jinsia tufanye kazi kwa pamoja.

Wenyewe asilia wa hizi dini zimewashinda nyinyi mnajifunika funika nazo, hapa hafunikwi mtu lazima vijana tuamke kwa pamoja si wakristo si waislamu tujenge nchi yetu na kesho tujivunie nchi yetu. tuachane na hao wanaopenda kuishi kwa kutegemea wafanyiwe kazi. Na kama waislamu wakiendelea hivi inamaana wanataka kuturubisha kwenye ukoloni wa watu weupe. Waliosoma vizuri historia wanajua wapelelezi, wamisionari na wafanyabiashara walimfunika vipi mwafrika. Leo wanaturudisha huko huko.
 
Ndiyo maana watu wenye akili na busara walitoa ushauri kwa Mkapa hasirudi katika majukwaa ya siasa uchwara za CCM! Sijui miaka minne ijayo kama tutakua hatujachinjana. Lakini kwa makada wote wa CCM mnaotawanya siasa za udini,mkumbuke vita haina macho! Hakuna atakayepona pale tutakapo anza kuvuna hii mbegu mnayoipalilia sasa.
 
Katika majadiliano haya, yalianza na kadhia ya BAKWATA na BASUTA kutaka kuombwa radhi na CDM, lakini kadiri majadiliano yanavyoendelea, tumewawacha wahusika (BAKWATA, BASUTA kama vile hawa ni wawakilishi wa waislamu wote, na CDM kama kwamba ni chama cha wakristo). Tunakwenda wapi? Hatuoni kwa kufanya hivi tunajitenga na sifa ya kuwa Great Thinkers?

Hivi BAKWATA na BASUTA wanawawakilisha waislamu wote au ni kikundi cha wachache kujali maslahi yao?
Hivi CDM ni chama cha Kikristo au ni chama cha kuwakomboa Watanzania wote?
Hivi hakuna waislamu katika CDM? Ikiwa wamo, hawa ni sehemu ya BAKWATA na BASUTA?

Ndugu zangu, tuwacheni udini tushughulike na kujenga nchi, tuishughulikie wanaoiua Tanzania ambapo naamini si waislamu wala wakristo, bali walafi wasiojali maslahi ya Watanzania, watoke dini wanayotoka.

MAMMAMIA, Nakubaliana na wewe kabisa. Na jambo kubwa la kujiuliza, ni kwanini BAKWATA na BASUTA hawakulaani mauji ya mwislama 'asiye na hatia' yaliyofanywa na polisi tarehe 5 January 2011 huko Arusha? Je marehemu huyo hakuwa sehemu ya BAKWATA? Na kama hakuwa sehemu ya BAKWATA hawa mabwana wanaotoa wapi mamlaka ya kuongea kana kwamba wao wanawakilisha waislam wote?

Pengine BAKWATA na BASUTA wangetuelewesha kama kuuwa mtu asiye na hatia inakubalika katika dini wanayodai kuisimamia? Na kama jibu ni la, basi lini watatoa kauli ya kuitaka serikali na jeshi la polisi kuomba msamaha? Kwa vyovyote vile, BAKWATA hawana historia ya kutetea maslahi ya waislam sana sana mtu anaweza kuwafananisha na wachumia tumbo wanaotumia sytle ya Kinyonga katika mawindo yao.
 
Baraza kuu la waislam Tanzania(BAKWATA), na Baraza kuu la Answar suna Tanzania(BASUTA), kwa pamoja wamelaani kitendo cha viongozi wa CDM Kumvua hijabu DC Fatuma kimario wamesema kitendo hicho walichofanya chadema kwa mujibu wa uislam ni kama wamewadhalilisha waislam wote Duniani kwa hiyo amewataka viongozi wa CHADEMA kuwaomba radhi waislamu.

Naibu mufti akiwa mjini Tabora alisema Fatuma ana imani yake japo ni DC, heshimuni imani yake kwani waliomchagua wanajua kuwa imani yake inamtaka avae hijab alisema sheikh mohamed issa wa Answar Sunna.

CHANZO: Taarifa ya habari Radio Imaan
Nilidhani wangemlaani huyo mwanamke kwa ajili ya umalaya wake wa kisiasa! Baadala yake wanakurupuka na hoja hafifu mithili ya watoto walio na mtindio wa ubongo! Huyo Mufti anayo elimu gani jamani. Mbona ni kiloja!
 
Jamani mbona mnapenda kukuza hata mambo madogo? Tangu lini kuvua hijab ni kuwa uchi? Ingekuwa hivyo si ingekuwa balaa? wanawake wangapi wa kiislamu wanaranda mitaani bila hijab? Au mtu akiwa DC ndio anakuwa muislamu sana? Yawezekana hijab ilivuka bahati mbaya ktk hizo prukshani za kubishania alichoenda kukifanya huko!

Kwa mujibu wa imani ya Bi Fatuma, kuvuliwa mtandio ni kuwekwa uchi. Na yes kwa mujibu wa anachokiamini ni kuwa wanawake waislam wasiovaa nguo za kujistiri pamoja na mtandio wako uchi (kwa mujibu wa dini yake)

Katiba ya jamhuri inamlinda katika imani yake hiyo na kuwataka wengine pia kutompokonya haki yake hiyo ya msingi.

Tunachoweza kusema hapa ni kuwa labda hawakumvua kwa kukusudia lkn cha kujiuliza jee ingelitokea purukushani na blouse yake kuchanika na kuonyesha maungo yake ya ndani wangefanyaje?

Iwapo Jibu ni wangemtafutia japo kanga kumsitiri, inamaana wamedharau hadhi ya mtandio wake kwake na hawakuona umuhimu wa kumsitiri kutokana na ujinga wa kutoelewa umuhimu wa kutomvunjia haki yake ya msingi (sitaki kusema ujinga wa kudharau uislam)

Iwapo Jibu ni wangemtoa hivyo hivyo uchi, inathibitisha tu kuwa safari ya ukombozi bado ni ndefu, kwani kikombolewa na mtu aso heshima kwa sheria, mdhalilishaji wa wanawake, asiyejali matokeo ya matendo yake ni sawa na kutokombolewa kabisa
 
ndugu zanguni hapa tunakosea udhalilishwaji ule hata mie sikubaliani nao.
inakuwaje mama yako anavuliwa chupi then unasherehekea? huu ni ushenzi lazima upinge. hata kama ni siasa sawa lakini ni utovu wa nidhamu.
AU MTU ANA NYONGWA ALAFU UNAFURAHIYA HATA BILA SHERIA KUCHUKUA MKONDO WAKE
najua wangeweza kumkamata kiungwana na kumuadabisha.
WALICHOFANY NI UDHALILISHAJI WA HALI YA JUU, ni kama padri kuvuliwa kofia na joho lake
UNACHEZEA HADHI YA MWANAMKE,
TUKIKUBALIANA NA KITENDO HICHO CHA AIBU KILICHO FANYIKA NI SAWA NA KUONA MAMA YAKO ANAVULIWA CHUPI / ANABAKWA ALAFU UNAFURAHIA
tuwe makini tusije tukapotea kabisa hata kwenye maadili yetu ya kitanzania.
 
Ajabu na kweli ! Wakiambiwa hawana akili wanakuja juu !! Mwanangu kazania kusoma upevuke kichwani.
 
Duh, nimepoteza muda kupita humu. Ushungi unaitwa Hijab eti kwa sababu kavaa Fatuma ! na kesho suruali iliyokatika zipu itaitwa kanzu eti kwa sababu kavaa Shabani. Kazi kweli kweli.
 
Duh, nimepoteza muda kupita humu. Ushungi unaitwa Hijab eti kwa sababu kavaa Fatuma ! na kesho suruali iliyokatika zipu itaitwa kanzu eti kwa sababu kavaa Shabani. Kazi kweli kweli.

jitoe jf, unapoteza muda au unatakiwa uelimishe
acha kukimbia tatizo
ukweli ndo huo
 
Duh, nimepoteza muda kupita humu. Ushungi unaitwa Hijab eti kwa sababu kavaa Fatuma ! na kesho suruali iliyokatika zipu itaitwa kanzu eti kwa sababu kavaa Shabani. Kazi kweli kweli.

ndio kwani vile wanavyo vaa masista kanisani tunaitaje????????

hicho ndicho haswa
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom