Bakwata, Basuta Walaani DC Kuvuliwa Hijabu

Bakwata, Basuta Walaani DC Kuvuliwa Hijabu

Status
Not open for further replies.
swali langu ni kwamba, kwa mambo ya msingi, BAKWATA imekuwa ikipuuzwa na waislamu kwa kuwa haijaweza kusimamia vizuri maslahi yao, je waislamu ni kweli mko pamoja na BAKWATA au ni BAKWATA ya CCM kama siku zote mnavyosema?

kuvuliwa hijabu kwa mtu aliyekosea matakwa ya democrasia si bora na afadhali mtu aliyekamatwa wizi kukatwa mkono au kukatwa uume kwa mjibu wa dini ya kiislamu na kadhi yao?

Suala lako halitaweza kujibiwa kamwe kwa kuwa hakuna mtu anaeweza kuwasemea waislam wote wa Tanzania. Hilo ni moja

Pili nafikiri si suala la Waislam kuiamini BAKWATA au la, ni suala la Jee ni haki kwa Bakwata kutetea haki ya Muislam aliyevuliwa hijab/mtandio?

Hoja za wengi ni kuwa Mama Fatuma ni mhalifu kwa hiyo Bakwata wangempinga kwa uhalifu wake. Suala linalokuja jee ni haki kwa mtu kunyimwa haki zake zote za msingi kwa sababu ni mhalifu katika kosa moja?

Note: Sipo kutetea haki za wavaa hijab wala haki za Bakwata, nipo kutetea haki za raia wa Tanzania. Raia wa Tanzania ana haki ya kutodhalilishwa regardless yeye ni jambazi au la. Na nitatetea haki ya mtu mwizi akikamatwa kuvuliwa nguo na kukimbizwa mtaani akiwa uchi wa mnyama, na kama ninavyotetea wasichana wanaopita njiani na nguo fupi na watu kuwaghasi na kuwanyanyasa na kuwanyima haki yao ya msingi kama raia.

Hatuwezi kuongoza wengine iwapo hatuoni faida ya kulinda na kuwatimizia wengine haki zao za msingi kama raia
 
nadhani tunashindwa kuelewa kuwa haki za msingi za mtu hazifutwi tu kwa sababu ana kosa jengine. Kibaka, jambazi, changudoa na mtu mwenye sifa zozote za uhalifu ana haki sawa ya kutimiziwa haki zake za msingi katika wakati wote kama alivyokuwa na haki raia mwema asie na doa la uhalifu. Katiba haisemi kuwa haki za msingi za raia zinafutika iwapo atashutumiwa/atakamatwa kwa kosa la uhalifu.
Haki hiyo ndio inalazimisha mhalifu kupatiwa wakili na serikali licha ya kuwa alikamatwa red handed akifanya uhalifu. Haki hiyo hiyo inamtaka jambazi aliyepigwa risasi baada ya kuua raia asiyekuwa na hatia, kupatiwa matibabu hospitali ili kuokoa maisha yake.

Vyama vya kiislam vina haki ya kumtetea kwa vile ni muislam mwenzao na vyama vya wanawake vina haki ya kumtetea kwa vile ni mwanamke mwenzao, ccm ina haki ya kumtetea kwa vile ni ccm mwenzao.

Ikiwa bakwata na wengineo hawatimizi wajibu wao kwenye mengine, bado hakuizuwii kutimiza wajibu wao kwenye hili.

umeneana vema.
Haki ya mtu haipokonywi kwa namna yoyote ile, ni sawa kabisa nakubaliana na wewe.
Sasa kwa nini mjadala umewekwa ionekane ni uislamu dhidi ya ukristo? Kwa nini hawa bakwata wanadai chama kiombe radhi tena si kwa mtu aliyedhalilishwa bali uislamu wenyewe?

Kama wangesema wabunge wa chadema wamemkosea DC, ingeleta maana lakini wameenda mbali zaidi, wameukosea uislamu-huu sasa ni udini, ni zaidi ya udhalilishaji wa mtu.

Kama wanadai uislamu umekosewa hata hiyo coment yako haina maana lakini kama wanadai dc ndo kakosewa, basi coment yako ina maana kubwa sana
 
Suala lako halitaweza kujibiwa kamwe kwa kuwa hakuna mtu anaeweza kuwasemea waislam wote wa Tanzania. Hilo ni moja

Pili nafikiri si suala la Waislam kuiamini BAKWATA au la, ni suala la Jee ni haki kwa Bakwata kutetea haki ya Muislam aliyevuliwa hijab/mtandio?

Hoja za wengi ni kuwa Mama Fatuma ni mhalifu kwa hiyo Bakwata wangempinga kwa uhalifu wake. Suala linalokuja jee ni haki kwa mtu kunyimwa haki zake zote za msingi kwa sababu ni mhalifu katika kosa moja?

Note: Sipo kutetea haki za wavaa hijab wala haki za Bakwata, nipo kutetea haki za raia wa Tanzania. Raia wa Tanzania ana haki ya kutodhalilishwa regardless yeye ni jambazi au la. Na nitatetea haki ya mtu mwizi akikamatwa kuvuliwa nguo na kukimbizwa mtaani akiwa uchi wa mnyama, na kama ninavyotetea wasichana wanaopita njiani na nguo fupi na watu kuwaghasi na kuwanyanyasa na kuwanyima haki yao ya msingi kama raia.

Hatuwezi kuongoza wengine iwapo hatuoni faida ya kulinda na kuwatimizia wengine haki zao za msingi kama raia

Kinadharia you are right bt kiuhalisia you are half right.
You know, kwa jinsi wengi tulivyokosa imani na jinsi wahalifu wanavyolindwa na system, ndiyo msingi wa wengi kupongezwa kwa DC kufanyiwa vile, tena ile haitoshi angefanyiwa kitu mbaya zaidi ili iwe fundisho kwa DCs/RCs waliovaa joho la kuisaidia serikali/umma wakati underwear zao ni kuibust CCM kwa njia haramu kama ya DC yule.

Nakwambia angefanyiwa kitu kibaya zaidi ingesaidia kwani wameshindwa kuusaidia umma wa TZ, na kuendekeza ujinga wa CCM. Chukua mfano wa DC wa kahama aliyeripotiwa kumtimuwa diwani wa CDM kwenye sherehe za kutimiza miaka 50 ya uhuru
 
CHADEMA wawaombe radhi waislam na mama fatuma kimario kwani kumvua hijabu ni udhalilishaji tunaona ulaya wanavyofanya juu ya waislam kuwadhalilisha, je? na chadema wanaiga hao wazungu?
 
Mkuu usi-mislead watu Hijab ni tofauti na mtandio

Hijab kwa mwanamke wa kiislam ni vazi la kidini na maamrisho kutoka kwa Muumba

Huwezi kulinganisha ni mitandao ya nuns ambayo in fact si amri ila utashi wa mvaaji...

Kudhalisha Hijab ni kudhalilisha alama za dini yetu Tukufu.

Kwani kuomba msamaha inawagharimu nini au ndio mnajidhihirisha chuki zenu kwa waislamu..total manifestation


Hapo kwenye red umejionyesha kuwa wewe ni mbabaishaji manake kwenye mchango wako mmoja umesema wewe si Muislamu.Sasa ukishaona hivyo ujue wewe ni hovyo kabisa.
 
Suala lako halitaweza kujibiwa kamwe kwa kuwa hakuna mtu anaeweza kuwasemea waislam wote wa Tanzania. Hilo ni moja

Pili nafikiri si suala la Waislam kuiamini BAKWATA au la, ni suala la Jee ni haki kwa Bakwata kutetea haki ya Muislam aliyevuliwa hijab/mtandio?

Hoja za wengi ni kuwa Mama Fatuma ni mhalifu kwa hiyo Bakwata wangempinga kwa uhalifu wake. Suala linalokuja jee ni haki kwa mtu kunyimwa haki zake zote za msingi kwa sababu ni mhalifu katika kosa moja?

Note: Sipo kutetea haki za wavaa hijab wala haki za Bakwata, nipo kutetea haki za raia wa Tanzania. Raia wa Tanzania ana haki ya kutodhalilishwa regardless yeye ni jambazi au la. Na nitatetea haki ya mtu mwizi akikamatwa kuvuliwa nguo na kukimbizwa mtaani akiwa uchi wa mnyama, na kama ninavyotetea wasichana wanaopita njiani na nguo fupi na watu kuwaghasi na kuwanyanyasa na kuwanyima haki yao ya msingi kama raia.

Hatuwezi kuongoza wengine iwapo hatuoni faida ya kulinda na kuwatimizia wengine haki zao za msingi kama raia
Nina wasiwasi we ndo uliyemchapa Mzee wetu Mwinyi makofi!! Je unataarifa,kuhusiana na Haram Boko uko Nigeria??wametaadharisha kulipua Universities,je ni wanafunzi wa dini gani watakufa?jibu ni wote.Je,CCM inapowatumia Waislam kama ''Toilet papers'' hamshuti,upeo wenu huwa ukoje?
Kama mnaona Tanzania si nchi ya amani kwenu,jiungeni na ndugu zenu wa Somalia,Sudan,North Nigeria,Afghan,Iraq,Pakstan ili mkamwagane damu,ili mpate'' thawabu''kwa allah!
 
CHADEMA wawaombe radhi waislam na mama fatuma kimario kwani kumvua hijabu ni udhalilishaji tunaona ulaya wanavyofanya juu ya waislam kuwadhalilisha, je? na chadema wanaiga hao wazungu?
Mbona mke wa mtu Fatma Rajabu alivuliwa hijabu na Mwigulu tena gesti hatujasikia cha Basuta wala bakulutu kutoa tamko acheni unafiki wenu njaa zinaifanya dini yenu hadi inapoteza maana.
 
chadema waombe radhi tu. lkn bakwata hawa wanafiki, walikuwa kimya waislam wa mwembe chai walipodhalilishwa na ccm
Waombe radhi lini wakati hizo siku tatu zimeshapita mtafanya nini kila siku huyo shehe ubwabwa Matope kutishia kuandamana. Andamaneni basi tuone kama hamjaacha hijabu barabarani maana FFU hawajui huyu kavaa hijabu wala buibui.
 
Nina wasiwasi we ndo uliyemchapa Mzee wetu Mwinyi makofi!! Je unataarifa,kuhusiana na Haram Boko uko Nigeria??wametaadharisha kulipua Universities,je ni wanafunzi wa dini gani watakufa?jibu ni wote.Je,CCM inapowatumia Waislam kama ''Toilet papers'' hamshuti,upeo wenu huwa ukoje?
Kama mnaona Tanzania si nchi ya amani kwenu,jiungeni na ndugu zenu wa Somalia,Sudan,North Nigeria,Afghan,Iraq,Pakstan ili mkamwagane damu,ili mpate'' thawabu''kwa allah!

Una uhakika unazungumza na mimi kweli? Manake nadhani umekosea njia hivi.
 
yule mama hakuvaa hijab,alivaa sketi na blauzi na kitambaa cha kichwani. WAISLAM TUWE MAKINI KUTUMIWA NA CCM,MA DC NA MA RC WOTE NI KADA WA CCM,TUMESAHAU MADHILA YALIYOFANYWA NA CCM JUU YA UISLAM?IOC,KADHI ILIWEKWA KWENYE ILANI YA CCM 2005 JUZI JK KATUGEUKA,PIA HATA KUDAI KUVAA SCURF WANAFUNZI WA KIKE TULIPIGWA MABOMU WAKATI WA MWINYI!PIA HATUJIULI DC ANATOKANA WAPI NA MAMBO YA UCHAGUZI MPAKA AWE NA AJENDA HIYO?WAISLAM TUTABAKI NA MATAMKO MPAKA LINI?TUMEFUNDISHWA KUZUIA JAMBO KWA MIKONO YETU,IKISHINDIKANA KWA MANENO NA MWISHO KULICHUKIA KABISA MOYONI!Juzi waislam wamefariki kwa uzembe ktk ajali ya mv spicer mbona hamkutoa tamko?
 
Kama kunakosa lilifanywa na CDM basi haki ni lazima ipatikane kwa sheria za Jamhuri wa Muungano wa Tanzania. Nadhani sii busara kuvifanya vyombo/taasisi za kitaifa zisizokuwa za kidini kuanza kuwajibika kwa taasisi za kidini.

Ni busara kuichia mahakama ikafanya kazi yake kufikia suala hili na sio dini kutumia uchochoro huu kwa manufaa ya kisiasa ambayo yanaweza kuwa nyuma ya ajenda ya watu wachache na sio taifa letu.

Maswali madogo tu,
1. Je, Mkiombwa radhi mtakuwa na uwezo wa kufuta kesi mahakamani?
2. Je, mmesikiliza pande zote mbili uli kujiridhisha kuwa kosa lilikuwa la cdm?
3. Je, mnaupande wowote katika siasa za nchi pamoja na Igunga?
 
Kwa wote mtaopata nafasi ya kusoma mawazo yangu,

Bakwata na Basuta wamekosea kwa kweli na hata kama wangekuwa na nia nzuri wangetakiwa watumie hekima. Mojawapo ya sifa kuu ya kuwa kiongozi ni kuwa na hekima na hasa unapo react kwa habari uliyoisikia kutoka upande mmoja. Viongozi wa dini wana jukumu kubwa la kuunganisha jamii lakini kwa muda fulani sasa wamekubali kutumika na wanasiasa kuigawa jamii. Kilichotekea kwa Bakwata na Basuta ni mkokotoo wa madhara ya kampeni za uchaguzi uliopita. Hii kutu haijawatoka viongozi wengi wa dini. Kwa nini viongozi wanatakiwa kutumia hekima hasa kwa kesi hii ya Igunga? Sababu zangu ni hizi zifuatazo:

1. Tukio la mkuu wa wilaya ni tukio la taharuki (chukulia kweli huyu mama alivuliwa hijabu/kilemba/kitambaa/mtandio). Sidhani kuwa watu walioenda pale walienda kwa madhumuni yaliyopangwa (contemplated) kwamba wanaenda kumvua kilemba mwanamke muislamu ili wamdharilishe.

2. Katika matukio ya rabsha/vurugu/hasira/kupambana (kutegemea sababu iliyowafanya wananchi wale waende kumkamata) kitu chochote kinaweza kutokea saa zingine hata kuumia au kupoteza maisha. Huwezi kuhitimisha kuwa wahusika walidhamiria kufanya hayo matokeo. Polisi wanaposhughulikia uhalifu mambo mengi hutokea kupoteza mali, majeruhi au hata vifo. Nivigumu sana kuwatuhumu moja kwa moja kwamba walienda kufanya kile kilichotokea.

3. Sasa hivi Igunga ni wakati wa uchaguzi na hali ya mambo ni tete. Vyama vyote vinavogombania vina wafuasi wa dini mbalimbali ikiwemo na dini yetu ya Uislamu. Makosa yanaweza kutendwa na tasisi, jamii, kikundi au mtu mmoja mmoja. Ndiyo maana hata mahakamani kwa kesi hii wamepelekwa watu kama mtu mmoja mmoja na siyo chama. Kama kweli itadhihirika pasipo shaka yoyote kwamba walitenda makosa hayo basi watahukumiwa kama mtu na siyo chama. Makosa yoyote hutendwa na watu wowote ndiyo maana magereza, polisi, mahakama hakuna dini.

4.Unapotoa tamko kwamba Bakwata na Basuta watawaambia waislamu wote wakiadhibu Chadema ni upotokaji mkubwa wa maadili ya dini. Kabla ya kutoa tamko kama hilo ilitakiwa hekima tu ya kuwaita viongozi wa chama hicho na kuongea nao kupata undani upande wao badala ya kutoa tamko lenye mrengo wa kisiasa na kupendelea chama kingine. Viongozi wa dini wanatakiwa kutenda haki na si kuchukua ushabiki wa kimakundi. Kiimani na kiroho kuwaadhibu chadema (nadhani wana maana waislamu tu tusikipigie kura) kwa sababu ambayo haina uthibisho wa kiroho kuna tija gani kwetu waislamu?

5. Mwenyezi Mungu Subhanahu Wataala ana vipomo vikali kuliko sie wanadamu. Na Yeye huona tofauti kuliko sisi wanadamu na kwa hivyo kwa imani yetu Mungu anajua kwa bayana Yule mama alikuwa anafanya nini pale hata kama atakuja na hadithi ya kuficha. Masheikh wetu hawana undani wa siri ya kile alichokuwa akikitenda pale wengine tunatia shaka tu lakina kwa hakika Maulana anajua nini mama yule alikuwa akikifanya pale. Nina mashaka sana na hukumu ya Maimamu wetu inaweza isiwe hukuma ya Mungu. Na kama hawana uhakika kwa nini basi kujiingiza matatizoni na kuwatia doa ambalo lingeweza kuepukwa?

6. Kama kweli Bakwata na Basuta wana nia isiyo ya kisiasa na ya kutowagawa wananchi kufuata dini zao, kwa nini tamko lao lisingewasihi watu wote bila kujali itikadi zao wakiadhibu Chadema? Je nikisema kwamba wanatumiwa na na chama fulani kukisafishia njia nitakuwa nakosea? Ndugu Nape Nnauye kwenye tamko lake juzi aliweka mbele sana habari ya hijabu waislamu wenye hekima tukajua nini kinachotafutwa hapa na CCM wanafurahi sana Bakwata na Basuta wameichukua hiyo agenda.

7. Viongozi wa Bakwata na Basuta, kama Waislamu wote tutakubali maelekezo yenu tusikipigie kura Chadema na kila mmoja wetu akatii, je tuna hakika nani atashinda kwenye uchaguzi ule? Je, waumini wa dini zingine wakiamua vinginevyo itakuwaje? Je Taswira kwa taifa zima itakuwaje siku za usoni?

Mwisho nawasihi tena viongozi wetu wa dini tuwe na hekima kushughulikia mambo tete kwenye jamii badala ya kusukumwa na jazba za makundi fulani fulani. Tutailinda jamii, na tutaheshimika na viongozi wa kisiasa pia. Viongozi wa siasa nao wawe makini kutowaingiza viongozi wa dini kwenye mirengo ya kisiasa. Tishio walilolitoa Bakwata na Basuta si jambo la kuchekelea hata kidogo, linalenga kubomoa jamii na kuimarisha/kupanua ufa wa udini ambao kwa sasa unaendelea kwenda kina zaidi. Tumwombe Mungu alinusuru taifa hili.

Mungu Ibariki Tanzania, Mungu Ibariki Libya.

umesema vizuri sana... ila hapo kwenye RED umeharibu (uchonozi fikra)
 
Ndo matatizo ya kuwapa vyeo wasiostahili. Wanadhani ndo muda wa kuonyesha waliowapa vyeo kuwa wanatetea maslahi yao. Nadhani waliomkamata walimtetendea kwa heshima
 
Hivi mzee Mwinyi alivyozabwa kibao kwenye hutba na kijana wa kiislam....

kitendo cha ukosefu wa nidhamu kwa rais mstaafu na akasamehe,

sikuona such 'tamkos' au malumbano meeeengi, tulikemea na mzee wa watu alipotezea

well said madam,nashangaa kwa huyu dc,tena cha ajabu kwa yule aliempiga mwinyi kuna watu walikuwa wanamsupport sana,NA HAKUNA MTU ALIETOA TAMKO
 
Alijitakia huyo,kwani zile vurugu za mwembechai barakhashia ziliishia wapi?
 
Hijabu iko wapi hapa?

igunga.jpg
 
Mkuu wangu unanifanya naanza kuamini maneno ya wakristu kuhusu elimu za waislaam na yawezekana kweli imechangia sana kuwa wajinga pamoja na kwamba Mtume alisistiza elimu...

Mkuu wangu, hijab ni vazi la kike na limesisitizwa kwa malengo na makusudi kama vile mzungu anavyosisitiza kuvaa tai kwa mwanamme. Ina maana yake na sababu zake mwanamke kuvaa hijab, na akivaa haimfanyi kuwa muislaam isipokuwa tunafuata mafundisho kama vile wewe unapovaa suruali ama nguo inayovuka magoti ni maagizo ya mitume vile vile ktk mavazi.

Na kisha ebu waulize hao masheikh je mwanamke aliyevaa mtandio wa Khanga kufunika kichwa chake ni Hijab? watakwambia hiyo sio Hijab isipokuwa Hijab ni mtandio ule ulotoka Dubai au Oman na ndivyo mnavyoitafsiri Kanzu kuwa vazi la waislaam. Kesho mtu akivamia na kuchaniwa kanzu basi ni kuudhalilisha Uislaam..
Hawa waarabu wamewaharibu sana kiasi kwamba hata majina mnaamini kabisa ni majina ya kiislaam mtu akiitwa Omar au Hamza lakini sii yule anayeitwa Richard, wakati huo huo huwezi kunambia swahaba yeyote wa mtume aliyebadilisha jina lake baada ya kuuukubali Uislaam kwani majina hayo waarabu wa imani zote huyatumia. Baba yake mtume aliiitwa Abdallah na hakuwa Muislaam lakini ukienda Bongo ukisema jina lako Abdallah basi lazima utakuwa Muislaam.. Tembeeni mkaizunguke dunia myajue mengi jamani, waarabu wanayatumia majina haya bila kujali dini zao. Jamani eeeeh Uislaam ni Imani na ibada, majina, hijab na kanzu sio Uislaam ...Abu Talib mtamweka wapi nyie!

Nitarudia kusema kwamba Hijab ni vazi la kike na limesisitizwa na mitume kwa wanawake wote (ustaarabu) na sii Uislaam, bali jinsi ya mwanamke to carry herself and be respected kama ilivyo hulka ya kidunia tunapomwona mwanamme amevaa shati na tai, tai inaongeza heshima fulani hata kama hakuna sababu ya maana kwa mtu asiyevaa tai, lakini ukweli utabakia kwamba mvaa tai atatazamwa na kupokelewa na heshima fulani ndivyo inavyokuwa kwa mwanamke na Hijab..Hii ni ktk moja ya mapungufu ya kibinaadam hatujakamilika.

Ama kweli mtume alisikitika sana na kusema hakika Umma wake ni wachache sana wataingia peponi!...na hakika dalilizote zinajionyesha, hapo hapo mimi naongezea kusema Uislaam ni dini isiyokuwa na watu, hali Wakristu ni watu wasiokuwa na dini...
- Ukweli unauma, mtanisamehe nyote.
Wewe unasema wenzako wameharibiwa sana na Waarabu....sasa wewe umeharibiwa na nani? ni mwarabu ndiye aliyekwambia kwamba ukristo siyo dini? Umezungumza kama wale malofa wanaotupigia kelele kila siku na ma vipaza sauti yao.....makafir makafir..!
Dini ni imani tu ndugu yangu....mtu anaweza kuabudu hata mti tu ila kama anafuata the golden rule basi anakuwa safi!
 
Mbona mke wa mtu Fatma Rajabu alivuliwa hijabu na Mwigulu tena gesti hatujasikia cha Basuta wala bakulutu kutoa tamko acheni unafiki wenu njaa zinaifanya dini yenu hadi inapoteza maana.
Hii ya Fatma Rajabu na mwigulu una picha yake?.Halafu ya hao watu nadhani ni binafsi zaidi na watajibu dhambi zao kwa namna nyengine.
Hii ya Chadema na Fatma Kimaro ina uzito mkubwa hasa kwamba imefanywa na chama kinachokusudia kuingia tena kwenye uchaguzi mkuu ili sera zake ziongoze nchi yenye waislamu wengi.
Iwapo kwenye kampeni munaonesha dharau kwa waislamu kiasi hiki kwa mkuu wa wilaya hali itakuwaje kwa waislamu mmoja mmoja ambao ni wanyonge sio kama DC pindi mukipewa kura kuingia ikulu.
Waislamu wa taasisi yoyote ile watakuwa wajinga kama watashindwa kuliona hilo mapema na kutahadharishana kwa mara nyengine.Kumbe walikuwa sahihi kwenye uchaguzi uliopita.
Anayedhani waislamu wana uoni finyu ajaribu kuusoma uislamu angalau kidogo.
 
yule mama hakuvaa hijab,alivaa sketi na blauzi na kitambaa cha kichwani. WAISLAM TUWE MAKINI KUTUMIWA NA CCM,MA DC NA MA RC WOTE NI KADA WA CCM,TUMESAHAU MADHILA YALIYOFANYWA NA CCM JUU YA UISLAM?IOC,KADHI ILIWEKWA KWENYE ILANI YA CCM 2005 JUZI JK KATUGEUKA,PIA HATA KUDAI KUVAA SCURF WANAFUNZI WA KIKE TULIPIGWA MABOMU WAKATI WA MWINYI!PIA HATUJIULI DC ANATOKANA WAPI NA MAMBO YA UCHAGUZI MPAKA AWE NA AJENDA HIYO?WAISLAM TUTABAKI NA MATAMKO MPAKA LINI?TUMEFUNDISHWA KUZUIA JAMBO KWA MIKONO YETU,IKISHINDIKANA KWA MANENO NA MWISHO KULICHUKIA KABISA MOYONI!Juzi waislam wamefariki kwa uzembe ktk ajali ya mv spicer mbona hamkutoa tamko?

wakumbushe wote wanaojiita wanzi wa bakwata na ansar suna.

Bakwata cku zote wanafanya kazi za chama
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom