Bakwata, Basuta Walaani DC Kuvuliwa Hijabu

Bakwata, Basuta Walaani DC Kuvuliwa Hijabu

Status
Not open for further replies.
Mkandara nisaidie kidogo, alosema mwanamke avae hijab ni mtume/mitume au Kur-an?

Kuvulia hijab inaweza kuwa si kudhalilisha uislam lkn ni kumdhalilisha aliyevuliwa, sawa na mwanamke mwengine kuvuliwa blouse au mwanamme kuvuliwa suruwali.

Ikiwa mtandio kwake ni vazi la kila siku basi amedhalilishwa kuvuliwa huko.

Jee vyama vya Kiislam vina haki na wajibu wa kumtetea? Bila ya shaka vina haki hiyo kwa vile aliyedhalilishwa ni Muislam na hiyo ndio kazi yao.

Vyama vya kutetea haki za wanawake pia vingetoa tamko nisingelishangazwa kwa vile wangelikuwa wanatetea haki ya mwanamke mwenzao
 
Mkandara nisaidie kidogo, alosema mwanamke avae hijab ni mtume/mitume au Kur-an?

Kuvulia hijab inaweza kuwa si kudhalilisha uislam lkn ni kumdhalilisha aliyevuliwa, sawa na mwanamke mwengine kuvuliwa blouse au mwanamme kuvuliwa suruwali.

Ikiwa mtandio kwake ni vazi la kila siku basi amedhalilishwa kuvuliwa huko.

Jee vyama vya Kiislam vina haki na wajibu wa kumtetea? Bila ya shaka vina haki hiyo kwa vile aliyedhalilishwa ni Muislam na hiyo ndio kazi yao.

Vyama vya kutetea haki za wanawake vingetoa tamko nisingelishangazwa kwa vile wangelikuwa wanatetea haki ya mwanamke mwenzao
Hili ndilo neno la leo!
 
Hawa waarabu wamewaharibu sana kiasi kwamba hata majina mnaamini kabisa ni majina ya kiislaam mtu akiitwa Omar au Hamza lakini sii yule anayeitwa Richard, wakati huo huo huwezi kunambia swahaba yeyote wa mtume aliyebadilisha jina lake baada ya kuuukubali Uislaam kwani majina hayo waarabu wa imani zote huyatumia. Baba yake mtume aliiitwa Abdallah na hakuwa Muislaam lakini ukienda Bongo ukisema jina lako Abdallah basi lazima utakuwa Muislaam.. Tembeeni mkaizunguke dunia myajue mengi jamani, waarabu wanayatumia majina haya bila kujali dini zao. Jamani eeeeh Uislaam ni Imani na ibada, majina, hijab na kanzu sio Uislaam ...Abu Talib mtamweka wapi nyie!

Ama kweli mtume alisikitika sana na kusema hakika Umma wake ni wachache sana wataingia peponi!...na hakika dalilizote zinajionyesha, hapo hapo mimi naongezea kusema Uislaam ni dini isiyokuwa na watu, hali Wakristu ni watu wasiokuwa na dini...
- Ukweli unauma, mtanisamehe nyote.

mkuu kidogo niseme hii ni name calling, huwezi amini, mimi naitwa abdallah na ni mkristo, jina langu lingine ni hamza, jina la baba ni richard, sekondari na chuo nilipata shida coz kundi kubwa la watu walijua mimi muislam, wengine walidiliki kusema nimerudia shule na kuiba jina la mtu, aisee haya majina kweli yamezidi kutumbukiza ujinga kwa waafrika, siwezi kumuita mtoto wangu tena majina yenye asili ya waarabu au wazungu,
 
Baraza kuu la waislamu Tanzania BAKWATA limewataka viongozi wa chadema kuwaomba radhi waislam kwani kitendo walichokifanya wabunge wake ni udhalilishaji dhidi ya uislam kufuatia wabunge wake kumvua hijabu DC Fatuma kimario kwani udhalilishaji waliomfanyia ni kama wamewadhalilisha waislam wote Duniani alisema Naibu mufti.
Nadhani dini siyo kuvaa hijabu ila ni matendo mema ya staa na si kama huyu DC aliyejificha katika vazi la hijabu kumbe nia ni kuiba kura, je ndugu zangu hii ni sawa? Hata Padri si kanzu iliyo muhimu bali kile atendacho katika jamii kila siku kwa hiyo tukiongea sana juu ya kuvuliwa hijabu tukasahau ukafiri na dhuluma aliyotaka kufanya basi hatuitendei haki hata hiyo dini yetu.
 
Duuuu, hawa ndo walikuwa wanataka mahakama ya kadhi yenye nguvu....ya kisheria. Hijabu ni nini kwani? waislamu acheni malalmiko katika kila kitu fanyeni maendeleo bana! tumechoka na vituko vyenu
 
CCM inacheza sana na akili za waisilamu maana ni rahisi sana kuwanasa. Wao ukitaka kuwateka tumia dini tu hata kama jana uliwatoa ngeo kama ni mwenzao mtapatana. Nadhani pengine ndivyo wananavyo fundishwa(ubinafisi wa kidini mpendelee mwisilami mwenzako)
Cha ajabu ni kwamba hawaamini kwamba CCM kamwe hawataweza kutimiza matakwa ya waisilamu yaliyo kinyume na katiba ya nchi hii hata kama mwenyekiti wake ni mwiisilamu. Atawandanganya tu na mwisho wa siku atawaambia hayo ni mambo yenu fanyeni wenyewe na huo ndo ukweli.

Hakuna Raisi nchi hii hata kama atakuwa shehe,padre au mchungaji atakayekubali kuvunja katiba ya nchi kwa ajili ya kuipendelea dini moja dhidi ya nyingine. Wenzetu waisilamu hawataki kukubaliana na hili wanadhani Raisi akiwa mwisilamu basi anaweza kupendelea uisilamu kitu ambacho hakitakaa kitokee nchi hii!

Kama Raisi wa Tanzania anataka asimalize hata mwezi Ikulu basi apendelee dini yake kwa uwazi aone kama kundi la pili litaogopa na kukaa kimya.

Kama kuna waisilamu wanaona CDM haimtendei haki (japo haijawahi kuwa na mamlaka ya kutenda au kutowatendea haki watanzania) aendelee kubaki ccm kama anaona kwake issue ni dini zaidi kuliko vita vya ufisadi na maisha magumu tuliyonayo watanzania kwa sasa. Hakuna anayemlazimisha mtu kuwaunga mkono chadema ila ni watu wenyewe wameua kutoka mioyoni mwao.

Hatuwadharau wenzetu waisilamu ila Imekuwa too much utafikiri wao ni yule mtoto kitinda mimba ambaye hagusi hata kidogo analia 'mamaaaaaa eti ....... ananishikakichwani'! Ndugu zetu lazima wajiamini waondokane na ile inferiority comprex na kudhani kuwa kuna mtu anawdharau.

Inashangaza sana kwanini kunakuwa na watu wao hujihisi kunyanyaswa tu kila wakati bila hata kuyaona manyanyaso yenyewe.
But nina marafiki zangu tumesoma nao ni waisilamu lakini wanajiamini sana na ni wapenzi wa chadema wa kufa mtu.

ndugu zetu jiaminini kwanza bila hivyo itasumbua sana na hatutakaa tutatue matatizo ya msingi ya nchi yetu. Kumbukeni mtaendelea kutumiwa tu na ccm kama toilet paper wakati wa uchaguzi wakishapata mnabaki palepale labda na nyie muwe mafisadi wakati dini hairusu.

Tuweni kitu kimoja bila kujali dini zetu tumshughulikie adui wa watanzania wote ambaye ni ccm. Hata Kama baadhi yenu mtakataa bado Mungu akisema ndiyo hakuna atakayezuia.

Mungu ibariki Tanzania!

asanteh sana mkuu.umetoa mfano mzuri wa kitinda mimba.
 
hatuombi radhi ng'o! Kwanza nyie mna mchango gani kwenye chama chetu? Make nyie ni taasisi iliyoundwa na ccm kama ilivyo kwa uvccm,uwt nk.
Tukiwaomba radhi ni kama kuiomba radhi ccm,kitu ambacho ni mwiko kwetu!
Viva CDM!
Vilemba, hijab vinatumika kuvalia mabomu, halafu hawa jamaa kweli ni minute-numerals wapo watu ni waislam wajutia kujitambulisha hivyo kwa sababu ya upuuzi wa hawa na wengineo, hata rais si ni mwenzenu? do you remember aliwaambieni nini kwenye kumaliza kushinda njaa? bet collect yourselves and comeup with something substantial mfano, ndugu zenu wa Zanzibar kule Pemba wamepata janga la kuzama kwa meli, i thought mngechangia hata kidogo, hamna pesa au chochote kweli? you're just swayed by CCM kama wadudu wa mafuriko, yaani fitna tu! Refeer Kikwete aliwaambia fikirieni mambo ya maana jamani! you are brainwashed forever msifikirie tena katika kujenga uchumi hata wa kwenu binafsi ili mbaki wapumbavu na trivial thinkers wakati wengine wanaendelea na kupasua anga!
wajua misemo ya kikulacho ki-nguoni mwako inawahusu kabisa! Fitna hata misikitini kwenu, hawawezi kushirikiana!
 
CCM inacheza sana na akili za waisilamu maana ni rahisi sana kuwanasa. Wao ukitaka kuwateka tumia dini tu hata kama jana uliwatoa ngeo kama ni mwenzao mtapatana. Nadhani pengine ndivyo wananavyo fundishwa(ubinafisi wa kidini mpendelee mwisilami mwenzako)
Cha ajabu ni kwamba hawaamini kwamba CCM kamwe hawataweza kutimiza matakwa ya waisilamu yaliyo kinyume na katiba ya nchi hii hata kama mwenyekiti wake ni mwiisilamu. Atawandanganya tu na mwisho wa siku atawaambia hayo ni mambo yenu fanyeni wenyewe na huo ndo ukweli.

Hakuna Raisi nchi hii hata kama atakuwa shehe,padre au mchungaji atakayekubali kuvunja katiba ya nchi kwa ajili ya kuipendelea dini moja dhidi ya nyingine. Wenzetu waisilamu hawataki kukubaliana na hili wanadhani Raisi akiwa mwisilamu basi anaweza kupendelea uisilamu kitu ambacho hakitakaa kitokee nchi hii!

Kama Raisi wa Tanzania anataka asimalize hata mwezi Ikulu basi apendelee dini yake kwa uwazi aone kama kundi la pili litaogopa na kukaa kimya.

Kama kuna waisilamu wanaona CDM haimtendei haki (japo haijawahi kuwa na mamlaka ya kutenda au kutowatendea haki watanzania) aendelee kubaki ccm kama anaona kwake issue ni dini zaidi kuliko vita vya ufisadi na maisha magumu tuliyonayo watanzania kwa sasa. Hakuna anayemlazimisha mtu kuwaunga mkono chadema ila ni watu wenyewe wameua kutoka mioyoni mwao.

Hatuwadharau wenzetu waisilamu ila Imekuwa too much utafikiri wao ni yule mtoto kitinda mimba ambaye hagusi hata kidogo analia 'mamaaaaaa eti ....... ananishikakichwani'! Ndugu zetu lazima wajiamini waondokane na ile inferiority comprex na kudhani kuwa kuna mtu anawdharau.

Inashangaza sana kwanini kunakuwa na watu wao hujihisi kunyanyaswa tu kila wakati bila hata kuyaona manyanyaso yenyewe.
But nina marafiki zangu tumesoma nao ni waisilamu lakini wanajiamini sana na ni wapenzi wa chadema wa kufa mtu.

ndugu zetu jiaminini kwanza bila hivyo itasumbua sana na hatutakaa tutatue matatizo ya msingi ya nchi yetu. Kumbukeni mtaendelea kutumiwa tu na ccm kama toilet paper wakati wa uchaguzi wakishapata mnabaki palepale labda na nyie muwe mafisadi wakati dini hairusu.

Tuweni kitu kimoja bila kujali dini zetu tumshughulikie adui wa watanzania wote ambaye ni ccm. Hata Kama baadhi yenu mtakataa bado Mungu akisema ndiyo hakuna atakayezuia.

Mungu ibariki Tanzania!
You presented the fact!Just like i was thinking!see my post
 
Mungu ni 'haki' mungu ni 'usawa' na mungu ni 'kweli tupu'. Hivyo nilitegemea BAKWATA kama chombo kinachosimamia maadili ya 'mungu' kupitia dini ya kiislama wangemtaka DC Mama Fatma Kimario kusema 'kweli yote' kuhusu mkutano aliokuwa anafanya mahali/muda kinyume na sheria za vyama vya siasa.

Pia BAKWATA wangefanya vema kujiridhisha kuwa huyo DC hakuna anafanya jambo lolote ambalo directly or indirectly lingenyakua haki ya raia yoyote ya kupata kiongozi wanayemtaka katika uchaguzi mdogo wa Igunga. Hayo ndiyo nilitarajia toka kwa BAKWATA kama kweli wanasimamia maadili mema. Mavazi ni jambo la mbali sana ukilinganisha na HAKI ya mtu kupata kiongozi bora.

Pia ni vizuri BAKWATA watathmini tena upya kwamba wanasimamia nini hasa? Kujiingiza kwenye siasa uchwara ni kukivunjia heshma hiki chombo cha waislam. Kwa wameshamhoji huyu DC na kujua alifuata nini pale?

Na kulikuwa na ulazima gani kwa yeye (DC) kufanya mkutano hapo wakati kuna mkutano wa chama kingine? Huu ni ustarabu? AAu hii inakubalika kwa BAKWATA kwamba mtu anaweza kuvuruga shughuli halali yenye manufaa kwa wengi kwa sababu binafsi?


Tunaambiwa mnapokhitilafiana katika uislamu rejeeni katika Kuran na hadithi. Sijui masheikh wetu kama wamejiridhisha kama anachovaa yule mama ni Hijjabu, mtandio au kilemba?

Tupate kwanza tafsir ya uislamu kuhusu hijjab, tusiingize dini takatifu katika mambo machafu.
 
Mkandara nisaidie kidogo, alosema mwanamke avae hijab ni mtume/mitume au Kur-an?

Kuvulia hijab inaweza kuwa si kudhalilisha uislam lkn ni kumdhalilisha aliyevuliwa, sawa na mwanamke mwengine kuvuliwa blouse au mwanamme kuvuliwa suruwali.

Ikiwa mtandio kwake ni vazi la kila siku basi amedhalilishwa kuvuliwa huko.

Jee vyama vya Kiislam vina haki na wajibu wa kumtetea? Bila ya shaka vina haki hiyo kwa vile aliyedhalilishwa ni Muislam na hiyo ndio kazi yao.

Vyama vya kutetea haki za wanawake pia vingetoa tamko nisingelishangazwa kwa vile wangelikuwa wanatetea haki ya mwanamke mwenzao

Nenda Mombasa na Lamu uone, hivi huyu mwanamke hata kama nguo zingine kavua na kubaki na hijab na kujiuza accordingly bado anaupa heshima uislam dunia nzima?
 
NJAAAAAAAA!!!!!!
Waislamu wenzangu njaa inatupeleka pabaya!!!
Hivi kweli katika dunia ya leo mavazi yanaweza kutumiwa kutafsiri imani ya mtu.
  • Nyerere alikuwa navaa kofia ambayo inavaliwa na watu wa imani ya dini ya kiislamu.Je kwa kuwa alikuwa mkatoliki muumini safi mbona watu hawakulalamika kuwa anainajisi dini yetu?
  • Kinondoni vijana wauza unga wanavaa kanzu na kofia za bei mbaya,mbona hatulalamiki?
  • Mkapa alishavaa kanzu na bagharashia,mbona hatukusikia kuwa dini imekashfiwa?
  • Changudoa wanaondoka nyumbani kwao wakiwa na hijab na ni jambo ambalo lipo wazi.
Waislamu wenzangu njaa inatuumiza na inatupeleka pabaya.Toeni fatwaa kwa mambo ambayo yana msingi sio kupanda train kwa mbele tunaonekana wajinga.
 
Baraza kuu la waislam Tanzania(BAKWATA), na Baraza kuu la Answar suna Tanzania(BASUTA), kwa pamoja wamelaani kitendo cha viongozi wa CDM Kumvua hijabu DC Fatuma kimario wamesema kitendo hicho walichofanya chadema kwa mujibu wa uislam ni kama wamewadhalilisha waislam wote Duniani kwa hiyo amewataka viongozi wa CHADEMA kuwaomba radhi waislamu. Naibu mufti akiwa mjini Tabora alisema Fatuma ana imani yake japo ni DC, heshimuni imani yake kwani waliomchagua wanajua kuwa imani yake inamtaka avae hijab alisema sheikh mohamed issa wa Answar Sunna. CHANZO: Taarifa ya habari Radio Imaan
Bakwata na Basuta mmeliona la hijabu tu, mnasemaje kuhusu redio imaan ya morogoro na vipazia sauti vinavyokashifu wakristo kwa sauti za kupaza? Mnadhani ni nmyie tu ndo mmedhalilishwa? Yametokea na yanaendelea kutokea katika taasisi kubwa ya umma ya elimu ya juu mpya hapa nchini ya mwanachuo kupigwa na kuchomwachomwa vitu na wanachuo waliovaa hijabu hamkukemea ndo kusema nyie moyo wa aina gani ambao wenzenu wanahalali ya kukashifiwa tu?Kemeeni haya ya waumini wenu ama kemeeni mioyo yenu pia kama mnawatuma wafanye haya
 
Kuna baadhi ya habari nimezisikia kwenye uchambuzi wa magazeti redioni asubuhi ya leo, zimenipa mawazo kuwa kuna kazi kubwa na ngumu sana mbele ya safari kama kuna nia ya kweli ya kuleta uhuru wa pili hapa nchini.

Hili tukio lililotokea siku chache zilizopita ambalo liko mahakamani sasa limefanywa kuwa la kidini. ajenda hapa ni kutaka kuwagawanya watu na kuendelea kuwatawala kama alivyofanya mkoloni mzungu yaani ''divide and rule'' ndivyo anavyofanya mkoloni mweusi akishirikiana na waganga njaa ili kulinda maslahi yake. Yaani kazi ni ngumu kweli kweli.
 
Chadema ni adui mkubwa atakae igawa nchi yetu kwa Ukristo na Uislam! Mungu tuepushie mbali balaa hili la Chadema!
 
Hii ni janja ya CCM kutumia wadini ili kuwatishia CHADEMA. Wao ndiyo wanaanza kupandikiza UDINI. Hili ni jambo la kisiasa na halina uhusiano na DINI.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom