baiser

JF-Expert Member
Dec 29, 2014
1,456
2,181
Ndugu wana JF, mwezi wa.12 /2020 nilifiwa na mamangu mzazi.

Leo saa Tisa na dakika kumi usiku (12/5/2021) nimeota ndoto niko na mdogo wangu nashusha mteremko kwa miguu nikitokea mjini Iringa kuja Ipogolo maeneo ya kitanzini tumekutana na mama akiwa kabeba kikapu chake anapandisha mjini yaani anatoka Ipogolo anapandisha iringa mjini kwa wenyeji wa Iinga watanielewa.

Tumeongea naye na tukamwomba MTU tupige nae picha ghafla akaanza kubadilika na kuwa wa blue kupoteza nuru ya sura yake halisi na kuwa kijana, lengo tusipate picha yake halisi.

Baada ya muda akabadilika na kuwa kijana wa kiume miaka kama 15 hivi na tukaanza kushusha nae kuja Ipogolo huku nikimuuliza maswali kuwa anaishije aliko.

Akajibu maisha mazuri aliko, hela kama zote ila tu hawaruhusiwi kuja kununua vitu wenyewe kuchanganyika na binadamu halisi.

Baadaye nilimpa mkate akapokea na kuniomba kopo la maji akatumie kuchota kwenye MTO Ruaha ili anywe, na ghafla nikastuka na ndoto ikaishia hapo.

Je, hii manaake nini? Is she a walking dead?
 
Kwanza pole kwa msiba. Ni psyche yako (akili) iko katika kuchakata ukweli wa msiba uliokupata. Na hii ni namna ya kukusaidia kuipokea na kuishi na huzuni iliyotokana na msiba huo. Ndoto za namna hiyo zaweza kujirudiarudia. lakini hupungua sana kadri mda mrefu unavyopita pale utakapokuwa tayari umeishaipokea hali na kuendelea na maisha kama kawaida.
 
Hujawah kuota na kukurupuka usingizin na kujiuliza hii ni nin? Na kuangalia saa sa ngapi?
Huo unakua ni muda ulioshtuka. Lakini hatujui ndoto imedumu muda gani hivyo hauwezi kutaja dakika uliyoanza kuota isipokua utataja saa.
 
Huo unakua ni muda ulioshtuka. Lakini hatujui ndoto imedumu muda gani hivyo hauwezi kutaja dakika uliyoanza kuota isipokua utataja saa
Ni uandishi wangu tu mbovu ilaa ndo namanisha mda wa kukurupuka.
 
Wakuu habari?

Naomba niende moja kwa moja kwenye mada. Mimi juzi niliota nimeteuliwa kuwa Mbunge wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Nilifurahia sana huo uteuzi. Sasa tatizo ikaja namna ya kufika Bungeni!

Kwanza nilipoondoka boss wangu wa kazini nilipo saiv alinitumia watu nikiwa njiani lakini sikutaka kurudi. Pili njia niliyopita ilikuwa kwanza ni porini halafu njia ni korofi mno na nilikutana na nyoka wawili walitaka kunitishia lakini baadae wakaniacha. Nasikia wabunge wakichangia hoja pembeni kidogo mwa njia yangu nilimkuta aliyekuwa mtangazaji wa BBC marehemu Isack Gamba ila aliponiona alinipisha.

Sasa nimekuja kushtuka usingizini wakati ndio nakaribia kumaliza hilo pori amabapo ningefikia barabara kuu ya lami wakati huo mbele yangu nilimuona binti moja amesimama kando ya barabara ni kama alikuwa ananisubiri ila sikufika pale alipo.


Naomba mnisaidia maana ya hiyo ndoto.
 
Ndoto huwa ni maelezo/taarifa unayopewa na malaika wako kwa njia ya mafumbo.
Kitu unachokiota kwenye ndoto kinaweza kisiwe kinahusika kwenye tafsiri halisi. Ili kutafsiri ndoto inatakiwa uangalie yale matukio yaliyojitokeza, je mwisho wa ndoto ulikuwa mzuri au mbaya?.

Uzuri wako wewe umeota kupata nafasi ya mafanikio ya uteuzi. Njiani umekutana na Mtu na Nyoka ambaye hajakudhuru, kisha ukakaribia kufika sehemu salama.

Tafsiri yake hii ni ndoto nzuri kwako, Pengine unakaribia kuja kupata Mke ila utapitia vikwazo kabla ya kuja kumpata. Au utapanda cheo kazini kwako ila kuna mfanyakazi mwenzako nae alikuwa anataka hicho cheo ila mwisho wa siku wewe ndio utateuliwa. Au kuna changamoto utazipitia kwenye jambo fulani linalokuhusu ila mwisho wake wewe ndio utapata ushindi.
 
Ndoto huwa ni maelezo ya mafumbo.
Kitu unachokiota kwenye ndoto kinaweza kisiwe kinachohusika. Ili kutafsiri ndoto inatakiwa uangalie yale matukio yaliyojitokeza.

Uzuri wako wewe umeota kupata nafasi ya mafanikio ya uteuzi. Njiani umekutana na Mtu na Nyoka ambaye hajakudhuru, kisha ukakaribia kufika sehemu salama.

Tafsiri yake hii ni ndoto nzuri kwako, Pengine unakaribia kuja kupata Mke ila utapitia vikwazo kabla ya kuja kumpata. Au kuna changamoto utazipitia kwenye jambo fulani linalokuhusu ila mwisho wake wewe ndio utapata ushindi.
Asante mkuu! Japo mkuu Mimi nilishampata na sina mategemeo ya kuoa mke wa pili kulingana na Imani yangu.
 
Mwenye ufahamu tafadhari anisaidie maana ya Ndoto hii, Nina bodaboda nafahamiana nae. Sasa Jana nimeota amenibeba tunaenda mahala fulani lakini njia aliyoitumia ni njia yenye mtelemko mkali sana, Katikati ya mtelemko huo nikamsimamisha na akasimama nikamwambia abadilishe njia na akakubali ghafla pikipiki ikazima.

Dakika kadhaa walitokea watu wasiojulikana wakiwa na mapanga, marungu na visu wakanisogelea wakasema toa ulichonacho nikatoa Tsh 50,000 nikawapa lakini walinirudishia 20,000 wakaondoka, Nikashtuka kutoka ndotoni, nusu saa badae niliota Ndoto kama hii lakini ikihusisha jinsia ya kike ninayefahamiana nae ndugu yangu wa karibu jinsia ya kiume yenyewe nilikmbia nikawaacha hao vibaka

Msaada tafadhali.
 
Mkuu hiyo ndoto unaweza kuitafakari na kuitafsiri wewe mwenyewe ukiunganisha na matukio yanayoemdelea katika maisha yako ya kila siku.watu unaofahamiana nao nk.

Hakuna anaweza kukutafsiria ndoto bila kujua uhalisia unaoendelea katika maisha yako ya kila siku.

So tafakari wewe mwenyewe,unganisha dots utapata jibu.
 
Kuwa makini kuna matapeli wanataka kukurudisha nyuma. Tena wanakuja kwa njia ya ushawishi mkubwa hasa kwa kutumia watu wako wa karibu.

Kuwa mwangalifu sana kushtukia mipango yao, maana utatapeliwa kiasi kikubwa cha fedha na utaweza kurudisha kiasi kidogo.
 
Back
Top Bottom