Asante Comrade Kinana, ni kweli Serikali ijenge barabara ya lami njia nane, Dar -Songwe

masopakyindi

Platinum Member
Jul 5, 2011
17,882
13,171
1659170988995.png

Comrade Kinana ndio kiongozi wa kwanza wa ngazi za juu kabisa katika ungozi wa CCM kujionea kero za barabara iliyosuswa na Awamu kadhaa( kuanzia alipochaguliwa Waziri wa Ujenzi-Magufuli, Awamu ya Mkapa) katika ujenzi wa barabara nchini.

Hapa mtandaoni tumelalamika sana , bila mafanikio, ubovu na ufinyu wa barabara hii kuu iendayao Malawi, Zambia na Congo.
Kutokana na tatizo hili, hasa pale Tunduma, malori yana paki lane moja.
Lane ya pili iliyobaki ndio yanapishana magari yote, na lane hiyo haizidi mita tatu na nusu!
(picha inajieleza)
Ni kero...... kero...... kero!!

Comrade Kinana kajionea pale Tunduma, Songwe, foleni ya malori yenye shehena ambayo wakati mwingine inaenda hadi kilometa 15 hadi 20 kurudi nyuma.
Awamu ya hasa mwendazake , iliisusa kabisa mikoa hii ya Nyanda za Juu Kusini kwa hii barabara ya Dar es salaam mpaka Songwe.
Funga kazi ni ubovu wa barabara kuanzia Igawa nadi Songwe.
Barabarahii finyu yenye mashimo na viraka lukuki, inapita katikati ya Jiji la Mbeya na kusababaisha kero na ajali zisizo na kifani.

Tnamshukuru sana Comrade Kinana kwa kuikumbusha Serikali wajibu wake uliotekelezwa kwa mikoa hii ya Nyanda za Juu kusini.
 
Naam, yaani kipande Cha Morogoro Dar, technically kina foleni, gari hazitembei, kipande fulani Cha Biharamulo Ngara takataka kabisa japo kinaingiza mabilioni kwa mamia
 
Kwa muonekano wa hiyo picha na maelezo yako mleta mada, kweli hiyo barabara ni muhimu sana kiuchumi kwa watu wa kanda hiyo, serikali ifungue macho sasa.
 
Mleta uzi ficha upumbafu..kwahiyo hii nchi tangu ipate uhuru raisi na waziri wa ujenzi tangu kipindi hicho ni JPM pekee?

Unasahau pia ccm ndio chama pekee kilichotawala hii nchi.?
Lawama zote zitupie kwa ccm sio jpm..jpm kafanya makubwa sana ambayo hata ccm wenyewe hawaamini kama yangefanyika.

#MaendeleoHayanaChama
 
Kwa muonekano wa hiyo picha na maelezo yako mleta mada, kweli hiyo barabara ni muhimu sana kiuchumi kwa watu wa kanda hiyo, serikali ifungue macho sasa.
Njia nane kutoka dar hadi tunduma ni ndoto, pengine miaka ijayo huko mbeleni. Kwa Sasa haiwezekani
Mradi Kama huo ni zaidi ya trillion 10. Pesa ipo wapi?
Kufikiria vikubwa ni jambo zuri, Ila kwa Sasa uhalisia unakataa. Hii miradi tu tuliyonayo sasa hivi ni mzigo mkubwa ambao hatujui tunaimalizaje
 
Njia nane kutoka dar hadi tunduma ni ndoto, pengine miaka ijayo huko mbeleni. Kwa Sasa haiwezekani
Mradi Kama huo ni zaidi ya trillion 10. Pesa ipo wapi?
Kufikiria vikubwa ni jambo zuri, Ila kwa Sasa uhalisia unakataa. Hii miradi tu tuliyonayo sasa hivi ni mzigo mkubwa ambao hatujui tunaimalizaje
Hawajamaliza hiki wanataka kushika
Kile

Ova
 
Hawajamaliza hiki wanataka kushika
Kile

Ova
Hapo sasa, kuwaza vikubwa ni Jambo zuri ila kuja uzi na kujilisha upepo kuwa tunaenda kujenga ni uongo. Alichofanya Kinana ni kutoa ushauri, yeye mwenyewe anajua mradi wa zaidi ya trillion 10 shughuli yake sio ndogo.
 
Hapo sasa, kuwaza vikubwa ni Jambo zuri ila kuja uzi na kujilisha upepo kuwa tunaenda kujenga ni uongo. Alichofanya Kinana ni kutoa ushauri, yeye mwenyewe anajua mradi wa zaidi ya trillion 10 shughuli yake sio ndogo.
Tatizo kubwa analolionyesha Comrade Kinana ni kuwazindua viongozi kuwa kwa kunyanyapaa Nyanda za Juu Kusini, serikali inajikosesha mapato kijinga.
Ujinga huu uliasisiwa na mwendazake akiwa waziri wa ujenzi.
 
Tatizo kubwa analolionyesha Comrade Kinana ni kuwazindua viongozi kuwa kwa kunyanyapaa Nyanda za Juu Kusini, serikali inajikosesha mapato kijinga.
Ujinga huu uliasisiwa na mwendazake akiwa waziri wa ujenzi.
Hilo sio tatizo bali ni wajibu wake kufanya hivyo..

Kimsingi yeye ndio mwenye chama na ana wajibu wa kuisimamia serikali itekeleze wajibu wake..
 
Back
Top Bottom