Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Arsenal (The Gunners) | Special Thread

Mimi ni shabiki nyumbu ila Arsenal ni timu nzuri sana kwa sasa. Wanaweza kubadili matokeo muda wowote. Kwenye soka kuna matokeo matatu,hivyo mashabiki wenzangu wa soka hasa timu ya Arsenal msiogope sana. Katika kitu sikitaki hata kukiota msimu huu ni City kubeba tena ndoo
 
Mkuu we usichokielewa ni nini?

Shida sio arsenal kufungwa, shida ni maneno ya baadhi ya misukule humu wanatuaminisha arsenal ni timu isiyogusika.

Sasa ikitokea mmebondwa ebana eeh, lazima tujeee.

Piga nyanii izooooo.
Huwez tegemea mashabiki wa timu wote waseme timu yao ni mbovu, wapo mashabiki wa aina mbili mbona wapo pia mashabik wa arsenal wenye mtazamo tofauti na hao unaowasema, kwaiyo maneno ni kawaida kwenye football kutamba na kutambiwa iyo ipo kabisa mzee
 
Msimu huu Arsenal hawako kama msimu uliopita mimi niliona tangu ligiu ianze, ni mashabiki wagumu tu ndio walikuwa wanabisha. Tatizo la Arsenal ni kama la Chelsea hawan wafungaji wazuri na Declan rice hana pivot wake mzuri, defence wako wawili tu Saliba na Gabriel
Kwenye usajili Arteta hakufanya vizuri lakini bado Arteta ni kocha mzuri, wakimtamani mwingine anaweza kuja kuwarudisha walikotoka. Bora sasa hivi wanashiriki michuano mikubwa ya UEFA ili pochi iongezeke na pia wachezaji wakubwa wapende kwenda Arsenal

Wanaosema Arteta ni average coach hamna shukrani, au mmesahau kuwa aliwakuta mavumbini akawaleta kwenye zulia na tiles sasa hampigwi vumbi tena?
EPL mkubali kuna ushindani, hii sio ligi ya wakulima ambapo kila timu ikitaka ubingwa inachukua tu
 
Bukayo saka ana goli 5 tu epl sawasawa na Darwin Nunez ambaye hapewi dakika nyingi. Huyu Star boy wenu ndio mnategemea awape ubingwa kama walishindwa kina Alexis Sanches, ameshindwa RVP aje aweze Saka
Uwakute sasa kina hamis77 na chawa wake wanavyoaminishana ujinga humu, wanadanganyana kabisa kua hakuna RW bora duniani kumzidi Sakatonge.
 
Mimi ni shabiki nyumbu ila Arsenal ni timu nzuri sana kwa sasa. Wanaweza kubadili matokeo muda wowote. Kwenye soka kuna matokeo matatu,hivyo mashabiki wenzangu wa soka hasa timu ya Arsenal msiogope sana. Katika kitu sikitaki hata kukiota msimu huu ni City kubeba tena ndoo
Kabisa kabisa. Mimi huwa nafurahi sana nikiona comment kama hizi. We unawajua vizuri sana hawa kondoo. Ni kuwapa moyo tuu, ukweli hawaumudu. Hap tunalisubiri CHAMBUZI, CHA-MMEE EEEE, CHAGOAT HAMISI lije kutuambia ni jinsi gani jana FC MATUMAIN HEWA wameupiga mwingi
 
Aaaah. Mambo gani tena haya Arteta na Arsenal? Nimelala vizuri nikijua nitaamka na kujikuta nimeketi zangu fresh kileleni nikiwachora kina Livakuku.
Yaani tumeshindwaje kuwapiga hawa hammers? Sitaki hata kujua. Kwa ujinga huu mimi naona tuachane na kutafuta ubingwa, tuwape Livakuku baraka zetu waupambanie wao. Tutumie muda huu kuboresha kikosi, haswa upande wa ushambuliaji. Halafu tufanye moja kati ya haya mawili:
1. Fukuzia mbali kabisa Arteta.
2. Baki na Arteta lakini yeye na timu nzima waanze sessions na wanasaikolojia washughulikie hiyo block inayowafanya washindwe kutimiza vitu simple tu kama kushinda mechi za lazima kabisa, tena dhidi ya wapinzani dhaifu kuliko Arsenal.
Timueni huyo mid table coach mtafute kocha mwenye mentality ubingwa la sivyo kila siku mtakua mnadanyana humu na hizo phase za michongo.
Mkiendelea kubaki na Aterta basi kila siku mtakua mnateta humu.
Msimu huu siioni Arsenal ya kupambania kombe bali naona Asenyo ya kupambania kubaki top 4.
 
Kabisa kabisa. Mimi huwa nafurahi sana nikiona comment kama hizi. We unawajua vizuri sana hawa kondoo. Ni kuwapa moyo tuu, ukweli hawaumudu. Hap tunalisubiri CHAMBUZI, CHA-MMEE EEEE, CHAGOAT HAMISI lije kutuambia ni jinsi gani jana FC MATUMAIN HEWA wameupiga mwingi
Kumbe siku hizi wanaitwa FC MATUMAINI HEWA?
 
Yaani timu yetu ni haiwezi kudeal na pressure.

Mfano ingekua leo tupo nafasi ya kwanza na tuna points ambazo wa chini yetu hawazifikii hata wakishinda mechi zao hii game tungeshinda vizuri tu
LEICESTER wanachukua Ubingwa walijikuta Nafasi ambayo hawakuitegemea, Ukiangalia Mzunguko wa Pili ilikuwa ni suala la Mwalimu zaidi. ARTETA Mwalimu mzuri lakini bado ni Mwanafunzi aliye kazini, Hawezi jua Kupambana na Pressure kwake Binafsi na kwa Wachezaji wake. {Na ana "EGO" kuamini anajua kumbe bado sana}

Game Nyingi kwa sasa Timu zikicheza na Arsenal zimeamua kuiheshimu na zinawadhuru sana kupitia Utumiaji nafasi, Jana unamaliza na Nafasi za Wazi zaidi ya 5 bila Goli halafu unawaza Ubingwa! Haaland ama Salah washatoka hiyo hatua, Ukitaka Ubingwa nenda nao Jino kwa Jino, Kuwa na ST/CF uhakika ambao kuwapata January ni Bahati nasibu. KDB akirudi kwa CITY ni kama Sajili Mpya.

ARSENAL imekuwa inafungwa aina ya Magoli yanafanana sana karibuni, Imekuwa kama Mbinu ya walimu wa Timu nyingine. Mnafungwa sana Mipira ya Kutenga, Kona, Faulo, kitu ambacho Mlikuwa hamna kabisa msimu ulopita!
 
Beki Ben White halafu mnataka ubingwa hivi mpo serious kweli?
Daaah. Arteta katuletea maneno mbofu mbofu mingi sana mjini ndani ya saa chache sana. Yaani mpaka Benny Blanco Master Mwenyewe kuna mtu anajitokeza kumdhihaki?
 
Arsenal wala hamna tatizo kubwa. Mnahitaji a top striker. Basi. Everything else inakua solved.

Hamuwezi kosa 5 BIG CHANCES halafu mkaanza kulia lia we need squad overhaul. Acheni ku over react qummmmamaqe
 
Back
Top Bottom