LEICESTER wanachukua Ubingwa walijikuta Nafasi ambayo hawakuitegemea, Ukiangalia Mzunguko wa Pili ilikuwa ni suala la Mwalimu zaidi. ARTETA Mwalimu mzuri lakini bado ni Mwanafunzi aliye kazini, Hawezi jua Kupambana na Pressure kwake Binafsi na kwa Wachezaji wake. {Na ana "EGO" kuamini anajua kumbe bado sana}
Game Nyingi kwa sasa Timu zikicheza na Arsenal zimeamua kuiheshimu na zinawadhuru sana kupitia Utumiaji nafasi, Jana unamaliza na Nafasi za Wazi zaidi ya 5 bila Goli halafu unawaza Ubingwa! Haaland ama Salah washatoka hiyo hatua, Ukitaka Ubingwa nenda nao Jino kwa Jino, Kuwa na ST/CF uhakika ambao kuwapata January ni Bahati nasibu. KDB akirudi kwa CITY ni kama Sajili Mpya.
ARSENAL imekuwa inafungwa aina ya Magoli yanafanana sana karibuni, Imekuwa kama Mbinu ya walimu wa Timu nyingine. Mnafungwa sana Mipira ya Kutenga, Kona, Faulo, kitu ambacho Mlikuwa hamna kabisa msimu ulopita!