Apson: The Beginning of TISS's Failure

Apson: The Beginning of TISS's Failure

DC na Northern Virginia hakufai kabisa....
Siku hizi pale St Peters wamekata kata miti ata jengo lenyewe linaonekana na kale kabarabara wamekawekea lami unakatiza tuu mbele ya jengo hawana noma sana sema ukisogelea geti ndio unaweza kuwekwa chini ya ulinzi kwa muda.

Anwyays ofisi ya station iko chini ya kitengo cha usalama wa ndani, walikuwa wanakaribisha wananchi wote kwenda pale kutoa mawazo yao..siku hizi wameihamishia kule sea view.

Napakumbuka pale stesheni, geti kubwa na vipikipiki vyao kibao!
 
Nafikiri hata CCM wenyewe hawatapenda kumsimamisha mtu kama Mwandosya maana wanajua kabisa ana kashifa inanukia ya kujilimbikizi mamilioni wakati wa ununuzi wa rada na ndege ya raisi kwahiyo nafikiri mwandosya asahau swala la uraisi. hata kama wasingekuwa na ugomvi na mwakyembe.

Inabidi JF tuanzishe facts check kama wanavyofanya CCN. Kama hapo juu filimbi ingelia maana facts haziko sahihi.
 
Jamani APSON kafanya kufuru alipokuwa mkurugenzi wa Usalama ni tajiri kupita kiasi na bahati mbaya ameweka vijana wengi toka kabila la watu wa Mbeya kwenye usalama wa Taifa hii ni hatari sana kwa Taifa.

1. Mkuu Nungwi, kuna mengi uko sawa isipokuwa hili la ukabila, watu wa Mbeya huko ndani wako wengi siku nyingi sana, toka enzi za Mwalimu, hata Chief Bodyguard wake Mwangota, Daktari wake wa binafsi Mwakyusa, kina Simbeye, na wengine wengi wa nafasi za chini walikuwa ni kutoka mkoa huo, sababu ni kwamba wanaaminika sana kwa royality, Mkurugenzi mstaafu aliwakuta huko tayari, kumbuka huwa wanakuwa recruited toka wakiwa shule na sehemu mbali mbali za taifa, hawachukuliwi tu wakiwa watu wazima, kwenye hili uko mbali na ukweli, lakini mengi uliyosema uko karibu sana na ukweli.

2. Mkuu Mtanzania, strong analysis na as far as the main topic is concerned, kwa kweli inatisha sana mimi ninasema kwamba ukimkamata Mkapa, utakuwa umeua ufisadi completely kwa sababu huu ufisadi ambao ni extreme, umeanzia kwake, hawa wengine walikuwa wanachukua mgawo tu, ndio maana nimesema huko nyuma kuwa kama Chenge, ana hela zote alizonazo, na alikuwa Mwanasheria Mkuu tu, sasa vipi waliokuwa na mawaziri enzi zile na hawa kina mstaafu wa idara? Maana dataz zinaonyesha kuwa Chenge, alipata hela hizo akiwa sheria, chini ya Mkapa, kina Kigoda, wanaendesha magari ya Range Rover za dola elfu sabini je wamepata wapi hizo hela? Hivi kweli kipindi chote cha uwaziri wa Kigoda, alilipwa mshara wa kuweza kununua hilo gari analoendesha sasa?

3. Mstaafu wa idara ni kweli ana mali nyingi sana, alizo ilimbikiza kipindi cha Mkapa, na ni kweli kwenye ule uchaguzi alicheza a double play game, na alifanya vile only kum-please Mkapa, lakini in the process akaishia kujiweka sawa na muungwana na hata kumrishisha mkulu wa sasa, kwa sababu sio siri kuwa ni yeye single handed aliyeamua na according to the dataz ni kwamba alikuwa amemtayarisha kwa siri, lakini kwa muda mrefu sana bila watu wa huko ndani kujua, maana namjua mkulu mmoja aliyedhani kuwa yuko karibu naye na kwamba atamrithisha, time ilipofika aka-wa-suprise mpaka ma-senior huko ndani, you wonder in all this ni kwa ajili ya interest ya wananchi au ya nani?

Wa-Tanzania, ni lazima tuendelee kupiga kelele kwa sababu tunajua kuwa tumetoka mbali sana politically, binafsi napenda kutoa heshima kwa serikali ya sasa kwa kutoa nafasi kwa wananchi kutoa maoni yetu kuhusiana na kila sekta ya serikali yetu, bila vipingamizi never before wa-Tanzania tumekuwa na hii nafasi ya uwazi bila kunyanyaswa, ingawa bado hii tabia haijawaingia vizuri huko serikalini na watawala wetu kwa ujumla, lakini ninaaamini kwamba mijadala kama hii na ya ufisadi wa kina Chenge, ni changamoto nzito sana kwetu wananchi kuwashupalia viongozi wetu wasiotaka kuwa kama sisi wananchi, yaaani wawazi na ninarudia kwamba ili kumaliza mzizi wa fitina na ishu ya uifisadi, ni lazima in one way or another Mkapa, ahusishwe na uchunguzi wa kina otherwsie tutakuwa tunacheza na mikia tu, huku kichwa kinaendelea kutuumiza!

Ahsante Wakuu!
 
FMES,

Umenikumbusha ya brother Mwangota RIP, Looh, jamaa alikuwa akiingia, wote mnatawanyika haraka sana, mnajua hapo hakuna amani tena.

Siku nimemkuta Muhimbili kule juu, yuko taabani, utafikiri sio yeye.

Hii dunia, tutende mema maana wote ni wasafiri tu na hakuna mjanja kwenye kifo.
 
Hivi ni kweli mkulu alinguka na ngoma, maana siku hizi najua mama watoto anajirusha na yule mzaire Asosa, au?

Halafu unakumbuka jinsi alivyokuwa akiwatandika vibao mabalozi na wakuu wote walio magoi goi mbele ya Mwalimu?

Yule mkulu alikuwa kiboko, mungu amlaze mahali pema!
!
 
FMES kuna dots kadhaa zinajiunga hapa....

Sasa na ile supposedly beef iliyokuwepo kati ya Apson na JK ilikuwa imepikwa?
 
FMES,

Umenikumbusha ya brother Mwangota RIP, Looh, jamaa alikuwa akiingia, wote mnatawanyika haraka sana, mnajua hapo hakuna amani tena.

Siku nimemkuta Muhimbili kule juu, yuko taabani, utafikiri sio yeye.

Hii dunia, tutende mema maana wote ni wasafiri tu na hakuna mjanja kwenye kifo.

Yeah...kifo...the greatest equalizer of all times, bar none!
 
Sasa na ile supposedly beef iliyokuwepo kati ya Apson na JK ilikuwa imepikwa?

Mkuu ninavyofahamu ni kwamba mwanzoni walikuwa na beef kweli, kwa sababu kuna ile njama ya kina Diria, ya kumhamisha mstaafu kwenda China, ili asishike nafasi ya Kombe ilikuwa ni njama ambayo mstaafu aliamini kuwa huenda muungwana, alihusika,
lakini ikaja kuwa mbaya zaidi kwenye mafaili ya maadili ya wagombea urais ambapo faili la muungwana, lilikuwa chafu sana na yeye aliamini kuwa mstaafu amehusika na kulichafua, kwa hiyo wakawa hawaongei kabisaa, lakini ilikuwa ni kwenye ule mchakato na deal kupikwa, Mkapa aliwatema wote kina Mangula, Ngwilizi, Masilingi, Idd Simba, Ngasongwa, lakini alim-include huyu mstaafu kwenye package, the first thing baada tu ya uchaguzi mtoto wa mstaafu Tom, alipewa offer ya uwaziri mdogo na mtandao, ikabidi mkulu mmoja wa CCM akaingilia kati na kuua hiyo offer, badala yake ikaishia ubunge wa bure na mwakipesile kupewa u-RC, na mstaafu kuchagua mrithi wake!
 
...swali zuri sana! nadhani umeshamjua aliye mawazoni mwangu kama culprit wa hii chaos....ni yeye aliyeanza ku-politicize hii taasisi na ndio maana tupo hapa tulipo!! kwani kulikuwa na precedency na legacy iliyokuwa set na kuachwa na bwa'kubwa al marhumu jinsi ya kuendesha kitego hiki!!.

utasema oooh, kafa miaka mia ilopita...well, issue ni alitumiaji ofisi kwa faida yake ndio maana hawa wa sasa hawaoni sababu ya kufanya vinginevyo!!!

familia ni misingi bwana, kama ni mibovu, usitegemee miujiza.........

Unajua wewe saa ingine uko ka' Dick Morris....ishu iko wazi lakini wewe unamshambulia Nyerere...Dick Morris naye akiulizwa swali kuhusu Obama badala kujibu swali anaanza kumshambulia Clinton....
 
Mkuu ninavyofahamu ni kwamba mwanzoni walikuwa na beef kweli, kwa sababu kuna ile njama ya kina Diria, ya kumhamisha mstaafu kwenda China, ili asishike nafasi ya Kombe ilikuwa ni njama ambayo mstaafu aliamini kuwa huenda muungwana, alihusika,
lakini ikaja kuwa mbaya zaidi kwenye mafaili ya maadili ya wagombea urais ambapo faili la muungwana, lilikuwa chafu sana na yeye aliamini kuwa mstaafu amehusika na kulichafua, kwa hiyo wakawa hawaongei kabisaa, lakini ilikuwa ni kwenye ule mchakato na deal kupikwa, Mkapa aliwatema wote kina Mangula, Ngwilizi, Masilingi, Idd Simba, Ngasongwa, lakini alim-include huyu mstaafu kwenye package, the first thing baada tu ya uchaguzi mtoto wa mstaafu Tom, alipewa offer ya uwaziri mdogo na mtandao, ikabidi mkulu mmoja wa CCM akaingilia kati na kuua hiyo offer, badala yake ikaishia ubunge wa bure na mwakipesile kupewa u-RC, na mstaafu kuchagua mrithi wake!

Ahsante kwa maelezo mkuu!!

Kuna kazi ya kuuondoa ufisadi ila taratibu tutafika.... puzzles zinajiunga taratibu zenyewe.
 
...swali zuri sana! nadhani umeshamjua aliye mawazoni mwangu kama culprit wa hii chaos....ni yeye aliyeanza ku-politicize hii taasisi na ndio maana tupo hapa tulipo!! kwani kulikuwa na precedency na legacy iliyokuwa set na kuachwa na bwa'kubwa al marhumu jinsi ya kuendesha kitego hiki!!.

utasema oooh, kafa miaka mia ilopita...well, issue ni alitumiaji ofisi kwa faida yake ndio maana hawa wa sasa hawaoni sababu ya kufanya vinginevyo!!!

familia ni misingi bwana, kama ni mibovu, usitegemee miujiza.........

Mkuu sheria ya sasa ya TISS nadhani imepewa nguvu sana na kuanza kazi rasmi huku ikitambulika wakati wa mkapa!

Just a hint with a light touch!
 
....tupo anga mbili tofauti dada langu, mie naongelea matumizi ya taasisi yaani ilivyokuwa politicized toka enzi hizo!! wewe unaongelea sheria.....kwanza ni kiongozi gani anaejali sheria ktk tanzania?? siasa v/s sheria......assume kwamba, wewe ni mimi, think hard labda utaona point yangu!!!

goodnight and goodluck.


Wewe unajuaje ilikuwa polticized toka enzi hizo? Ulikuwepo? Toa ushahidi wa politicization unayodai na si majungu....
 
Hivi kuna mtu humu anaamini Apson atafanya la maana pale ili twende mbele? the guy has been there forever na mawazo yake ya old Soviet union,mambo mengine ni kujitakia tuu kuwapa kazi watu kama hawa.
 
......ubishi wa dizaini hiyo nimeshaachana nao zamani sana!! mie nilikuwa natoa mawazo yangu, kama hutaki basi....

No, umetoa madai...nimeomba utoe ushahidi unaothibitisha madai hayo umeshindwa na sasa unaleta visingizo vya "ubishi wa dizaini hiyo nimeshaachana nao zamani sana"....kama ni hivyo basi hata utoaji wa madai ambayo huwezi kuthibisha nakusihi uachane nao mara moja...
 
kuna haja ya kupitia mafile ya cabinet officers wote wa wakati wa mkapa pamoja na wakurugenzi wa mashirika ya umma kwa sababu ufisadi wa aina ya juu ulianza katika kipindi cha Mkapa.
 
Nafikiri hata CCM wenyewe hawatapenda kumsimamisha mtu kama Mwandosya maana wanajua kabisa ana kashifa inanukia ya kujilimbikizi mamilioni wakati wa ununuzi wa rada na ndege ya raisi kwahiyo nafikiri mwandosya asahau swala la uraisi. hata kama wasingekuwa na ugomvi na mwakyembe.

Aa wapi, hata wajaribu vipi kila mtu anajua swala la rada dili lilikuwa limeshapigwa kabla mwandosya hajawa waziri, hata ubunge...(angalia hansard za bunge na speech zake - dili lilianza kusainiwa 1997 na hela by 1998 ishaanza kuvuja hazina kwa ajili ya ununuzi). Kama una data weka humu...
watachokonoa kila sehemu lakini wapi...(paper trail ipo)ndo maana Mwandosya bado wanajaribu kumsumbua kila saa.
 
tatizo wewe dunia yako imeanza, inazunguka na inaishia na huyo marehemu. Leo hii inflation imepanda kufikia 9 percent tatizo Nyerere; wamekomba Benki Kuu, tatizo Nyerere; wameuziana Kiwira, tatizo Nyerere; Dito kamlipua mtu, tatizo Nyerere; yaani wewe huyo Nyerere alikuwa na uungu gani wa kuweza kubeba mizigo yote hiyo. Mwisho utasema hata talaka zinavyozidi na kuongezeka kwa ukwimi vilianza na Nyerere kwa sababu vilianza wakati wa Nyerere.

Sasa kwa vile wewe kila kitu kinaanzia kwa Nyerere basi tusaidie tufanye nini ili aje atubadilishie nchi na kuibadilisha taasisi hii?
 
Kwa mujibu wa watu wengi niliozungumza nao ndani na nje ya idara wanasema wakati wa awamu ya kwanza kulikuwa na ufanisi sana ukizingatia wakati ule tulikuwa tunawindwa na makaburu as well as CIA they had to be on their best form.
 
Icadon, huyu kijana anafikiri tuliweza kuhost nchi kadhaa wakati wa harakati za ukombozi na usalama wa Taifa kama huu wa sasa. hivi anajua ni mara ngapi makaburu wamejaribu kuinfiltrate Tanzania na wakashindwa. Enzi hakuna cha mzungu wala mjomba ake mzungu aliyepigiwa magoti.
 
Back
Top Bottom