Angola walitangaza zabuni na DP World ikashinda na sasa yasimamia kitengo cha makontena bandari ya Luanda

Richard

JF-Expert Member
Oct 23, 2006
14,939
20,400
1688749850957.png


Naam, ni DP World Luanda Port.

Bandari ya Luanda ni moja ya bandari kubwa nchini Angola kati ya bandari zake zikiwemo za Lobito na Benguela ambazo zipo pembezoni mwa bahari ya Atlantic.

Lakini serikali ya Angola kwa kuona ufanisi mdogo uso na tija kwa uchumi wake ikaamua kutafuta mzabuni ambae ataendesha shughuli za khasa makontena katika bandari ya Luanda ili kuleta tija zaidi na manufaa makubwa ya kiuchumi. Ikaunda kamisheni ambayo itasimamia utekelezaji wa mpango wa kubinafsisha shughuli za bandari na pia kusimamia shughuli zinofanywa na mzabuni DP World kwenye kitengo cha makontena.

Lakini serikali hiyo imeweka masharti yake kwa mzabuni yoyote atakaeshinda na moja ya masharti hayo ni mzabuni kuendesha shughuli zake za usimamizi wa shughuli za makontena kwa miaka 20. Ikifika miaka 20 kama kuna uwezekano wa kuendelea na mkataba basi mkataba utapitiwa upya na mzabuni atapitishwa kuendesha shughuli zake bandarini hapo kwa miaka mingine.

Hatua hii ni sawa na ile ya kubinafsisha bandari ya Lobito kwa wawezekezaji wa ndani na nje kitendo kinoitwa "concession" na benki iitwayo Eagle Stone ya uwezekezaji pamoja na Benki ya Dunia ndo wamekuwa washauri wakuu wa namna ya kurekebisha uchumi wa Angola kwa kuanza na bandari kama hii ya Lobito na ile ya Luanda.

Nifafanue kidogo kuhusu neno "Concession" yaani makubaliano kwamba kwa mfano weye una duka kubwa la bidhaa mbalimbali yaani "departmental store" lakini wakaribisha wauzaji wengine wenye aina zingine za bidhaa tofauti zenye nembo mbalimbali ndani ya duka lako. Wauzaji hawa wengine ambao si waajiriwa wako wao hupanga tu ndani ya duka lako na weye waruhusu wao kujenga duka lao watakavyo ndani humo na kuuza bidhaa zao humo, kuajiri watu wawatakao na pia kufanya mambo yao wanavyoona wao kwa makubaliano ya kukulipa kamisheni inotokana na faida ya mauzo ya bidhaa zao.

Hivyo hapo serikali ya Angola bado ni mmiliki wa bandari zote za Angola lakini imeachia baadhi ya shughuli khasa za kuhusu usimamizi wa makontena ziendeshwe na wabia na makampuni binafsi hususan katika bandari yake ya Luanda ni kampuni ya DP World imeshinda zabuni na sasa ndo yaendesha bandari ya Luanda.

DP World sasa wasimamia kitengo cha makontena cha MPT (multi purpose terminal) na walianza kazi rasmi tarehe 1 March 2021. Bwana Franscisco Pinzon raia wa Panama ndie alieteuliwa na DP world kuongoza MPT akiwa na uzoefu wa miaka 20 katika shughuli za uendeshaji wa bandari na uongozi wake.

Akitoa taarifa ya shughuli za DP world kuanza kazi katika kitengo cha makontena bandarini hapo, afisa mtendaji mkuu na mkurugenzi mwendeshaji bwana Suhail Al Banna amesema DP world wana furaha kuwa nchini Angola na kuendeleza kitengo cha makontena bandarini hapo ili kusaidia kukuza uchumi wa Angola.

Hapa ningependa zaidi msaada wa wanasheria katika kufafanua maana ya maneno yafuatayo: Memorandum of understanding, contract, agreement in principal na agreement. Kisha tufananishe au kulinganisha maneno haya na hili neno "Concession", kwa maana kwamba DP World wamekubaliana na serikali ya Angola kupata uwezo kuendesha shughuli za makontena katika bandari ya Luanda na pia kukifanya kitengo hicho kiwe kitovu cha biashara katika ukanda wa kusini magharibi mwa Afrika.

DP World starts operations of multipurpose terminal at Port of Luanda​


Luanda, Angola,
01
March
2021


 Suhail Al Banna, CEO and Managing Director of DP World Middle East and Africa

We are proud to be in Angola to further develop the terminal as a trade hub in the southern west Africa region, which will support the country’s economic growth objectives by attracting further investment and increased trade.
Suhail Al Banna, CEO and Managing Director of DP World Middle East and Africa.

Serikali ya Angola iliweka ushindani huo wa wazabuni na makampuni kadhaa ya kimataifa yakiwemo kama vile kampuni za Multipaques, Advanced Maritime Transport na China Harbour Engineering Company zilishiriki kupigania zabuni hiyo. Tume maalum ya kutathmini wagombea wa zabuni ambayo iliundwa rasmi na wizara ya masuala ya usafirishaji katika mpango wake uitwao Master Plan, ilikuja na uamuzi kwamba DP World ndo wenye sifa zinofaa na wapewe zabuni.

Sio siri, DP World ni kampuni kubwa yenye uwezo mkubwa na uzoefu wa kazi za kushughulikia makontena yapatayo milioni 70 kwa mwaka. Pia DP World inaweza kulipa kwa mwangalizi (Serikali ya Angola) kiasi cha dola milioni 440 kwa mwaka huku dolali zingine milioni 150 zikilipwa wakati wa utiaji saini na kabla kazi haijaanza!, yaani kwa lugha ingine "Kifunga Uchumba!"

Kwahiyo tumejifunza nini hapo?

Kwanza, tumejifunza kwamba serikali ya Angola bado ni mmiliki wa bandari zote za Angola na imeingia makubaliano na kampuni ya DP World kuendesha shughuli za makontena tu na si vinginevyo katika bandari ya Luanda.

Pili, serikali ya Angola iliweka ushindanishi wa zabuni kwa makampuni mbalimbali yakiwemo ya kimataifa yalotaka kufanya kazi katika bandari ya Luanda. Zabuni hiyo ilitangazwa mwezi December 2019 na DP world ikaja tangazwa kuwa imeshinda zabuni hiyo mapema mwaka 2020. Jambo hilo laonyesha wazi kwamba serikali iliweka jambo hilo wazi na kujulikana wazi kwamba si siri.

Tatu, Serikali ya Angola kupitia wizara ya usafirishaji iliunda tume maalum ya kutathmini zoezi zima la kutafuta wazabuni na kuweka ushindanishi. Hilo pia linalinda heshima kwa serikali (integrity) na imani kwa wnaanchi wake na pia kuonyesha kwamba serikali yajali raia wake na imeweka mbele maslahi ya nchi zikiwemo mali za taifa.

Tumeambiwa kwamba mazungumzo ya mkataba huu yalianza tangia mwaka 2019 hivyo kuwa sawa kabisa na wenzetu wa Angola katika mahckato mzima, je ni wapi tulikwama katika kuhakikisha kunakuwepo ushindanishi wa kupata mzabuni? Au je, kuna tume yoyote iloundwa chini ya wizara ya biashara na viwanda au wizara ya ujenzi au usafirishaji ilohakikisha kuwa kuna uwazi /openness) katika hili na kutathmini mchakato mzima wa kumpata mzabuni?

Je, hili suala ni la kulipeleka Bungeni kwa kuidhinisha tu (rubber stamp) bila kuzingatia maoni ya wananchi au uwepo wa tume hiyo ambayo ingekuwa ikifanya kazi yake kwa niaba wananchi na maslahi ya taifa kwa ujumla?

Je, ni kwanini tumechukua hatua tulizochukua ambazo ni tofauti na hatua ambazo wenzetu na waafrika wenzetu serikali ya Angola imechukua? Je kwanini tusiombe ushauri wa ndugu zetu Angola kwenye hili ili tupate mawazo mazuri ya namna ya kumpata mzabuni hata kama ni DP World kwa kutumia njia sahihi?

Naomba nimalizie kwa kusema yafuatayo:

Hii nchi ni yetu sote na kila maamuzi ambayo serikali yachukua yawahusu watanzania wote na kizazi kijacho, hivyo serikali inawajibika kwa hatua zozote zinohusu maslahi ya taifa hili.

Pia serikali isidharau kauli, ushauri na mijadala mbalimbali kuhusu jambo hili kwani ni fukuto kubwa sana ndani ya mioyo ya watanzania ambao wanazo video zote zinohusu suala la bandari tangia mchakato wake uanze.

Na mwisho, serikali isitishe kuwatumia baadhi ya watu inaoamini kuwa wana ushawishi (influence) kwa jamii hivyo kuweza kusawazisha mambo na kuyapitisha malengo yake yenye kasoro nyingi. Watu hawa ni kweli wana nguvu kubwa ya ushawishi iwe kwenye mitandao ya kijamii, vituo vya redio au televisheni, lakini baadhi yao wamekosa weledi, uwezo wa kufikiri kwa kina na ni waendekezaji mizaha.

Suala linohusu maslahi ya taifa halihitaji mizaha.

Vyanzo vilivyochangia mada hii: Trifigura, DP World Luanda Port, Maritime Institute na vyombo kadhaa vya habari.
 
Tungefuata utaratibu wa manunuzi sidhani kama kungekuwa na malalamiko.

Hata tungefanya kwa single source na kuwapa DPW pia kusingekuwa na tatizo lolote.

Watu hawaichukii DPW au uwekezaji, watu wanachukia ujinga wa viongozi wetu kuingia mikataba ya kipumbavu kila mara.
 
Walipewa mkataba wenye vipengele kama hivi vya kwetu?

Hoja kuu zinazohitaji majibu ni hizi hapa

1.) Tofauti ya ‘Makubaliano’ na ‘Mkataba’ ni ipi hasa kiasi mseme ule sio mkataba, kwamba ni makubaliano tu ya awali, na je Mkataba huo (makubaliano hayo) ni wa miaka mingapi? (UKOMO)

2.) Ni kwa faida ya nani kwamba DPW anapewa haki ya bandari zote za Tanganyika, kwamba hakuna mwekezaji mwingine yeyote anaweza kuja kufanya uwekezaji kwenye bandari za Tanganyika bila udalali wa DPW, je, ukiritimba huu ni kwa faida ya nani?

3.) Ni kwa faida ya nani, DPW apewe haki ya kudai kipande chochote cha ardhi yenye ukubwa wowote anaoutaka yeye ndani ya ‘Territory’ ya Tanganyika na sisi tumpe ardhi hiyo kwa kuondoa watu na miradi yote ndani ya eneo alilolitaka, na tumpatie bire kabisa kwa gharama zetu sisi, hata fidia tulipe sisi ili kuondoa watu kumpisha, huu uwendawazimu ni kwa faida ya nani?

4.) Ni kwa faida ya nani, kwamba sisi tuliowekeza matrillion ya mikopo kuendeleza bandari na tukiwa kama wamiliki wa rasimali ya bandari, tupate 0% ya faida itakayotokana na uendeshaji wa huduma za kibandari, yaani ni kana kwamba yeye kawekeza 100% na hivyo achukue 100%? Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

5.) Ni kwa faida ya nani, kwamba mkataba unahusisha bandari za Tanganyika tu na sio za Zanzibar, ilihali bandari ni suala la Muungano? Je, Zanzibar haitaki kunufaika au yenyewe haitaki matunda ya mkataba huu? Ukizingatia walioongia huu mkataba wote ni waZanzibari, kuanzia Samiah Suluhu Hassan, Makame Mbarawah, Hamza Johari na wenzao, kwamba hawataki Zanzibar yao ipate matunda mazuri ya mkataba huu?!

6.) Ni kwa faida ya nani kusema kwamba, hata DPW akavunja mkataba na kukiuka kanuni na taratibu zote zinazotambulika kimataifa, bado hatutaweza kuvunja , kuusema vibaya au kujitoa kwenye mkataba, milele! Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

7.) Ni kwa faida ya nani kwamba pamoja na kuwa DPW watachukua 100% ya faida, bado tena faida hiyo watapewa Msamaha wa kodi kwa 100%, yaani hata hicho wanachovuna nacho hatuchukui kodi, na wakti huo huo tunakamuliwa kodi za miamala, uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?
 
Hata ukisoma miongozo ya benki ya dunia, checklist on protection of foreign direct investment, moja ya kigezo muhimu ni kuweka wazi mfumo wa tenda. Uendelezaji wa miondombinu mikubwa kama viwanja vya ndege, reli na bandari inahitaji mfumo wa tenda uwe na uwazi.

Jingine kubwa zaidi, mikataba au concessions ni lazima visema kuhusu a method of financing and duration of project. Kama umetumika mfumo wa BOT (Build, Operate, Transfer) au BOO (Build, Operate, Own) au BOOT (Build, Operate, Own, Transfer) inabidi iwekwe dhahiri ili tufahamu lini muwekezaji atamaliza miradi yake.
 
Walipewa mkataba wenye vipengele kama hivi vya kwetu?

Hoja kuu zinazohitaji majibu ni hizi hapa

1.) Tofauti ya ‘Makubaliano’ na ‘Mkataba’ ni ipi hasa kiasi mseme ule sio mkataba, kwamba ni makubaliano tu ya awali, na je Mkataba huo (makubaliano hayo) ni wa miaka mingapi? (UKOMO)

2.) Ni kwa faida ya nani kwamba DPW anapewa haki ya bandari zote za Tanganyika, kwamba hakuna mwekezaji mwingine yeyote anaweza kuja kufanya uwekezaji kwenye bandari za Tanganyika bila udalali wa DPW, je, ukiritimba huu ni kwa faida ya nani?

3.) Ni kwa faida ya nani, DPW apewe haki ya kudai kipande chochote cha ardhi yenye ukubwa wowote anaoutaka yeye ndani ya ‘Territory’ ya Tanganyika na sisi tumpe ardhi hiyo kwa kuondoa watu na miradi yote ndani ya eneo alilolitaka, na tumpatie bire kabisa kwa gharama zetu sisi, hata fidia tulipe sisi ili kuondoa watu kumpisha, huu uwendawazimu ni kwa faida ya nani?

4.) Ni kwa faida ya nani, kwamba sisi tuliowekeza matrillion ya mikopo kuendeleza bandari na tukiwa kama wamiliki wa rasimali ya bandari, tupate 0% ya faida itakayotokana na uendeshaji wa huduma za kibandari, yaani ni kana kwamba yeye kawekeza 100% na hivyo achukue 100%? Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

5.) Ni kwa faida ya nani, kwamba mkataba unahusisha bandari za Tanganyika tu na sio za Zanzibar, ilihali bandari ni suala la Muungano? Je, Zanzibar haitaki kunufaika au yenyewe haitaki matunda ya mkataba huu? Ukizingatia walioongia huu mkataba wote ni waZanzibari, kuanzia Samiah Suluhu Hassan, Makame Mbarawah, Hamza Johari na wenzao, kwamba hawataki Zanzibar yao ipate matunda mazuri ya mkataba huu?!

6.) Ni kwa faida ya nani kusema kwamba, hata DPW akavunja mkataba na kukiuka kanuni na taratibu zote zinazotambulika kimataifa, bado hatutaweza kuvunja , kuusema vibaya au kujitoa kwenye mkataba, milele! Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

7.) Ni kwa faida ya nani kwamba pamoja na kuwa DPW watachukua 100% ya faida, bado tena faida hiyo watapewa Msamaha wa kodi kwa 100%, yaani hata hicho wanachovuna nacho hatuchukui kodi, na wakti huo huo tunakamuliwa kodi za miamala, uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?
Good.
 
Kwenye Andiko lako neno Rwanda imeonekana, sijui ukimaanisha Rwanda au Angola?

Kwa viongozi wetu, wameshawahi kuona sehemu yeyote duniani waliofanikiwa kwa kuendesha mambo ya michakato ya uwekezaji kwa Usiri? Je wanajua kweli namna bora ya kuinua uwajibikaji na kutia wananchi wake Hari ya kuwajibika kwa ajili ya nchi yao?

Yaani mimi nifanyekazi kwa bidii bila kufisadi Mali ya UMMA wakati natambua kabisa kuwa kuna mkataba Serikali iliingia kwa SIRI na haina faida kwa nchi? Nitakuwa kichaa.
 
Je mkataba wa Dp na Angola ni wa milele??
Hapana ni miaka 20 na kisha wataketi tena kuzungumza na kujadili mkataba mpya.

Cha msingi na muhimu ni kwamba Bandari za Angola bado ziko chini ya serikali hivyo ni mali yao lazima waitunze.
 
Kwenye Andiko lako neno Rwanda imeonekana, sijui ukimaanisha Rwanda au Angola?

Kwa viongozi wetu, wameshawahi kuona sehemu yeyote duniani waliofanikiwa kwa kuendesha mambo ya michakato ya uwekezaji kwa Usiri? Je wanajua kweli namna bora ya kuinua uwajibikaji na kutia wananchi wake Hari ya kuwajibika kwa ajili ya nchi yao?

Yaani mimi nifanyekazi kwa bidii bila kufisadi Mali ya UMMA wakati natambua kabisa kuwa kuna mkataba Serikali iliingia kwa SIRI na haina faida kwa nchi? Nitakuwa kichaa.
Mkuu, nilimaanisha Angola.

Nilikuwa nafananisha na Rwanda kwa nchi ambazo zimepitia vita na kuanza kazi ya kuinua uchumi wao.

Nimerekebisha hiyo, twende kazi.
 
View attachment 2681266

Naam, ni DP World Luanda Port.

Bandari ya Luanda ni moja ya bandari kubwa nchini Angola kati ya bandari zake zikiwemo za Lobito na Benguela ambazo zipo pembezoni mwa bahari ya Atlantic.

Lakini serikali ya Angola kwa kuona ufanisi mdogo uso na tija kwa uchumi wake ikaamua kutafuta mzabuni ambae ataendesha shughuli za khasa makontena katika bandari ya Luanda ili kuleta tija zaidi na manufaa makubwa ya kiuchumi. Ikaunda kamisheni ambayo itasimamia utekelezaji wa mpango wa kubinafsisha shughuli za bandari na pia kusimamia shughuli zinofanywa na mzabuni DP World kwenye kitengo cha makontena.

Lakini serikali hiyo imeweka masharti yake kwa mzabuni yoyote atakaeshinda na moja ya masharti hayo ni mzabuni kuendesha shughuli zake za usimamizi wa shughuli za makontena kwa miaka 40. Ikifika miaka 40 kama kuna uwezekano wa kuendelea na mkataba basi mkataba utapitiwa upya na mzabuni atapitishwa kuendesha shughuli zake bandarini hapo kwa miaka 50 mingine.

Hatua hii ni sawa na ile ya kubinafsisha bandari ya Lobito kwa wawezekezaji wa ndani na nje kitendo kinoitwa "concession" na benki iitwayo Eagle Stone ya uwezekezaji pamoja na Benki ya Dunia ndo wamekuwa washauri wakuu wa namna ya kurekebisha uchumi wa Angola kwa kuanza na bandari kama hii ya Lobito na ile ya Luanda.

Nifafanue kidogo kuhusu neno "Concession" yaani makubaliano kwamba kwa mfano weye una duka kubwa la bidhaa mbalimbali yaani "departmental store" lakini wakaribisha wauzaji wengine wenye aina zingine za bidhaa tofauti zenye nembo mbalimbali ndani ya duka lako. Wauzaji hawa wengine ambao si waajiriwa wako wao hupanga tu ndani ya duka lako na weye waruhusu wao kujenga duka lao watakavyo ndani humo na kuuza bidhaa zao humo, kuajiri watu wawatakao na pia kufanya mambo yao wanavyoona wao kwa makubaliano ya kukulipa kamisheni inotokana na faida ya mauzo ya bidhaa zao.

Hivyo hapo serikali ya Angola bado ni mmiliki wa bandari zote za Angola lakini imeachia baadhi ya shughuli khasa za kuhusu usimamizi wa makontena ziendeshwe na wabia na makampuni binafsi hususan katika bandari yake ya Luanda ni kampuni ya DP World imeshinda zabuni na sasa ndo yaendesha bandari ya Luanda.

DP World sasa wasimamia kitengo cha makontena cha MPT (multi purpose terminal) na walianza kazi rasmi tarehe 1 March 2021. Bwana Franscisco Pinzon raia wa Panama ndie alieteuliwa na DP world kuongoza MPT akiwa na uzoefu wa miaka 20 katika shughuli za uendeshaji wa bandari na uongozi wake.

Akitoa taarifa ya shughuli za DP world kuanza kazi katika kitengo cha makontena bandarini hapo, afisa mtendaji mkuu na mkurugenzi mwendeshaji bwana Suhail Al Banna amesema DP world wana furaha kuwa nchini Angola na kuendeleza kitengo cha makontena bandarini hapo ili kusaidia kukuza uchumi wa Angola.

Hapa ningependa zaidi msaada wa wanasheria katika kufafanua maana ya maneno yafuatayo: Memorandum of understanding, contract, agreement in principal na agreement. Kisha tufananishe au kulinganisha maneno haya na hili neno "Concession", kwa maana kwamba DP World wamekubaliana na serikali ya Angola kupata uwezo kuendesha shughuli za makontena katika bandari ya Luanda na pia kukifanya kitengo hicho kiwe kitovu cha biashara katika ukanda wa kusini magharibi mwa Afrika.

DP World starts operations of multipurpose terminal at Port of Luanda​


Luanda, Angola,
01
March
2021


 Suhail Al Banna, CEO and Managing Director of DP World Middle East and Africa


Suhail Al Banna, CEO and Managing Director of DP World Middle East and Africa.

Serikali ya Angola iliweka ushindani huo wa wazabuni na makampuni kadhaa ya kimataifa yakiwemo kama vile kampuni za Multipaques, Advanced Maritime Transport na China Harbour Engineering Company zilishiriki kupigania zabuni hiyo. Tume maalum ya kutathmini wagombea wa zabuni ambayo iliundwa rasmi na wizara ya masuala ya usafirishaji katika mpango wake uitwao Master Plan, ilikuja na uamuzi kwamba DP World ndo wenye sifa zinofaa na wapewe zabuni.

Sio siri, DP World ni kampuni kubwa yenye uwezo mkubwa na uzoefu wa kazi za kushughulikia makontena yapatayo milioni 70 kwa mwaka. Pia DP World inaweza kulipa kwa mwangalizi (Serikali ya Angola) kiasi cha dola milioni 440 kwa mwaka huku dolali zingine milioni 150 zikilipwa wakati wa utiaji saini na kabla kazi haijaanza!, yaani kwa lugha ingine "Kifunga Uchumba!"

Kwahiyo tumejifunza nini hapo?

Kwanza, tumejifunza kwamba serikali ya Angola bado ni mmiliki wa bandari zote za Angola na imeingia makubaliano na kampuni ya DP World kuendesha shughuli za makontena tu na si vinginevyo katika bandari ya Luanda.

Pili, serikali ya Angola iliweka ushindanishi wa zabuni kwa makampuni mbalimbali yakiwemo ya kimataifa yalotaka kufanya kazi katika bandari ya Luanda. Zabuni hiyo ilitangazwa mwezi December 2019 na DP world ikaja tangazwa kuwa imeshinda zabuni hiyo mapema mwaka 2020. Jambo hilo laonyesha wazi kwamba serikali iliweka jambo hilo wazi na kujulikana wazi kwamba si siri.

Tatu, Serikali ya Angola kupitia wizara ya usafirishaji iliunda tume maalum ya kutathmini zoezi zima la kutafuta wazabuni na kuweka ushindanishi. Hilo pia linalinda heshima kwa serikali (integrity) na imani kwa wnaanchi wake na pia kuonyesha kwamba serikali yajali raia wake na imeweka mbele maslahi ya nchi zikiwemo mali za taifa.

Tumeambiwa kwamba mazungumzo ya mkataba huu yalianza tangia mwaka 2019 hivyo kuwa sawa kabisa na wenzetu wa Angola katika mahckato mzima, je ni wapi tulikwama katika kuhakikisha kunakuwepo ushindanishi wa kupata mzabuni? Au je, kuna tume yoyote iloundwa chini ya wizara ya biashara na viwanda au wizara ya ujenzi au usafirishaji ilohakikisha kuwa kuna uwazi /openness) katika hili na kutathmini mchakato mzima wa kumpata mzabuni?

Je, hili suala ni la kulipeleka Bungeni kwa kuidhinisha tu (rubber stamp) bila kuzingatia maoni ya wananchi au uwepo wa tume hiyo ambayo ingekuwa ikifanya kazi yake kwa niaba wananchi na maslahi ya taifa kwa ujumla?

Je, ni kwanini tumechukua hatua tulizochukua ambazo ni tofauti na hatua ambazo wenzetu na waafrika wenzetu serikali ya Angola imechukua? Je kwanini tusiombe ushauri wa ndugu zetu Angola kwenye hili ili tupate mawazo mazuri ya namna ya kumpata mzabuni hata kama ni DP World kwa kutumia njia sahihi?

Naomba nimalizie kwa kusema yafuatayo:

Hii nchi ni yetu sote na kila maamuzi ambayo serikali yachukua yawahusu watanzania wote na kizazi kijacho, hivyo serikali inawajibika kwa hatua zozote zinohusu maslahi ya taifa hili.

Pia serikali isidharau kauli, ushauri na mijadala mbalimbali kuhusu jambo hili kwani ni fukuto kubwa sana ndani ya mioyo ya watanzania ambao wanazo video zote zinohusu suala la bandari tangia mchakato wake uanze.

Na mwisho, serikali isitishe kuwatumia baadhi ya watu inaoamini kuwa wana ushawishi (influence) kwa jamii hivyo kuweza kusawazisha mambo na kuyapitisha malengo yake yenye kasoro nyingi. Watu hawa ni kweli wana nguvu kubwa ya ushawishi iwe kwenye mitandao ya kijamii, vituo vya redio au televisheni, lakini baadhi yao wamekosa weledi, uwezo wa kufikiri kwa kina na ni waendekezaji mizaha.

Suala linohusu maslahi ya taifa halihitaji mizaha.

Vyanzo vilivyochangia mada hii: Trifigura, DP World Luanda Port, Maritime Institute na vyombo kadhaa vya habari.
Baada ya kusoma heading tuu nikajua umeandika ujinga..

Waziri Mbarawa alisema zaidi ya makampuni 8 yalijitokeza na DP World ndio ikashinda Kwa vigezo Sasa huu upotoshaji unatoka wapi?
 
Walipewa mkataba wenye vipengele kama hivi vya kwetu?

Hoja kuu zinazohitaji majibu ni hizi hapa

1.) Tofauti ya ‘Makubaliano’ na ‘Mkataba’ ni ipi hasa kiasi mseme ule sio mkataba, kwamba ni makubaliano tu ya awali, na je Mkataba huo (makubaliano hayo) ni wa miaka mingapi? (UKOMO)

2.) Ni kwa faida ya nani kwamba DPW anapewa haki ya bandari zote za Tanganyika, kwamba hakuna mwekezaji mwingine yeyote anaweza kuja kufanya uwekezaji kwenye bandari za Tanganyika bila udalali wa DPW, je, ukiritimba huu ni kwa faida ya nani?

3.) Ni kwa faida ya nani, DPW apewe haki ya kudai kipande chochote cha ardhi yenye ukubwa wowote anaoutaka yeye ndani ya ‘Territory’ ya Tanganyika na sisi tumpe ardhi hiyo kwa kuondoa watu na miradi yote ndani ya eneo alilolitaka, na tumpatie bire kabisa kwa gharama zetu sisi, hata fidia tulipe sisi ili kuondoa watu kumpisha, huu uwendawazimu ni kwa faida ya nani?

4.) Ni kwa faida ya nani, kwamba sisi tuliowekeza matrillion ya mikopo kuendeleza bandari na tukiwa kama wamiliki wa rasimali ya bandari, tupate 0% ya faida itakayotokana na uendeshaji wa huduma za kibandari, yaani ni kana kwamba yeye kawekeza 100% na hivyo achukue 100%? Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

5.) Ni kwa faida ya nani, kwamba mkataba unahusisha bandari za Tanganyika tu na sio za Zanzibar, ilihali bandari ni suala la Muungano? Je, Zanzibar haitaki kunufaika au yenyewe haitaki matunda ya mkataba huu? Ukizingatia walioongia huu mkataba wote ni waZanzibari, kuanzia Samiah Suluhu Hassan, Makame Mbarawah, Hamza Johari na wenzao, kwamba hawataki Zanzibar yao ipate matunda mazuri ya mkataba huu?!

6.) Ni kwa faida ya nani kusema kwamba, hata DPW akavunja mkataba na kukiuka kanuni na taratibu zote zinazotambulika kimataifa, bado hatutaweza kuvunja , kuusema vibaya au kujitoa kwenye mkataba, milele! Uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?

7.) Ni kwa faida ya nani kwamba pamoja na kuwa DPW watachukua 100% ya faida, bado tena faida hiyo watapewa Msamaha wa kodi kwa 100%, yaani hata hicho wanachovuna nacho hatuchukui kodi, na wakti huo huo tunakamuliwa kodi za miamala, uwendawazimu huu ni kwa faida ya nani?
Makubaliano hayana msingi wa kisheria hayo mambo ya mda Serikali imeshasema yataonekana kwenye mkataba wa utekelezwaji Sasa shida Iko wapi?
 
Tungefuata utaratibu wa manunuzi sidhani kama kungekuwa na malalamiko.

Hata tungefanya kwa single source na
Baada ya kusoma heading tuu nikajua umeandika ujinga..

Waziri Mbarawa alisema zaidi ya makampuni 8 yalijitokeza na DP World ndio ikashinda Kwa vigezo Sasa huu upotoshaji unatoka wapi?

kuwapa DPW pia kusingekuwa na tatizo lolote.

Watu hawaichukii DPW au uwekezaji, watu wanachukia ujinga wa viongozi wetu kuingia mikataba ya kipumbavu kila mara.
Lazima mngezusha lingine mana hamnaga sera zozote mnasubili ccm iwape mfupa ili muutafune. Mko kama fisi
 
Back
Top Bottom