Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 21,552
- 52,287
ANAYOFANYA CHRISTINA SHUSHO NI MATOKEO YA WANAUME WENGI KUOA WANAWAKE WATUMWA "WASIOHURU. SIKU WAKIPATA UHURU WAO HAYO NDIO HUTOKEAGA.
Anaandika Robert Heriel
Mtibeli
Huwezi mfanya Mwanamke mtumwa alafu ukamuita Mkeo.
Unajua Watu wengi wamechukua wanawake na kuwageuza watumwa wa kingono na vijakazi wao alafu hujinasibu kuwa Wameoa. Hakuna ndoa ya hivyo. Sema umemnunua Mwanamke na kumgeuza mtumwa wa ngôno na kijakazi wako hapo sisi Watibeli tutakuelewa.
Mfano, kwenye ndoa hakunaga ndoa ya Wake wengi. Ila kwenye utumwa wanaume huruhusiwa kuchukua wanawake watumwa wengi na kuwaita Wake zao ilhali sio kweli na sio Haki.
Kama ilivyo kwa sisi wanaume tusivyoweza kukubali kuwa na Mwanamke mwenye mahusiano na wanaume wawili. Ndivyo hivyohivyo kwa wanawake.
Wanaume wengi hupenda kuishi na Wanawake watumwa kuliko kuoa Mke. Sio ajabu wanaume wengi hujiamini na kutaka Mwanamke mwenye kipato duni au asiyefanya kazi, na wengi huenda mbali kwa kuchukua vibinti vidogo ili wavitumikishe kitumwa.
Kimantiki huwezi pata kitu kinachoitwa heshima kwa mtumwa. Mtumwa hawezi kukupa heshima. Heshima hutolewa na Watu Huru.
Kupewa heshima na mtu asiyehuru au mtumwa huitwa nidhamu ya woga, unafiki na ulaghai.
Kuoa Mwanamke mdogo kiumri ambaye hana maamuzi sio tuu ukatili bali pia ni dhulma ambayo baadaye lazima iligharimu.
Mimi kama Mtibeli halisi nasema, hasa kwa vijana. Ikiwa unahitaji kuishi na mwanaume ambaye utamuita mke basi yakupasa ûtafute mwanamke aliyehuru.
Namaanisha huru kiakili, kihisia, kimwili na kiroho.
Christina Shusho NI kielelezo cha wanawake wengi walioolewa pasipo uhuru wao kuheshimiwa na kuthaminiwa.
Nilieleza pia, Mke hatolewi Mahari. Ila watumwa hutolewa mahari.
Mwanamke aliyehuru hawezi kukubali kutolewa mahari kwa sababu mahari msingi wake mkuu ni kumdunisha Mwanamke na kumdhalilisha ingawaje kwa umbo la nje waliolianzisha walilifanya kama kumheshimisha.
Mwanaume ni bora ikiwa atajua kusimamia Haki. Na Mwanamke atakuwa bora kama mwanaume ikiwa atajua haki zake na nani wa kuzisimamia.
Usioe Mwanamke asiyehuru(tegemezi) na kama utamuoa basi hakikisha unampatia uhuru wake. Ajitegemee.
Usimuozeshe binti yako kama bado hayupo huru. Huko ni kumkosea binti yako.
Usioe Mwanamke asiyefanyakazi, na kama umemuoa akiwa hana kazi basi hakikisha unampa kazi au anasimamia kazi na miradi ya familia. Nazungumzia kazi za kuzalisha kipato sio kazi za nyumbani. Kazi za nyumbani zitafanywa na mtu yeyote au machine. Baba au mume uwe kiongozi alafu mke au mama awe msaidizi. Hiyo ndio tafsiri ya ndoa kama hamtaki iwe ndoani.
Usioe Mwanamke ambaye hakupendi(moyo wake haupo huru na wewe). Atakusumbua na wewe utamsumbua.
Usimlazimishe Mwanamke kuwa na wewe hata kama mmeishi miaka mingi.
Usiingilie uhuru wa mtu mwingine wa kuchagua na kuutendea mwili wake. Kama ameku-cheat na anataka mwanaume mwingine muache aende.
Elewa, Mwanamke aliyehuru hadanganywi ila anafanya kwa Makusudi.
Ila watumwa hudanganywa kwa sababu wapo kwenye harakati za kutafuta uhuru wao.
Usioe mwanamke asiyeweza kujitunza mwenyewe, wala kujitafutia kipato. Huyo sio mke, huyo ni mtumwa.
Mke mchapakazi haimaanishi kazi za nyumbani pekee bali kazi za uzalishaji mali. Hata siku usipokuwepo unajua kabisa ile ndoto ya familia uitakayo itatimizwa na mkeo. Na sio ukifa basi watoto wako ndio habari imeisha.
Oa Mwanamke anayejua Haki zake kwani mtu kujua haki zake ni tafsiri ya kujua haki zako pia.
Mtu asiyejua haki zake hawezi kujua haki zako.
Elewa, mwanamke anayekubali kuonewa jua naye kuna sehemu ànakuonea au upo wakati unaokuja atakuonea tuu. Kwa sababu hiyo ni HAKI.
Ukijiona wewe ni mwanaume na unathamani kwenye ndoa kuliko Mwanamke elewa hata mwanamke atajiona anathamani kuliko wewe. Haitakuwa ndoa bali ndoano full kuumizana.
Lakini ukijitoa kwa mwenzako naye atajitoa. Ukimtañguliza mwenzako naye atakutanguliza.
Heshima yako kama mwanaume haipo kwa kumfanya Mwanamke mtumwa wako. Ila ipo kwa kumfanya Mwanamke kuwa Mtu na kulinda utu wake.
Yale yote unayotaka kufanyiwa basi mfanyie mwenzako. Na yale yote isiyotaka kufanyiwa basi usimfanyie mwenzako.
Kuwa mwanaume sio tafsiri ya tiketi ya kufanya dhulma na uhalifu wa kijinsia kwa Mwanamke.
Kama nilivyoandikaga, kuwa mzazi sio kigezo cha kufanya dhulma kwa watoto wako kisa uliwazaa.
Ni ruhusa na Haki yako kumuacha(kutoa talaka) Mwanamke ambaye ulimpenda, na ukafanya kila jitihada na kuheshimu na kulinda ûtu na hadhi yake na yako lakini ikashindikana. Vivyohivyo kwa Mwanamke.
Ni yule Mtibeli kutoka nyota ya Tibeli.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Kahama, Shinyanga.
Anaandika Robert Heriel
Mtibeli
Huwezi mfanya Mwanamke mtumwa alafu ukamuita Mkeo.
Unajua Watu wengi wamechukua wanawake na kuwageuza watumwa wa kingono na vijakazi wao alafu hujinasibu kuwa Wameoa. Hakuna ndoa ya hivyo. Sema umemnunua Mwanamke na kumgeuza mtumwa wa ngôno na kijakazi wako hapo sisi Watibeli tutakuelewa.
Mfano, kwenye ndoa hakunaga ndoa ya Wake wengi. Ila kwenye utumwa wanaume huruhusiwa kuchukua wanawake watumwa wengi na kuwaita Wake zao ilhali sio kweli na sio Haki.
Kama ilivyo kwa sisi wanaume tusivyoweza kukubali kuwa na Mwanamke mwenye mahusiano na wanaume wawili. Ndivyo hivyohivyo kwa wanawake.
Wanaume wengi hupenda kuishi na Wanawake watumwa kuliko kuoa Mke. Sio ajabu wanaume wengi hujiamini na kutaka Mwanamke mwenye kipato duni au asiyefanya kazi, na wengi huenda mbali kwa kuchukua vibinti vidogo ili wavitumikishe kitumwa.
Kimantiki huwezi pata kitu kinachoitwa heshima kwa mtumwa. Mtumwa hawezi kukupa heshima. Heshima hutolewa na Watu Huru.
Kupewa heshima na mtu asiyehuru au mtumwa huitwa nidhamu ya woga, unafiki na ulaghai.
Kuoa Mwanamke mdogo kiumri ambaye hana maamuzi sio tuu ukatili bali pia ni dhulma ambayo baadaye lazima iligharimu.
Mimi kama Mtibeli halisi nasema, hasa kwa vijana. Ikiwa unahitaji kuishi na mwanaume ambaye utamuita mke basi yakupasa ûtafute mwanamke aliyehuru.
Namaanisha huru kiakili, kihisia, kimwili na kiroho.
Christina Shusho NI kielelezo cha wanawake wengi walioolewa pasipo uhuru wao kuheshimiwa na kuthaminiwa.
Nilieleza pia, Mke hatolewi Mahari. Ila watumwa hutolewa mahari.
Mwanamke aliyehuru hawezi kukubali kutolewa mahari kwa sababu mahari msingi wake mkuu ni kumdunisha Mwanamke na kumdhalilisha ingawaje kwa umbo la nje waliolianzisha walilifanya kama kumheshimisha.
Mwanaume ni bora ikiwa atajua kusimamia Haki. Na Mwanamke atakuwa bora kama mwanaume ikiwa atajua haki zake na nani wa kuzisimamia.
Usioe Mwanamke asiyehuru(tegemezi) na kama utamuoa basi hakikisha unampatia uhuru wake. Ajitegemee.
Usimuozeshe binti yako kama bado hayupo huru. Huko ni kumkosea binti yako.
Usioe Mwanamke asiyefanyakazi, na kama umemuoa akiwa hana kazi basi hakikisha unampa kazi au anasimamia kazi na miradi ya familia. Nazungumzia kazi za kuzalisha kipato sio kazi za nyumbani. Kazi za nyumbani zitafanywa na mtu yeyote au machine. Baba au mume uwe kiongozi alafu mke au mama awe msaidizi. Hiyo ndio tafsiri ya ndoa kama hamtaki iwe ndoani.
Usioe Mwanamke ambaye hakupendi(moyo wake haupo huru na wewe). Atakusumbua na wewe utamsumbua.
Usimlazimishe Mwanamke kuwa na wewe hata kama mmeishi miaka mingi.
Usiingilie uhuru wa mtu mwingine wa kuchagua na kuutendea mwili wake. Kama ameku-cheat na anataka mwanaume mwingine muache aende.
Elewa, Mwanamke aliyehuru hadanganywi ila anafanya kwa Makusudi.
Ila watumwa hudanganywa kwa sababu wapo kwenye harakati za kutafuta uhuru wao.
Usioe mwanamke asiyeweza kujitunza mwenyewe, wala kujitafutia kipato. Huyo sio mke, huyo ni mtumwa.
Mke mchapakazi haimaanishi kazi za nyumbani pekee bali kazi za uzalishaji mali. Hata siku usipokuwepo unajua kabisa ile ndoto ya familia uitakayo itatimizwa na mkeo. Na sio ukifa basi watoto wako ndio habari imeisha.
Oa Mwanamke anayejua Haki zake kwani mtu kujua haki zake ni tafsiri ya kujua haki zako pia.
Mtu asiyejua haki zake hawezi kujua haki zako.
Elewa, mwanamke anayekubali kuonewa jua naye kuna sehemu ànakuonea au upo wakati unaokuja atakuonea tuu. Kwa sababu hiyo ni HAKI.
Ukijiona wewe ni mwanaume na unathamani kwenye ndoa kuliko Mwanamke elewa hata mwanamke atajiona anathamani kuliko wewe. Haitakuwa ndoa bali ndoano full kuumizana.
Lakini ukijitoa kwa mwenzako naye atajitoa. Ukimtañguliza mwenzako naye atakutanguliza.
Heshima yako kama mwanaume haipo kwa kumfanya Mwanamke mtumwa wako. Ila ipo kwa kumfanya Mwanamke kuwa Mtu na kulinda utu wake.
Yale yote unayotaka kufanyiwa basi mfanyie mwenzako. Na yale yote isiyotaka kufanyiwa basi usimfanyie mwenzako.
Kuwa mwanaume sio tafsiri ya tiketi ya kufanya dhulma na uhalifu wa kijinsia kwa Mwanamke.
Kama nilivyoandikaga, kuwa mzazi sio kigezo cha kufanya dhulma kwa watoto wako kisa uliwazaa.
Ni ruhusa na Haki yako kumuacha(kutoa talaka) Mwanamke ambaye ulimpenda, na ukafanya kila jitihada na kuheshimu na kulinda ûtu na hadhi yake na yako lakini ikashindikana. Vivyohivyo kwa Mwanamke.
Ni yule Mtibeli kutoka nyota ya Tibeli.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Kahama, Shinyanga.