Anayejua habari za JKT

Anayejua habari za JKT

Daah Haya Bana wabongo kwa kunyanyasana kihadhi na kinafasi bana acha Tu Basi Aisee Ila najiuliza Mleta Uzi je?
Basi Aisee business hii naicha coz all Eyez on me .
Nadhan kama umesoma sheria kuna kfungu knasema right to speak ila without kuvunja sheria....nadhan kwzi ile ya shetani bado inaendelea HAKUNA KUNYAMAZA CHANGIA WAT U FEEL IS RIGHT without excuse ...kwan ye nan??
 
Mkuu unajua umeongea mengi sana? Nakushauri usiandike chochote kwenye huu uzi.
Weww kama nan??kwan anakula kwenu huyu MAKANYA??embu acha hizo mambo kuwa na heshima jarbu kuheshimu mawazo ya mwingine hakuna sehemu umetukanwa wala kukukejeri huu uzi ulianzishwa ili watu watoe updates mbalimbali kama kuna any information. ..if ur not interested u can find another place that fits u.. tuache sisi tunaopeana hope bakia ww mwenye uhakika wa kwenda
 
Asante Mkuu, namaanisha hapohapo Tanzania Postal Bank. Kama anayekata viuno ili kunufaisha familia yake na watoto sio vibaya sana.

Nipo hapa TPB kama Channel ya kuniweka vizuri ili niende sehemu nyingine, mshahara wa hapa ni tegemezi kwangu na kwa wengine. Ninachokipata nitawaachia wanaonitegema kwa kiasi flani ili kiwasaidie punde nikienda JKT.

Naenda JKT kutazamia kutimiza ndoto zangu, katika maisha yangu nafanya kile ambacho moyo wangu unatamani, napenda sana kuwa na amani. Nikishindwa JKT na seheme zingine zote ambazo zinaweza kutimiza ndoto zangu basi nitatafuta kazi nyingine ya kufanya, ila kwa sasa bado sijakata tamaa kwamba siwezi timiza ndoto yangu. Na sijaona cha kunizuia ili nisitimize ndoto yangu.

Sijui kwanini umesema mimi ni muanzilishi wa Thread zinazohusu JKT, unaweza ukanionesha ni thread gani nimeanzisha? Napenda kuingia ktk Thread zinazohusu JKT ili nijue naenda wapi na inabidi nifanye nini ili kukabilia na changamoto hizo kabla ya kuanza mafunzo na baada.

Wewe ni mtu mzima, kama umetimiza malengo yako basi hongera sana, sisi bado tuna kwenye process, hata wewe ulivyokuwa kwenye process haukutamani ukatishwe tamaa, na sisi pia hatutamani kusikia mambo vitu hasi bali chanya.

Umeongea mengi na maneno ya ajabu na matusi kedekede ila naomba nikwambie kwamba mimi ndo kwanza naona umenipa hali mpya na shauku mpya ya kuingia JKT, mahali palikuwa na shida au kikwazo mbele basi kuna ushindi karibu. Wana wa Israel walikutana na ukuta wa Yeriko ila Yeriko ilidondoka, walipita jangwani ila Mungu aliwapa maji ktk mwamba, Wana wa Israel walivyoona bahari, waliingiwa na wasiwasi ila baadae mlango ukafunguka, vijana wenzangu mnaosubiri nafasi za JKT nawaambia ya kwamba mlango utafunguka. Usisikilize maneno ya watu wanakwambia nini, tazama moyo wako una shauku ya nini. Wapinzani ni wengi na vita ni nyingi ila nawasihi tupambane, Mungu atafungua mlango.

Kusudi la Mungu haliwezi kuzuiwa na chochote kile, cha msingi ni uvumilivu na kujiandaa kisaikolojia.

Nawapenda sana vijana wenzangu.
Aisee ningekua msimamizi Wa usali kwenye wilaya au mkoa wako nafasi ungepata..

Jeshi haliitaji kukata tamaa kizembe wanangu.
 
Nafasi zmeshatangazwa source my bro captain pale navy kgamboni ndo kanambia now niende kwa mshauri wa mgambo nikfka nmpgie simu....usipuuzie nenda kwa mkuu wa mkoa now
Huyu bro ako CAPTAIN Navy kigamboni anasemaje kwa sasa?? Alikwambia nafasi zimetoka kitambo tu, vp umeshaenda depo afandeee?

Bila Shaka atakuwa captain feki
 
Huyu bro ako CAPTAIN Navy kigamboni anasemaje kwa sasa?? Alikwambia nafasi zimetoka kitambo tu, vp umeshaenda depo afandeee?

Bila Shaka atakuwa captain feki
Jna lako na comments znaendana keep it up RAZA
 
Mimi nadhani tuwe na subira,muda ukifika tutapambana,hapa kila mtu ana chanzo chake cha habari,ambacho kwa namna moja au nyingine hatuna uhakika na hizo source zao za information.
 
Najiuliza..watu wanavyohustles hivi kupata chance na imetokea umemaliza miaka yako miwili unapewa cheti unaambiwa rudi nyumbani si yatatokea kama yale ya mwaka juzi ya askari wa JKT kugoma?

Mungu awasimamie kwa sababu ni kweli kabisa sio kila anaeenda NS huwa anapata chance ya kukatwa bogi la maana.Wengine watarudi uraiani
 
Back
Top Bottom