Marando ninamfahamu binafsi japo siyo kwa karibu sana. Alikuwa ni mmoja wa timu ya usalama wa taifa nyakati za Nyerere ambapo kulikuwa na timu kali sana ya akina Walingozi. Hata hivyo mwanzoni mwa mwaka 1987, ikiwa ni ndani ya mwaka mmoja tu baada ya Nyerere kuondoka madarakani, timu ya usalama wa Taifa pale Ikulu ilibaidilishwa sana ikiwa ni pamoja na kustaafishwa kwa Opiyo ambaye ndiye aliyekuwa mkuu wao. Marando akaanzisha kampuni yake ya sheria, kwa vile amesomea sheria, na ndipo pia alipoanzisha vuguvugu la kudai vyama vingi vya siasa kupitia ile mikutano yake ya NCCR; mimi nilihudhuria mikutano michache ya NCCR kabla hajaanzisha chama kilichopewa jina la NCCR-Mageuzi.
Sijajua lengo lake katika NCCR ile wakati huo kwani inawezekana ilikuwa ni preemetive tactics, ila kwa yeyote aliyekuwapo Tanzania mwaka 1995 enzi za NCCR-Mageuzi kabla haijachafuliwa na Mrema ni vigumu kuamini kuwa kweli Marando bado alikuwa akiitumikia serikali ya CCM wakati huo. Na iwapo alikuwa haitumikii CCM wakati huo, ninakuwa na ugumu kuamini kuwa atakuwa anaitumikia CCM leo