Kosa kubwa lililofanywa na Chama Kikuu cha Upinzani Tanzania 'CHADEMA' na hatua zinazopaswa kuchukuliwa ili kukirudisha Chama

Enzi na Enzi

JF-Expert Member
May 29, 2020
888
821
Wapendwa wana JF,

Nadiriki kuandika uzi huu hapa nikiamini wataalam wa mambo ya SIASA wapo katika jukwaa pendwa la JF.

Mada yangu ni kuangazia makosa yaliyofanyika mpaka chama cha demokrasia na maendereo chadema kikafikia hatua hii mbaya kilipo kwa sasa.

Hili halina ubishi kuwa CHADEMA kina wakati mgumu kuliko nyakati zote katika siasa hapa Tanzania.

Hakuna ubishi kuwa, chadema kweli kilikuwa nichama cha demokrasia tukiacha maendeleo. Hili linathibitika wazi kuwa! CHADEMA ndo iliibua vijana wengi na kuwajenga kisiasa kitu kilichoperekea kuiamsha hata CCM.

MAKOSA WALIYOFANYA CHADEMA

1. Kiburi

Chadema walijawa na kiburi baada yachama kukubarika mpaka ngazi ya vijijini na raia wa kawaida ukiacha wenye heshima za utajiri, elimu, nk. Ni kweli ndani ya Chadema kulikuwa na kuheshimiana, umoja na kupendana, badala ya kuendeleza utamaduni huo, wakajawa na kiburi wakaanza kubaguana kwa kigezo cha elimu, umaarufu, ukwasi wa fedha na ukanda. Walikuja kushtuka baadae wakiwa wamechelewa, wakaanza kutoa vyeo kwa misingi ya usawa japo ilikuwa too late.

2. Tamaa
Walijawa na tamaa ya kutaka njia ya mkato kuchukua nchi nakuacha misingi mizuri iliyowajenga ! Pamoja na maonyo ya watu walioona mbari lkn hawakujari ! Hii inanikumbusha ajari mbaya ya meli ya Titainic iliyotokea baada ya Nahodha kudharau maonyo kwa sababu ya kiburi nakweli meli ilizama.

Nakumbuka DR. W. Slaa alionya kuwa E. N Lowasa asipokelewe na kukabidhiwa kugombea urais kwakuwa ilikuwa ni kazi ngumu kumsafisha uchafu ambao wao walimpaka, akaishia kuambiwa alitaka urais! Hata kama ilikuwa ndivyo, ni bora ya Dr. ambaye alikuwa zao la Chadema.

Chadema walisahau kuwa walikuwa ndani ya mapambano ambayo haikustahiri mateka mlie mteka apewe siraha na awe mshauri wenu huku akiwaongoza katika vita na maadui ambao yeye alikuwa upande wao.

Lakini haikutosha wakawachukua wana CCM wengi ambao hata kwa hakiri ndogo kwa hadhi waliyofikia hawawezi kufia chama tofauti nakinachowapa ridhiki wao na watoto wao kizazi na kizazi, *hii ilikuwa tamaa*

3. Siasa za uanaharakati
walisahau kuwa siasa ni siasa na harakati ni harakati, wakaingiza harakati za kuanza kutukana viongozi, ubabe, kupinga kila kitu! Wakashusha hadhi ya siasa nakujipambanua kuwa wao ni wanaharakati, tabia hii iliperekea kila ntu kuwashangaa!

Wakatuna mahakama, wakatukana police, wakatukana Rais na mawaziri, wakuu wa mikoa nk. Ikafika sehem kila mtu ndani ya chadema akawa msemaji simwanamke si mwanamme watanzania wakawashangaa. CCM wakakaa kimya, wakaandaa ntu mmoja wa kuwajibu kiuanaharakati nae ni MSIBA. Hoja za serikari zikajibiwa na Dr Abasi, Msemaji wa serikali, hoja za chama zikajibiwa na Polepole au Dr Bashiru Ally! Wao ikawa vurugu! Leo heche, kesho Msigwa, usiku Lema, mchana Ester Bulaya, asubuhi Halima Mdee, mara John Mrema, mara Mangi Kimambi, mara Fatma Karume na wengine; kifupi ikawa vurugu.

Chadema nahisi waliwadharau katibu mkuu Dr Mashinji, Prof. Baregu, Prof. Safari na wengine. Wakaingia mkenge wakujibishana na mkuu wa mkoa wa Dar P. Makonda, akawa anawajoki kwa kuwapa matamko ya kisiasa wanajaa hasira! Nahisi CCM ilikuwa imewasoma. Na kama kuna mtu kacheza nao Chadema, ni P. Makonda. Mi namuona anaijua siasa.

4. Chadema wakaanza kutetea wezi, wauza dawa za kulevya, wahujumu uchumi, vibaka na wanywa viroba!
Vyeti feki napo wakatetea, wakapinga utumbuaji mda huo wananchi wakifurahi. Nadhani ilifika hatua taarifa ya habari bila kusemwa magufuri haikunoga kwa watazamaji. Hili lilikuwa nikosa, wakawa wanashangilia ndege zetu kukamatwa, wakatamka bungeni na kwenye mitandao kuwa Barrick itaishitaki nchi matokeo yake rais wa Barrick akatia team kwa ndege binafsi. Hili nalo lilikuwa kosa kubwa kama chama kinachotaka kushika dola.

5. Covid19
Korona imewamaliza sana chadema, nabila aibu hawakutaka kujisahihisha mapema, kwani aliyetoa tamko ni ester bulaya baada ya malalamiko alitakiwa mbowe atengue hyo kauli mapema lkn wakashadidia kiasi kwamba mpaka wao kwa wao ikawala , na mbaya zaidi Dr john pombe magufuri akawa mshindi baada ya shirika ka afya WHO kukariri yaleyale aloyasemq mh. Rais, baadae marekani na nchi jirani nao wakaufyata mkia! Hapo napo walikurupuka.

Kelele zilizopigwa mda mlefu za rudhuku ya chama kuliwa na watu wachache zikashika kasi, utemi ndani ya chama ukashika kasi mambo ambayotulionya mapema, nahata wanapokuja na majibu hawajibu maswali ya wanachama kuhusu matumizi ya rudhuku, ujenzi wa ofice za chama mikoani na masrahi ya wanachama wengine.

NINI CHA KUFANYA


Chadema mkubari matokeo yakuwa chama mmekipasua kwa mambo niliyoyataja na mengine mengi ambayo sikuyaeleza humu!! Inabidi mtulie mrudi kuziba ufa japo nikazi ngumu, muachane na siasa za matusi na na siasa za kuvizia. Kama kweli mnataka kuchukua dola. Huwezi ukamtukana IGP ukamtukana TISS, ukatukana MAHAKAMA ukamtukana RAIS hasa asiye mwizi na ukafanikiwa.

Hata kama ni wabaya kwako cheka nao lakini si wema kwako! Siku wakiingia anga zako unawalipua. Lakini hizo siasa mnazofanya za kutegemea mataifa ya magharibi, na wanaharakati hazitawasaidia.

Yupo wapi Mabere Nyaucho marando? Yupo wapi Prof A. Safari? Yupo wapi Dr W. Slaa? Yupo wapi W. Lwakatare? Mmekaa mkajiuliza kwanini wabunge na wanachama wanahama chama? Je, wote wananunuliwa? Kama ndiyo, kwa nini wanunuliwe? Je, na nyie mlinunua wabunge na wana CCM waliohamia kwenu?

ANGALIENI MLIPO ANGUKA MKAPATENGENEZE MUENDELEE NA SAFARI

Enzi na enzi

Dar es salaam.
 
Mambo ni motoooo
 

Attachments

  • IMG_20200531_121920.jpg
    IMG_20200531_121920.jpg
    45.6 KB · Views: 4
Kila kitu kama kimepangwa hivyo no way out but I believe that uwanja wa siasa ukiwa wa Uhuru na haki hayo maelezo yako is nothing.

Potelea pwete wacha INIUE.
 
Kuweka kumbukumbu sawa! Kwenye hiyo namba 2 ni kwamba Dr. Slaa hakuwa zao la Chadema. Aliingia Chadema mwaka 1995 akitokea Ccm mara tu baada ya kuondolewa kwa zengwe kwenye mchujo wa kura za maoni kugombea Ubunge Jimbo la Karatu.

Baada ya kuhamia Chadema ndipo aliposhinda kwenye huo uchaguzi na kuwa mmoja wa Wabunge wachache wa Chadema kuchaguliwa kwa wakati huo.

Hivyo hana tofauti na baadhi ya Makamanda wengine wakiwemo akina Mchungaji Msigwa, Lema na hata Mbowe mwenyewe usikute naye alikuwa ni Kada Mtiifu wa CCM kabla ya kuanza kwa Mageuzi ya Kisiasa ya mwanzoni mwa miaka ya 1990's
 
Kuweka kumbukumbu sawa! Kwenye hiyo namba 2 ni kwamba Dr. Slaa hakuwa zao la Chadema. Aliingia Chadema mwaka 1995 akitokea Ccm mara tu baada ya kuondolewa kwa zengwe kwenye mchujo wa kura za maoni kugombea Ubunge Jimbo la Karatu.

Baada ya kuhamia Chadema ndipo aliposhinda kwenye huo uchaguzi na kuwa mmoja wa Wabunge wachache wa Chadema kuchaguliwa kwa wakati huo.

Hivyo hana tofauti na baadhi ya Makamanda wengine wakiwemo akina Mchungaji Msigwa, Lema na hata Mbowe mwenyewe usikute naye alikuwa ni Kada Mtiifu wa Ccm kabla ya kuanza kwa Mageuzi ya Kisiasa ya mwanzoni mwa miaka ya 1990's
Haijalishi alitokea wapi? Lakini alikijengea heshima Chadema.
 
Enzi na Enzi,

Ni article ndefu sana na bahati mbaya yako ni kuwa haivutii kuisoma....

Nimeishia mistari miwili tu kusoma na kukinai moja kwa moja...

Na nadhani pia ni kwa sababu umeandika UONGO wa MAMBO ambayo hata wewe mwenyewe huyaamini....yaani unapiga propaganda mfu.
 
Enzi na Enzi,

Sijui ni tatizo gani limeikumba ccm hivi sasa, fuatilia vizuri huku mitandaoni, kuna Id mpya na wote wanaiponda cdm, na kumsifia Magufuli. Na kujisahau au kwa maelezo maalumu huwa wanamtaja Makonda. Tatizo kubwa la kundi hili jipya asilimia 90 ya hizi id mpya hawajui kanuni za uandishi. Wengi wao hawajui wapi waweke koma, nukta, nafasi baina ya neno na neno, alama mbalimbali kama za mshangao, kuuliza nk. Mfano mzuri ni ww mleta mada, pitia bandiko lako ni kama chakula kilicho ndani ya mavi.

Ajenda kubwa ya nyie vilaza mliojazwa humu ndani na ccm/ Makonda, na kutupa sababu za kupandikiza kuwa ni kwanini cdm inaanguka. Kana kwamba hatujui kuwa cdm haianguki, bali kuna siasa chafu kupitia ulevi wa madaraka ndio zinazotaka kuiangusha cdm. Nawashauri hilo kundi jipya kuleni hizo hela za walevi wa madaraka, lakini pia mjiongeze kwa kujifunza kuandika kwa usahihi.
 
Naipenda CHADEMA toka moyoni sibabaishwi naa porojo. Kwenye harakati za kutetea nchi kuna watakao umia kwaajili ya wengine. Licha ya chadema kuumizwa bado iko mstari wa mbele kupigania maslahi ya wanchi. Nawakumbusha mataga mwende mkafuatilie michango na hoja mbalimbali za wabunge bubgeni utaona michango ya wabunge wa chadema +zito kabwe ndio yenye tija kuli ya wabunge mataga . Kwa hali hii mimi mzalendo wa nchi ni lazima niungane na wapigania haki na maslahi ya wananchi. People's Powerrrrrr !
 
Sijui ni tatizo gani limeikumba ccm hivi sasa, fuatilia vizuri huku mitandaoni, kuna Id mpya na wote wanaiponda cdm, na kumsifia Magufuli. Na kujisahau au kwa maelezo maalumu huwa wanamtaja Makonda. Tatizo kubwa la kundi hili jipya asilimia 90 ya hizi id mpya hawajui kanuni za uandishi. Wengi wao hawajui wapi waweke koma, nukta, nafasi baina ya neno na neno, alama mbalimbali kama za mshangao, kuuliza nk. Mfano mzuri ni ww mleta mada, pitia bandiko lako ni kama chakula kilicho ndani ya mavi.

Ajenda kubwa ya nyie vilaza mliojazwa humu ndani na ccm/ Makonda, na kutupa sababu za kupandikiza kuwa ni kwanini cdm inaanguka. Kana kwamba hatujui kuwa cdm haianguki, bali kuna siasa chafu kupitia ulevi wa madaraka ndio zinazotaka kuiangusha cdm. Nawashauri hilo kundi jipya kuleni hizo hela za walevi wa madaraka, lakini pia mjiongeze kwa kujifunza kuandika kwa usahihi.
Ushauri wako nimeukubali kuhusu makosa hayo madogo madogo! Hizo ni error typing mkuu! Naukizingatia mimi sio mwandishi, ila nilichogundua ujumbe umeusoma na ukauelewa, ndio maana hujapinga hoja hata moja wala kuleta utetezi juu ya nilichoandika zaidi kuishia kuandika matusi , ooh..! Mala Mavi mala nimetumwa na makonda!

Sijashangaa maana nishalisema hapo ktk andiko kuwa! Ccm waliwasoma chadema kuwa mnajazba na kiburi ! Wakajua namna ya kuwajibu.

Makonda nae alishawajua kuwa mnajaziba na ubabe, nae akawa anawapa maneno ya kisiasa ili mlopoke nakweli ndivyo ilivyokuwa!

Hii inaonyesha chadema wanapitia njia ile ile waliyopitia wote walokataa ushauli nahisi hata wewe utakuwa kundi la walewale au utakuwa mwanachadema.

COVID19 INAUA, CHAUKUA TAHADHALI
Enzi na enzi
Dar es salaam.
 
Naipenda CHADEMA toka moyoni sibabaishwi naa porojo. Kwenye harakati za kutetea nchi kuna watakao umia kwaajili ya wengine. Licha ya chadema kuumizwa bado iko mstari wa mbele kupigania maslahi ya wanchi. Nawakumbusha mataga mwende mkafuatilie michango na hoja mbalimbali za wabunge bubgeni utaona michango ya wabunge wa chadema +zito kabwe ndio yenye tija kuli ya wabunge mataga . Kwa hali hii mimi mzalendo wa nchi ni lazima niungane na wapigania haki na maslahi ya wananchi. People's Powerrrrrr !
Michango ya chadema bungeni ni tunataka dar es salaam Lockdown

Barrick atatushitaki mahakama ya usuruhishi tumuache abebe dhahabu kwa sababu tulisaini

Maridhiano ya kisiasa

Kufunga plaster mdomo

Kupinga burgert.

Hiyo ndio michango!! loh!!
Peoples power ni yakumchangia mh. Mbowe na kununua matrekta ifakara.
 
Michango ya chadema bungeni ni tunataka dar es salaam Lockdown

Barrick atatushitaki mahakama ya usuruhishi tumuache abebe dhahabu kwa sababu tulisaini

Maridhiano ya kisiasa

Kufunga plaster mdomo

Kupinga burgert.

Hiyo ndio michango!! loh!!
Peoples power ni yakumchangia mh. Mbowe na kununua matrekta ifakara.
Jamaa unauelewa mdogo sana, tulia pembeni soma michango ya wengine huku jf utaelimika.

Hii kitu "burgert" ndio nini?!
 
Majibu yenu yooote ni no 1 tu.

Ni article ndefu sana na bahati mbaya yako ni kuwa haivutii kuisoma....

Nimeishia mistari miwili tu kusoma na kukinai moja kwa moja...

Na nadhani pia ni kwa sababu umeandika UONGO wa MAMBO ambayo hata wewe mwenyewe huyaamini....yaani unapiga propaganda mfu....
 
Back
Top Bottom