Kufariki kwa ugonjwa au sababu nyingine yoyote (al8limradi hujauawa kwa ujambazi) siyo kejeli na wala siyo aibu.Kila Mtu akifariki corona, kwani Kabla ya corona Watu walikuwa hawafi.
Please tuache Kejeli za kishamba. Watu wa Kigoma tunamheshimu saaana, ndiye muasisi wa Uboreshaji wa zao la Michikichi.
R . I .P Brigedia Mstaafu Emmanuel Maganga Mzee wa Sauti ya Zege/Sauti nzito.
Corona ipo, inaua kama yanavyoua magonjwa mengine hatari. Tahadhari ichukuliwe kwa kufuatana na aina ya ugonjwa wenyewe, sawa na ambavyo huwa tunachukua tahafldhari kwa magonjwa mengine ya hatari.
Malaria ipo, kuna matangazo ya kuelimisha, kuna vyandarua vya misaada na vya kununua, na pia kuna madawa. Kwenye magonjwa ya mlipuko kama vile kipindupindu huwa kuna kunatolewa elimu ya kutosha na uhamasishaji wa kupambana nao. Kuna magonjwa ya hatari kama TB tunafanya hivyo hivyo. Kuna shida gani kwenye corona?
Ujinga ni kuwaaminielsha watu kuwa Tanzania hakuna corona. Uwendawazimu ni kusema tumeishinda corona. Tumeishinda corona, tumefanya nini hata kuishinda?
Siungi mkono lockdown, lakini ni vema kuukiri ukweli, tutoe elimu sahihi kwa watu wote ili watu wachukue tahadhari.
Ndugu yangu alipigwa vikali na corona. Amekaa hospital Dar siku 21 ICU, bill sh 7m. Mfanyakazi mwenzangu amepigwa corona Mwanza, amekaa ICU siku 14, nikaazuiwa hata kumwona. Halafu anatokea mjinga mmoja akuambie hakuna corona, mtu wa namna hiyo utamwitaji zaidi ya muuaji na hayawani?
Tuna ndugu zetu, watoto wetu, wadogo zetu, na marafiki zetu ni madaktari. Wanaeleza wazi uwepo wa huu ugonjwa. Mbaya zaidi wanasema wamezuiwa kabisa kusema mtu yeyote anaugua au amefariki kwa covid 19. Hivi sisi ni Taifa la namna gani? Rwanda hapo, Serikali imetangaza wazi kuwa mchumi wao mkuu wa Benki kuu amekuwa afisa wa kwanza wa juu kuuawa na Covid 19. Hivi kwa kuueleza ukweli huo, wamepungukiwa na nini?
Ndugu zangu hakuna aliye shujaa wa kifo. Hakuna anayechagua aina ya kifo (labda wale wanaojiua), na ndiyo maana huwezi kumdharau au kumkejeli mwanadamu yeyote kwa aina ya kifo chake.
Covid 19 ipo nchini, na bila ya jitihada za serikali, ni ngumu sana kuepuka magonjwa ya hatati ya kuambukiza maana inahitajika jitihada yako binafsi na ya wale wanaokuzunguka.
Serikali itoke na kuweka wazi hali ya ugonjwa wa Covid 19, na kuwaelekeza wananchi wanachotakiwa kufanya ili kupunguza maambukizi. Haya maneno ya kuwadanganya watu kuwa tumeishinda corona, ni uwendawazimu. Kwa maneno ya kipuuzi kama hayo tutashindwa hata kupata misaada ya chanjo (sasa hivi chanjo zote zinazotolewa nchini, ni za misaada toka mataifa wahisani) kwa mataifa ambayo yamekuwa yakitusaidia miaka yote. Gharama ya chanjo ya covid-19 kwa mtu mmoja ni dola 200 (TZS 450,000), sisi wenyewe hatutaweza.
Tuache ujinga, tuache kutafuta sifa na umaarufu wa kisiasa kupitia afya za raia. Corona ipo, na serikali inatakiwa kuchukua uongozi katika kupambana nayo.
Sent using Jamii Forums mobile app