TANZIA Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Brig. Jen Mstaafu Emmanuel Maganga afariki Dunia

Nakubaliana na wanajamvi kuwa corona ipo na haijawahi kuisha ila sio kila mtu anayefariki chanzo chake ni corona maana hata huko ambako maambukizi ni mengi magonjwa mengine hayajaacha kuchukua watu wa Mungu muhimu ni kuchukua tahadhari kwa kila mmoja wetu
 
Kujiita jiwe mbele ya korona ni ujuha na uuaji makusidi wa RAIA.
 
Rip
FB_IMG_1611291977675.jpg
 
Hivyo vifo vya mitandaoni kwani hawaishi mtaani mkuu

Ni kweli wanaishi mtaani mkuu ila nilichokuwa nataka aweke ushadi kutoka kwenye mtaa wake!!
Mtandaoni kila mtu anaandika chochote! .
Ila yote kwa yote corona ipo ila haiui maelfu ya watanzania Kama watu wanavyoandika humu.
 
kijana wa Rafiki ambaye ni Mhe. Hakimu Mkazi yangu pia amefariki dunia akipatiwa matibabu huko Tabora.
 
Kwanini tuangalie mitandao ya kijamii kuhusu wanao kufa mitaani?
Kwa sababu wewe uko mtaani ningependa kwa kuutumia mtaa wako kama mfano halisi utoe ushahidi jinsi mnavyozika watu kila siku sababu ya corona na sio kusema Mambo ya mitandao ya kijamii !

Twambie mtaani kwako kwa Siku mnazika watu wa ngapi?

Ndugu, jamaa , marafiki zako waliokufa kwA corona tuoneshe hizo data usiseme mitandao ya kijamii

Hawa wanaokata kumba kila kukicha hauoni? Jamaa zangu watatu wana corona!!
 
Inavyoonekana kabla ya corona ilikuwa tz hajawahi kufa maarufu.

Kweli wewe ni EMPTY HEAD ,unajua maana ya Takwimu? Fanya comparison ya 2017 Dec-April 2018 vs 2018 Dec-April 2019 vs 2019 Dec-April 2020 vs 2020 Dec-Up to Now kisha uje na UTUMBO wako.
 
Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Brigedia Jenerali mstaafu, Emmanuel Maganga amefariki dunia leo Usiku huu.

Taarifa za awali zinasema kuwa Brigedia Jenerali mstaafu, Emmanuel Maganga amefariki dunia wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Jeshi mkoani Tabora.

Alikuwa anaumwa nini, ama changamoto ya kupumua?
 
Kweli wewe ni EMPTY HEAD ,unajua maana ya Takwimu? Fanya comparison ya 2017 Dec-April 2018 vs 2018 Dec-April 2019 vs 2019 Dec-April 2020 vs 2020 Dec-Up to Now kisha uje na UTUMBO wako.

Hizo takwimu wewe umezitoa wapi ziweke hapa tuone!!
Tuseme Sasa hivi watu wanakufa sababu ya corona haya na hiyo miaka mingine uliyoweka walikuwa wanakufa sababu ya Nini?
 
Mkuu wa mkoa mstaafu Brigedia Jenerali Mstaafu Emmanuel Maganga amefariki dunia. Mhe. Maganga amefariki dunia wakati akipatiwa matibabu katika hospitali ya Milambo mkoani Tabora usiku wa kuamkia leo. Mkuu wa mkoa wa Tabora Dr. Philemon Sengati amethibitisha kifo hicho. Brigedia Jenerali Maganga alistaafu ukuu wa mkoa mwaka 2020 wakati wa maandalizi ya uchaguzi mkuu wa raisi, wadunge na madiwani

Chanzo: Millard Ayo

********
Brigedia Jenerali Mstaafu Maganga alilitumikia jeshi la wananchi wa Tanzania kwa muda wa miaka 37, akiwa kitengi cha ugakuzi wa Ulinzi jeshini (Defense Inspection Unit). Aliagwa rasmi pamoja na maafisa wenzake wa ngazi za juu mnamo tahere 04 Machi 2016 katika gwaride maalum lilioandaliwa katika kambi ya Jenerali Abdallah Twalipo, Temeke Dar Es Salaam. Aliteuliwa mwaka huo huo kuwa mkuu wa mkoa wa Kigoma.
 
Back
Top Bottom