AJIRA

AJIRA

Kodi ya nyumba =150,000/-
Chakula = 200,000/-
Usafiri/Nauli = 75,000
Umeme/Maji = 20,000
Kusomesha watoto = 250,000/-
Sadaka = 15,000/-
King'amuzi = 28,000/-
Vifurushi vya simu/Muda wa maongezi = 15,000/-
Perfumes/Sabuni/manukato = 25,000/-
Akiba = 22,000

Hapo hujanunua shati,suluali, Mkanda, Kiatu kizuri

Hujaombwa mchango na jamaa zako kwaajili ya harusi/kitchen part/kipaimara n.k

Vijana, ila kama hutakuwa na biashara binafsi sio rahisi kutoboa kwenye haya maisha 🙌
duuh! sasa mwenye matumizi kama hayo ni bachela au mtu na familia yake ?
 
Hivi kuna kitu gani behind ajira.? unakuta mtu analipwa 800k kwa mwezi lakini anamaisha magumu ndy nn sasa.?

Alie na ufafanuzi mzuri anieleweshe... si kwa miezi miwili tu hapo unakua na 1.6M × 10 miezi = 16M kwa mwaka😀
Kwani hiyo hesabu ya milioni 16 umeipataje we kijana?

Miezi 10x80,0000/= unapata milioni nane

Miezi 12 unapata milioni 9600000/=
Sasa tukisema huko shuleni ulienda na hakujakusaidia itakuwa ni kosa kweli?
 
Kwani hiyo hesabu ya milioni 16 umeipataje we kijana?

Miezi 10x80,0000/= unapata milioni nane

Miezi 12 unapata milioni 9600000/=
Sasa tukisema huko shuleni ulienda na hakujakusaidia itakuwa ni kosa kweli?
Nilikua wrong,, ahahahaha..
Nikichukua 2 miezi ambayo ni 1.6M nikazidisha na miezi kumi badala ya kujumlisha😀
 
duuh! sasa mwenye matumizi kama hayo ni bachela au mtu na familia yake ?
Kuna watu wana familia, na wanalipwa hayo malipo

Kuna wengine ni bachela na wanalipwa hicho kiasi pia

advantage ya asiye na familia, atakuwa na akiba nyingi kwani zaidi ya shilingi 250,000 niliyoi-address kama ada itatumika kwenye akiba
 
Kuna wengine ni bachela na wanalipwa hicho kiasi pia

advantage ya asiye na familia, atakuwa na akiba nyingi kwani zaidi ya shilingi 250,000 niliyoi-address kama ada itatumika kwenye akiba
sasa apo kwa bachela angeweza punguza matumizi, si anakuwa na matumizi sawa na mtu mwenye familia, mfano kulipia kodi atleast 50k kwa mwezi aweze jenga yake kabla majukumu mengine kuongezeka !
 
sasa apo kwa bachela angeweza punguza matumizi si anakuwa na matumizi sawa na mtu mwenye familia, mfano kulipia kodi atleast 50k kwa mwezi aweze jenga yake kabla majukumu mengine kuongezeka !
Kupanga ni kuchagua, ukiweza kujipanga vizuri unaweza kupata nafuu kidogo ukaweza hadi kufanya savings

Ukishindwa kujipanga, utajikuta miaka yote upo vile vile

Unanukia perfume ya laki 2, lakini ukipata shida hata ya laki 5 ni hadi upige simu ukope kwa wana
 
Back
Top Bottom