AJIRA

AJIRA

Kama mshahara wa 800,000 kwa mwezi unadai kwa mwaka mtu anakuwa na milioni 16 basi nikwambie hivi, ukiajiriwa hadi utavaa nguo zimetoboka makalioni.

Kwanza huo mshahara hujahesabu makato ya kodi, shirika la hifadhi ya jamii, bima, bodi ya mikopo kama alikopa, mchango wa uanachama chama cha wafanyakazi.

Bado hujatoa hela ya kula, nauli, pango la nyumba na matumizi mengine. Na kwa akili yako hii hata ukifanya biashara utakula mtaji. Maana ukiuza 200,000 kwa siku utakula yote kumbe wewe kwenye hayo mauzo faida yako ni 40,000 na bado kwenye hiyo faida ya 40k hujatoa expenses kama bills zote na kodi. Mwisho wa siku kwa mwezi unaweza kuta faida ghafi ni 800,000 ila wewe unatumbua zaidi ya 1,200,000 kwa mwezi. Mwaka unaisha duka lina mapengo.
Ni point sana,, ahahahaha suruali imetobika🤣
 
Huo mshahara ni Mzuri na mkubwa kwa vijijini. Ila mjini ni kasheshe

Labda usiwe na wategemezi, usitumie starehe yoyote na uwe na posho za kufanya mshahara wako utoshee future plans.

Mfano ukishaaanza ujenzi tu. Hicho ni kifungo na ukiingia mikopo ya bank. Mambo yananoga zaidi
 
Kipato kinavyo ongezeka na mahitaji yasiyo kuwa ya lazima uongezeka pia, mfano kulala hoteli ya milioni 10 kwa siku wakati unaweza ukalala chumba cha elfu 40 na ukabaki mtu yule yule.
 
Nilikua nikijiuliza sana,, hili swali ujue 800k kwa mwezi ni hela kabisa😀
Hiyo ni pesa ya kawaida sana kijana, lakini inafaa kwa mnao anza maisha.
Last year kijana wangu aliacha kazi sehem kwamba mshahara ni mdogo (700,0000) kwakweli nilimshangaa sana maana bado yupo nyumbani, anapata kilakitu hadi nauli ya kwenda na kurudi kazini
 
Hui mshahara ni Mzuri na mkubwa kwa vijijini. Ila mjini ni kasheshe

Labda usiwe na wategemezi, usitumie starehe yoyote na uwe na posho za kufanya mshahara wako utoshee future plans.

Mfano ukishaaanza ujenzi tu. Hicho ni kifungo na ukiingia mikopo ya bank. Mambo yananoga zaidi
Duuh!,, kwa mfano ukikopa bank afu ndy inakua umejichimbia shimo.?
 
Kipato kinavyo ongezeka na mahitaji yasiyo kuwa ya lazima uongezeka pia, mfano kulala hoteli ya milioni 10 kwa siku wakati unaweza ukalala chumba cha elfu 40 na ukabaki mtu yule yule.
Hii inacost. Unaongezewa mshahara na kuwa manager.

Ukitaka kuishi kimeneja. Ununue gari, upange nyumba mtaa mzuri , watoto wasome shule nzuri na wewe uende sehemu za starehe za class yako. Hapo ongezeko halitoonekana
 
Hiyo ni pesa ya kawaida sana kijana, lakini inafaa kwa mnao anza maisha.
Last year kijana wangu aliacha kazi sehem kwamba mshahara ni mdogo (700,0000) kwakweli nilimshangaa sana maana bado yupo nyumbani, anapata kilakitu hadi nauli ya kwenda na kurudi kazini
Sasa anamchongo,, upi sasa!
 
Kodi ya nyumba =150,000/-
Chakula = 200,000/-
Usafiri/Nauli = 75,000
Umeme/Maji = 20,000
Kusomesha watoto = 250,000/-
Sadaka = 15,000/-
King'amuzi = 28,000/-
Vifurushi vya simu/Muda wa maongezi = 15,000/-
Perfumes/Sabuni/manukato = 25,000/-
Akiba = 22,000

Hapo hujanunua shati,suluali, Mkanda, Kiatu kizuri

Hujaombwa mchango na jamaa zako kwaajili ya harusi/kitchen part/kipaimara n.k

Vijana, ila kama hutakuwa na biashara binafsi sio rahisi kutoboa kwenye haya maisha 🙌
 
Duuh!,, kwa mfano ukikopa bank afu ndy inakua umejichimbia shimo.?
Mikopo ya kununua gari la kutembelea au ukazike pesa kwenye ujenzi ambao haukuingizii pesa ya kurejesha mkopo ni ni tofauti na mkopo wa kukuza biashara tayari unaijua....
 
Hii inacost. Unaongezewa mshahara na kuwa manager.

Ukitaka kuishi kimeneja. Ununue gari, upange nyumba mtaa mzuri , watoto wasome shule nzuri na wewe uende sehemu za starehe za class yako. Hapo ongezeko halitoonekana
Manager angalau,, nahisi anapesa ndefu...
 
Kodi ya nyumba =150,000/-
Chakula = 200,000/-
Usafiri/Nauli = 75,000
Umeme/Maji = 20,000
Kusomesha watoto = 250,000/-
Sadaka = 15,000/-
King'amuzi = 28,000/-
Vifurushi vya simu/Muda wa maongezi = 15,000/-
Perfumes/Sabuni/manukato = 25,000/-
Akiba = 22,000

Hapo hujanunua shati,suluali, Mkanda, Kiatu kizuri

Hujaombwa mchango na jamaa zako kwaajili ya harusi/kitchen part/kipaimara n.k

Vijana, ila kama hutakuwa na biashara binafsi sio rahisi kutoboa kwenye haya maisha 🙌
Vp kama ndy unaanza maisha huna watoto...
 
Sasa anamchongo,, upi sasa!
Sihitaji mchango wake, maana majukumu yangu ya msingi nilisha maliza kumsomesha na nikamtafutia kazi.
Kwasasa sijamuuliza chochote zaidi najisemea moyoni ngoja apigwe jua afulie hadi aijue dunia, ingawa namuona anapambana kutafuta new job
 
Hiyo ni pesa ya kawaida sana kijana, lakini inafaa kwa mnao anza maisha.
Last year kijana wangu aliacha kazi sehem kwamba mshahara ni mdogo (700,0000) kwakweli nilimshangaa sana maana bado yupo nyumbani, anapata kilakitu hadi nauli ya kwenda na kurudi kazini
Unamshangaaje na umeshasema "anapata kila kitu hadi nauli" Mkuu

Huyo anafurahi kuwa tegemezi na pengine bado anahisi ana muda sana. Japo sikuwa tegemezi kama yeye lakini kuona nina muda wa kufanya mistake za kuchagua chagua ilinicost

Kwa hiyo mpe muda. Pengine ana ubavu wa kupata vya zaidi. So mpe moyo lakini mpe nafasi awe responsible pia 🙏🏽
 
Sihitaji mchango wake, maana majukumu yangu ya msingi nilisha maliza kumsomesha na nikamtafutia kazi.
Kwasasa sijamuuliza chochote zaidi najisemea moyoni ngoja apigwe jua afulie hadi aijue dunia, ingawa namuona anapambana kutafuta new job
Msikilize atakua,, na mindset ya biashara si unajua kadiri muda unavyosonga mawazo pia hubadilika...
 
Back
Top Bottom