Crashwise
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 22,227
- 8,760
Inavyoelekea, wanasubiri waraka kutoka Tengeru kwa mwenye mali!
utahangaika sana mama mchawi wa zitto ni yeye mwenyewe hakuna za waraka kutoka tengeru wala nini kuna ushahidi mpaka wa video..
Inavyoelekea, wanasubiri waraka kutoka Tengeru kwa mwenye mali!
Eti wanadai ule waraka alioukiri Kitila ni feki! Na kwamba baada ya kikao kijacho wakilazimika kuutoa ule orijino watafanya hivyo!
My take: chadema mtamfanya Zito aseme ambayo hakutaka kuyasema!itakula kwenu!
Kawachezea kwalipi? Yaleyaliyo semwa kwenye ule waraka msipofanyia kazi shauriyenu.
Zito hakatai kufukuzwa.yupo tayari.anacho kataa yeye kesho na keshokutwa cdm ikiwa vipande vipande asilaumiwe yeye.
Sory, nimeingia kwenye thread ya machizi.
TUNA M-MISS SANA J.K.NYERERE:
1. Idd Amini - Alipoivamia Tz.... Mwalimu alitamka tutampiga nduli!.. Na kweli Idd Amini alipigwa hadi akaikimbia Uganda.... 2. Kolimba - Alipotamka CCM imepoteza Dira na Mwelekeo... Mwalimu alimwita Dodoma akamuuliza nani kakutuma useme hivyo?!.. Ndio ukawa mwisho wa Kolimba!.. 3. Samweli Sitta - Alipokuwa kiongozi wa serikali ya wanafunzi UDSM aliongoza mgomo wa wanafunzi wenzake kudai siagi na maziwa!... Mwalimu aliibuka pale chuoni akamuuliza Samweli Samweli kwenu mnakunywa maziwa kweli?!.. Akamwambia lala chini, akamcharaza bakora na mgomo ukaishia hapo hapo!... 4. Abdul Jumbe! - Alipotaka serikali tatu!.. Nyerere alimuuliza moja kujumlisha moja ni ngapi?!.. Jumbe akajibu ni mbili!.. Nyerere akamwambia kama ni mbili mbona unataka serikali tatu?!.. Huo ndio ukawa mwisho wa Abdul Jumbe kuwa Rais wa Zanzibar!.. 5. John Samwel Malecela - Ni baada ya taarifa kuzagaa kuwa amebadili dini na jina ili apate kuungwa mkono na nchi za kiislamu kugombea Urais mwaka 1995!.. Nyerere alimwambia wee John wewe umeenda Arabuni mara moja umebadilisha jina sasa unaitwa Jumanne!. Ukienda mara ya pili si utabadilisha kabila?!... Huo ukawa mwisho wa ndoto zake kuwa Rais wa Tz !... 6. Edward Lowassa - Alipokodi ndege binafsi ikampeleka hadi dodoma kwenye vikao vya mchujo wa wagombea Urais kupitia CCM mwaka 1995 alimpa lift JK!.. Nyerere alimuuliza mmekuja na Ndege dodoma pesa mmetoa wapi?!.. Jina la Lowassa likakatwa kabla ya vikao vya mchujo!.. . Natamani Nyerere angekuwepo sasa na mwaka 2015!
Nimeichukua kule, nimeileta huku!
Kwa mujibu wao ni DR.SLAA, ingawa hata wao hawaamini kama Slaa anaweza kuwa Rais..
Eti wanadai ule waraka alioukiri Kitila ni feki! Na kwamba baada ya kikao kijacho wakilazimika kuutoa ule orijino watafanya hivyo!
My take: chadema mtamfanya Zito aseme ambayo hakutaka kuyasema!itakula kwenu!
Kadi ya kriniki ya wajawazito?au kadi gani?
Jamani,let's be realistics! Hivi chadema ni chama cha siasa au mradi wa siasa!?
Zitto akitimuliwa kesho yake chadema inakufa bila zito hakuna chadema.
Zitto atafanya ziara nchi nzima. Cdm KEISHNEY
Chadema wamepoteza mwelekeo.
Zitto hana ubavu wa kuchezea vichwa za maelefu ya Watanzania wanaokiunga mkono chadema. Sauti ya wengi ni sauti ya Mungu. Mtu mmoja hawezi kushindana na nguvu za Mungu.
Muambieni akome kabisa, na wala hatuogopi kumtimuwa.
Kwa mujibu wa Takwimu sahihi CCM imewahi kushinda uchaguzi mmoja tu wa 20005! Mwaka 1995 Lyatonga alishinda japokuwa nae alikuwa mole wa CCM! Mwaka 2000 Lipumba alishinda, Mwaka 2010 Dr Slaa alishinda kwa mbali... Maajabu Rais kutangazwa mshindi eti kwa kura chini ya milioni 5! ...IGP kaona mbali ndiyo maana anaachia ngazi mapema kabla ya 2015 mliyomlazimishia...Ingekuwa hivyo mngeshinda uchaguzi.
CHADEMA imejaa mambumbumbu! haiwezekani mtu kama Lema ambaye ufahamu wake una walakini awe na maamuzi makubwa hivyo kwenye Chama! huu ni ubatili!
Kama Zitto hana Ubavu kwanini wanakuwa waoga kuitisha Uchaguzi.
Chadema ni ma mafia wa ukweli! Bora zito asijitoe kwa usalama wake, wanaweza kum chacha wangwe!