Ahmed Rajab: Laana iliyoipiga CHADEMA

Ahmed Rajab: Laana iliyoipiga CHADEMA

Rajab namheshimu sana kama great thinker wa kweli ila kwa hili sikubaliani naye kabisa, na haya ni maoni yangu kama alivyoyatoa yeye. Ninaamini katika demokrasia na ninafahamu nini maana ya demokrasia, lakini ninaona sio mara zote unaachia demokrasi kama kiongozi na kiongozi aliye bora ni lazima aangalie mazingira yakoje na kundi la watu wake likoje kabla ya kuachia demokrasia kutamalaki.
Tunasoma katika historia juu ya akina Stalin, akina Mao, akina Mousolin na tuliaminishwa kuwa walikuwa madikteta lakini mazingira ya wakati ule ya ushindani wa kisiasa na kiuchumi kati ya mataifa yalilazimu viongozi wawe hivyo kwani ilikuwa rahisi tu kuhujumiwa na taifa lingine kwa maslahi ya kiuchumi - hasa utafutaji wa rasilimali za dunia. Leo hi ukiziangalia China, Urusi zimeweza kujinasua katika ubabe wa MArekani kwa sababu ya kuhakikisha hawaachii demokrasia kiholela ambayo ingemuwezesha MArekani kupenyeza mamluki wake ambao wangetumika kuhujumu jitihada za Warusi na Wachina kusonga mbele kimaendeleo na hivyo kukwaza ushindani wa mataifa hayo kwa Marekani. NA sasa China imeanza kuachia demokrasia kidogo kidogo baada ya kuona mahali walipofikia kimaemdeleo MArekani haiwezi kuwa kitisho tena.
Kwa maana hiyo ninaona na uongozi wa CHADEMA unafuata mfano huo wa viongozi waanzilishi wa mataifa haya makubwa sasa. PAsipo kufanya hivyo kwa kipindi hiki cha mpito CCM mpinzani mkubwa wa CHADEMA ambayo haitapenda kuona Chadema ikisimama na kutoa upinzani wenye nguvu na kukipokonya madaraka ya kuongoza nchi. Chadema wakiachilia kiholela demokrasia wanaweza kujikuta wana mapandikizi wa CCM kama ilivyokuwa NCCR na hatimaye ikafa kama vinywa vya viongozi fulani wa CCM walivyokuwa wanajigamba kuwa Chadema ingekufa kabla ya 2014.
Tunaamini kuwa ili Chadema ikue na kufikia hatua ya kuiondoa madarkani CCM ni lazima kuachia demokrasia kidogo kidogo kwa kuwachunguza vilivyo wote wanaoutaka uongozi. Kwanini CCM ndio ipige kelele sana juu ya demokrasia ndani ya Chadema, wakati kwao hakuna demokrasia kama tulivyotegemea kwani tunaambiwa Uenyekiti ndani ya chama hiki hauogombaniwui na ye yote na hii ilimgharimu Shibuda wakati fulani - nadhani hapa Shibuda anaweza kutukumbusha yaliyomkuta alipoonyesha nia ya kugombea uenyekiti wa chama kitaifa.
Chadema mwendo ni huo huo watoto wa mjini wanasema ''mdogo mdogo''. Itakapofika wakati muafaka achieni demokrasia itamalki ndani ya Chama lakini kwa sasa ni lazima muwe makini sana.
Mkuu Mkuruka,hii nd'o nilitaka niitumie kumjibu kitila mkumbo na pumba zake kwenye ya magazeti ya kila wiki.Tatizo walilonalo mashabiki wa akina Zitto ni kuwa huwezi kuachia demokrasia kwenye vyama kwenye nchi ambayo chama kilicho madarakani serikali yake ipo tayari kuwanunua wapinzani kwa kiasi kikubwa cha pesa ili kuwavuruga,utaratibu wa Chadema nimeupenda sana na nd'o maana nawasupport waweze kuingia madarakani kwasababu wameonyesha wanaweza.Tatizo moja dogo ninaloliona wapunguze makanjanja wa kichaga kwenye nafasi wasizozistahili hapo makao makuu.
 
Mkuu Mkuruka,hii nd'o nilitaka niitumie kumjibu kitila mkumbo na pumba zake kwenye ya magazeti ya kila wiki.Tatizo walilonalo mashabiki wa akina Zitto ni kuwa huwezi kuachia demokrasia kwenye vyama kwenye nchi ambayo chama kilicho madarakani serikali yake ipo tayari kuwanunua wapinzani kwa kiasi kikubwa cha pesa ili kuwavuruga,utaratibu wa Chadema nimeupenda sana na nd'o maana nawasupport waweze kuingia madarakani kwasababu wameonyesha wanaweza.Tatizo moja dogo ninaloliona wapunguze makanjanja wa kichaga kwenye nafasi wasizozistahili hapo makao makuu.

Sasa kama hao wanachama wananunulika kirahisi hivyo kweli mna haja ya kuwa nao?

Amandla.....
 
Njemba imeshakula ubwabwa wa MACCM basi ikaamua kuandika pumba zake, nasikia iko safarini kuwahi ubwabwa mwingine Zenj kusherehekea miaka 50 ya mapinduzi ikishapata ubwabwa za Zenj itaandika article nyingine kuhusu CHADEMA na Zenj. Mtu mzima hovyoooooooo!!!! Mxyuuuuuuuuuuuuuu
Wewe jamaa kila mtu akitoa rai yake kuikosoa Chadema kwako katumwa.
 
Wewe jamaa kila mtu akitoa rai yake kuikosoa Chadema kwako katumwa.

watu wanaamini kuwa chadema ipo perfect haistahili kukosolewa.
Wanataka kila thread isifie chadema tuu.
 
Hata huko kijijini kwao hakuna kituo cha afya, hakuna madawati wanafunzi darasani wanakaa chini na leo kwasababu umeshiba umewasahau hata wazazi na ndg zako waonapigika huko kijijini.
 
hakuna kundi, mikakati ni kawaida kuwa na makundi....it happens naturally.

kama uwezo wako wa kufikiri na reference unaleta ya yule diktetta Nyerere aliyekuwa hana demokrasia

nakupa pole kubwa sana

so una copy na ku paste toka kwa Nyerere??

huna hoja, umeishiwa na wewe ni wa kugopwa kama ukoma

from now onwards, sikuchukuliaa kama senior bali kama senior mjinga kabisa kupata kuonekana ndani ya JF............

Reference ni Nyerere?? aliyekuwa anapigiwa kura za mtu na kivuli?? mpaka leo CCM HAMNA DEMOKRASIA yet kwa akili zako unataka chadema kiwe kama ccm...what a joke..

what does that makes you??

so dissapointed na mfano wa Nyerere, I would have slapped you

Mbona unatokwa povu?
Nyerere alifanikiwa kujenga chama imara kilichowaunganisha Watanzania wote mpaka pale kilipotekwa na mafisadi. Nyerere asingestahmili watu mfano wa Zitto na Kitila ndani ya chama. Ni mfano wa kuigwa. Endelea kutokwa povu!
 
Ccm wanalalama tu kama mbwa kapigwa jiwe la mguu. Mtalialia sana safari hii,CDM siyo cuf au nccr mliowageuza misukule yenu.
 
Neno Demokrasia sasa limebeba maana nyingi zaidi ya idadi ya watanzania, tuseme kama watunzi wa sheria wangetunga sheria ya Demokrasia basi zingetolewa maana na tafsiri nyingi za neno demokrasia kiasi ambacho mawakili wangekuja na utetezi lukuki ktk kuitafsiri Demokrasia. Sitaki kuamini kwamba watu hawajui nini maana ya Demokrasia! Ila nataka niamini demokrasia maana yake ni vile wewe unavyotaka iwe kwa maana Mwizi atasema si Demokrasia kuweka mageti na walinzi makini ktk nyumba maana wanatufanya tushindwe kuiba na hivyo hapo hakuna demokrasia. Ahmed Rajab ktk andishi lake la Laana iliyoipiga CHADEMA amechagua maana hii! ya mwizi akizuiwa kuiba basi aseme hapo hakuna Demokrasia! Ukweli hauji kuwa UONGO na kujifanya wajinga hakufanyi UKWELI kuwa UONGO tuache unafiki unatuondolea utu wetu.
 
  • Thanks
Reactions: WCM
Njemba imeshakula ubwabwa wa MACCM basi ikaamua kuandika pumba zake, nasikia iko safarini kuwahi ubwabwa mwingine Zenj kusherehekea miaka 50 ya mapinduzi ikishapata ubwabwa za Zenj itaandika article nyingine kuhusu CHADEMA na Zenj. Mtu mzima hovyoooooooo!!!! Mxyuuuuuuuuuuuuuu

Hivi kila anayeikosoa CDM au anayetoa mtazamo tofauti dhidi ya maamuzi ya CDM amenunuliwa na CCM au msaliti? This thinking antithetically epitomizes the lack of democracy within CDM. Yaani kifupi ukiwa na mawazo tofauti ndani ya CDM wewe ni msaliti na hufai kuwa ndani ya chama.

Duh!
 
Rajabu unachofanya ni spring doctor kwa kutuaminisha unataja madhambi ya ccm kwa kuchambua cdm kwa mtazamo wa kihafidhina.unafanya fallacy inayoitwa beg for the question
 
Mbona unatokwa povu?
Nyerere alifanikiwa kujenga chama imara kilichowaunganisha Watanzania wote mpaka pale kilipotekwa na mafisadi. Nyerere asingestahmili watu mfano wa Zitto na Kitila ndani ya chama. Ni mfano wa kuigwa. Endelea kutokwa povu!

Kwa hiyo tatizo lako si udikteta bali ni Zitto? Basi mngetundea haki kama hata jina la chama lingebadilishwa ku-reflect hilo. Chama cha uDikteta na Maendeleo? CHADIMA.

Amandla......
 

Uandishi wa kutoka upenuni kuhusu masuala ya mwandani? Anyway kwa Mzanzibari kutoiunga mkono CHADEMA si ajabu
 
Mbona unatokwa povu?
Nyerere alifanikiwa kujenga chama imara kilichowaunganisha Watanzania wote mpaka pale kilipotekwa na mafisadi. Nyerere asingestahmili watu mfano wa Zitto na Kitila ndani ya chama. Ni mfano wa kuigwa. Endelea kutokwa povu!
Mbona Nyerere kaishi na mafisadi wengi tena mwingine aliwapigia kampeni kuwa rais Mkapa?
 
Huyu mzee ni mtu huru kimawazo kabisa,kila anayeleta ukweli mnasema lumumba,badilikeni hata kama mnaipenda chadema,mbona sie wengine hatuipendi ccm,na bado tunasema mbowe na dr slaa ni wa kuogopwa,hawafai kwa namna yeyote ile na sababu mara kibao tunazitoa,jengeni demokrasia tuikomboe nchi yetu,vinginevyo ccm itatoka lakin cdm kitakuwa kibaya kuliko ccm,ipo cku.
Jk aliomfunga Babu Seya sababu ya malaya anafaa.
 
Back
Top Bottom