A failed assassination plot against Dr. Ulimboka...

A failed assassination plot against Dr. Ulimboka...


Hivyo hivyo ulivyoona, kuwa migomo ni miongoni mwa harakati za mwisho kabisa katika kudai kudai haki pale njia za awali zinapokuwa zimeshindikana. Sasa inabidi uangalie kama njia za awali zilikuwa zimeshindika kwa hao madaktari wako.
 
Asubiri akifa atapewa nafasi ya kwenda kutoa pole na rambirambi kama kawaida yake!
 
Inawezekana kabisa kupigwa kwa Dr. Ulimboka ikawa inatoka kwa vigogo wa wizara ya Afya waliong'olewa ambao amewakatiza ulaji na wengine wako njiani kufikishwa mahakamani.
 
Na limeshaanza kuwa, PINDA "We have marked your words!"
 
Lakini kwani kwa mgomo huu wa pili wanapoteza nini kama tayari walishapoteza madaraka yao.
kwa mtizamo wangu naona walioko madarakani ndio waliotenda wakiogopa kupoteza madaraka.

Eh mungu mrudishie afya yake huyu kijana..
Na laana iwaendee wale wote waliohusika kupanga na kutenda hicho kitendo!

Mkuu kisasi cha kumwagiwa unga huwa hakiishi. Utamsaka tu mbaya wako siku zote.
 
Mother theresa na mwenzake nighngale wakifufuka leo hii WATAKUFA KWA KIHORO...
>swtlj...binadamu angekua anatosheka na pesa wale mafisadi wangeshatosheka.
>wewe unaesema nitoe taarifa polise,ALIEKWAMBIA POLISI NI MALAIKA NI NANI?WEWE MWENYEWE SI AJABU NI DAKTARI NA UNAFANYA MAMBO HAYO KAMA KAWA.
 
Mother theresa na mwenzake nighngale wakifufuka leo hii WATAKUFA KWA KIHORO...
>swtlj...binadamu angekua anatosheka na pesa wale mafisadi wangeshatosheka.
>wewe unaesema nitoe taarifa polise,ALIEKWAMBIA POLISI NI MALAIKA NI NANI?WEWE MWENYEWE SI AJABU NI DAKTARI NA UNAFANYA MAMBO HAYO KAMA KAWA.
 
Mkuu umeongea ukweli mtupu,
kuna vibaraka wanajaribu kupotosha watu kwa kuitetea serikali uaji ya wanyonge,
sasa kila mtu anaenda anaelewa kwamba serikali yetu ni adui yetu.

Unajua Serikali pia inaweza kutumia mbinu ya hovyo kutimiza malengo yake ili iwachanganye watu. Yaani watu watasema haiwezekani serikali kufanya hivi. Sasa kuna mwalimu mmoja wa sekondari alinipigia stori kuhusu waalimu wanaowatongoza wanafunzi wa kike. Unajua wanafanyaje? Ili mtu asiwashuku huwa wanaongeana mwananfunzi mwenyewe katika mazingira ya wazi ambako wanaonekana sio kwa kujificha ficha. Katika hali ya kawaida mtu atasema ah, haiwezekanai mwalimu yule anamtongoza yule msichana hadharani, kumbe actuuly ndio anatongoza vizuri tu! Ndivyo navyoliona pia kwa upande wa serikali inawezakan ilituma wauaji wale wasifanye hilo jambo kitaalam sana ili ionekane ni wahuni tu walifanya hivo na sio serikali. Unaonae ingefanyika more professionally pia pia serikali ingewajibika zaidi. Serikali haiwezi kukwepa lawama kila upande unaibana>
 
Hakuna phrase inayoniudhi kama hii ambayo hutumiwa sana na vijakazi wa Dhaifu kuwa " hakushauriwa vizuri" ! Yaani huyu kila siku anaongopewa na hashauriwi vizuri yeye tuu ? Either inadhiirisha hii kazi haiwezi au yy na hao washauri ni wachovu, which means Mnyika was right on the money !!

Hizi ndiyo elimu za uchumi wa Mwigulu : Mimi sina digirii lkn sihitaji ushauri kama nikiwa kiongozi kujua kuwa kwa hali yetu ya umatonya hatuhitaji baraza la mawaziri kubwa, hatuitaji posho za vitafunwa ktk wizara wakati wataalam wetu, waalimu na hata wananchi wa vijijini wapo hoi. Pia sihitaji kwenda kutembelea wizara na kuwatoa watu kazini, na ningepiga marufuku hao wafanyakazi kununuliwa vibendera na/au kusikia wametumbua mamisosi baada ya ziara ! Wala huhitaji digirii kujua kuwa safari za nje zisizona tija sio kazi yangu rais (ndo maana kuna waziri wa nje) na nisingekubali kukutana na watu wa nje hovyo-hovyo (ikulu imekuwa kama uwanja wa saba saba). Yaani hata Chamelion akija bongo lazima atinge ikulu ??? !!

Ninge-mbana sana PM kuhakikisha anasimamia vizuri na kwa karibu cabinet na ningechagua PM ambaye sio mtu wa kulia lia, bora niwe na PM ambaye anachukua action ASAP na anaweza kutetea maamuzi yake kwangu. Ningewakomesha mawaziri kwa kuwapangia ratiba za kuwa mikoani na vijijini angalau mara moja kwa mwezi, na kutoa taarifa ya mandishi kwa PM ambaye angetakiwa ku-compile report na kuja kwangu kuijadili mara moja kwa mwezi.

Ningepanga ratiba za kushtukiza mara kwa mara ktk sehemu mbalimbali nchini (amiri jeshi mkuu uwezo anao) na mwisho nisingeuwa mtu wa kucheka cheka ovyo hata visivyochekesha !


Jamani naona watu mmecharge kama mafahali wawili ndani ya zizi! Ni vizuri kuwa na tahadhari kumhusisha Rais na kutekwa kwa Dr. Yes uongozi wake una matatizo lakini kumhusisha na hili jambo tunakwenda mbali. Kikwete si mtu wa visasi vya namna hii. Ana njia nyingi tu kama angetaka za kumdhibiti Dr. na asingekuwa na haja ya kutumia njia ya aibu namna ile.

Mtu anayesababisha shida ya madaktari ni waziri mkuu. Ameshidwa kumshauri rais ipasavyo kwenye jambo hili.
 
Leo nimeyakumbuka maandiko matakatifu ya Yesu,kwa kweli imeniuma sana hasa nikikumbuka kuzaliwa,kusalitiwa,kuteswa na kuuwawa kwa Yesu kristo.Wengi tungependa Yesu aonekane waziwazi lakini haijatokea na limekuwa suala la kiimani zaidi ya kwamba Yesu atarudi tena kwa ajili ya ukombozi na ufufuo....!Kuteswa kwa Yesu ilikuwa ni mpango wa Mungu kwa ajili ya Ukombozi kwa wanadamu.Kama mtume MUHAMAD,Yesu alijitoa maisha yake kwa ajili ya wengine na siku anasulubiwa aliamua kushangaa kiasi cha mateso alichokipata hadi akaamua kuuliza "Ikiwa mti mbichi watendwa hivi vipi kwa mti mkavu?",Na ilifika wakati Yesu alihisi amesaulika na mwenyezi mungu,akaamua kuuliza "Heroi heroi Rama sabakitani...Yaani mungu wangu mbona umeniacha?"Siwezi kuyalinganisha maisha ya Dokta Ulimboka na maisha ya Yesu ua Mtume Muhamad,lakini nafsini naguswa kufanya hivyo hasa kwa haya anayoyapitia Mr.Ulimboka.Yesu kabla ya kukata roho alisema "YAMETIMIA" lakini Dr.Ulimboka ameshindwa kufanya hivyo kwa kuwa siku yake haijafika,Au mungu anasubiri Dokta Ulimboka amalize kuifanya kazi yake ndipo aseme yametimia?Au Dokta amekataa kunywa kikombe hiki peke yake?Ikiwa kijana Ulimboka ambae ni mtanzania ametendwa hivi vipi kwa wasio watanzania?au vipi kwa wasio watumishi wa serikali?
 
Naomba nieleweshwe hawa jamaa wa usalama kwa kawaida wanafundishwa na kutumwa hata kuua. Je kuna uhalali wowote wa kisheria (achilia mbali maadili yanayopingana na uuaji) kwa serkali kufanya hivi? Je serkali inaweza kushtakiwa wapi kama inaonekana kudhuru raia??
 
If they wanted him DEAD, he'd be dead by now, na mngekuwa mnaongea mambo mengine kabisa.......probably, they still need him for something..........the big question is wat is it??

and kimtazamo wangu, 1st, wat has bin done to him isnt fair, Unless, he(ulimboka) framed it....najua kwa hili, wengi mtanilaumu, but mkisoma stories nyingi kama hizi, mtaona, ulimboka hatokuwa wa kwanza, kufake something like this, but FOR GOOD REASONS..............cause, seriously, kama wangetaka afe, angekufa longtym........

2dnly, killing one person for the benefit of two or more people, i find it reasonable................
Usiseme hivyo mana waliofanya ni wanadamu na wewe ni mwanadamu pia na katika kutaka kuua sio lazima mtu afe. Kwani hajawahi kusikia mtu wamepanga kumuua na hata baadaye daktari ana-certify death lakini mwisho wa siku anakuja kuzinduka au saa ingine anazindukia chumba cha kuhifadhia maiti. Yote ya Mungu kuna ushuhuda pia katika watu wake wa Tanzania katika hii serikali.
 
Hebu jiulize ni kiasi gani hutumika kwa ubadhirifu tz.juzi tu umesikia bilioni zaidi ya 300 uswisi.tatizo sio hela ni usimamizi mbovu na matumizi yasiyofaa.Na si kweli kwamba madai yao ni mshahara,waulize watakuambia mshahara ni dogo tu hata kwa uzalendo wangeweza kusamehe kama serikali ingekuwa sikivu kama inavyoijisifu.

Kutoka kwenye pesa zinazoibiwa na mafisadi wa ccm kama dola bil 300 zilizoko uswiss.

Haya ndio majibu marahisi niliyoyasemea.
 
tusisukumwe na hisia juu ya kipigo cha dr.ulimboka and eventually reaching to a sanctity statement that the government has afrontly commited a crime to dr.ulimboka without making critical analyisis about event.


Yawezekana kabisa serikali kushiriki katika tukio hilo haramu ili kuzima nguvu ya kiongozi huyo katika kuongoza migomo ya madaktari hao.lakin swali la kujiuliza ni kwamba ni serikali gani iso na akili ikafanya uovu huo dhahiri? Kwani serikali imeashiwa mbinu za kum abduct mtu? Evi mara ngapi tumesikia fulani amepotea,amekfa katika mazingira tatanishi?


Pia,yawezekana watu wasioitakia serikali kuhusika tukio ili kudhihirisha udhaufu wake nahivyo kujiimarisha kisiasa ama kikanda na hatimaye kuchukuwa nchi 2015 kama inavyondotewa.kwa mfano ikumbukwe ter.12,january,2011 kipo chama kilisema wazi kuwa,kitahakikish kinatumia kila aina yavitimbi ili kuhakikisha nchi haitawaliki.je chama hicho hakiwezi kuwaziwa kwa tukio hili kama ni mbinu kutekeleza mkakati?



Aidha,migomo ya madaktari ilisababisha baadhi ya mawaziri kutupwa nje pale raisi alipotengua baraza na kuunda lingine.je hamuoni ka hawa wanaweza kufanya hivyo kwa aidha kulipiza kisasi au kumkomoa rais kwa kuwatupa nje?


Vilevile ifahamike kuwa,migomo ya madakatari inasababisha vifo vya watu waso na hatia.je hamuwezi kuona kuwa hizi ni hasira za wananchi wanaopoteza ndugu zao kwa migomo ya madaktari?


Lakini pia,juzi tu tumeshuhudia askofu mmoja akitamka kuwa,ccm ijiandae kuaga ikulu mwaka 2015.je hamuwezi kuona kuwa,haya ni maandalizi ya kufikia lengo hilo la askofu hoyo?


Mwisho napenda kusema kuwa, tusiharakie kuishtumu serikali kuhusika na tukio hilo bali tuachie tume kufanya uchunguzi kwani mchawi atapatikana tu.


Naomba kuwasilisha wanajamii






Hata huyu angekufa ingekuwa katika mazingira ya kutatanisha sema Mungu ameamua kuuonyesha uovu wa Serikali hadharani.Hili la swala la vyama oooh mara chama kimoja kitafanya nchi isitawalike!!!!!oooh maneno kibao unataka kupoteza ukweli(hali halisi)?Hii Serikali ni dhaifu,ni sawa na mtu alieishiwa hoja akaanza kutukana na sasa Serikali nayo ineamua kuua(imeishiwa hoja).
 
tusisukumwe na hisia juu ya kipigo cha dr.ulimboka and eventually reaching to a sanctity statement that the government has afrontly commited a crime to dr.ulimboka without making critical analyisis about event.


Yawezekana kabisa serikali kushiriki katika tukio hilo haramu ili kuzima nguvu ya kiongozi huyo katika kuongoza migomo ya madaktari hao.lakin swali la kujiuliza ni kwamba ni serikali gani iso na akili ikafanya uovu huo dhahiri? Kwani serikali imeashiwa mbinu za kum abduct mtu? Evi mara ngapi tumesikia fulani amepotea,amekfa katika mazingira tatanishi?


Pia,yawezekana watu wasioitakia serikali kuhusika tukio ili kudhihirisha udhaufu wake nahivyo kujiimarisha kisiasa ama kikanda na hatimaye kuchukuwa nchi 2015 kama inavyondotewa.kwa mfano ikumbukwe ter.12,january,2011 kipo chama kilisema wazi kuwa,kitahakikish kinatumia kila aina yavitimbi ili kuhakikisha nchi haitawaliki.je chama hicho hakiwezi kuwaziwa kwa tukio hili kama ni mbinu kutekeleza mkakati?



Aidha,migomo ya madaktari ilisababisha baadhi ya mawaziri kutupwa nje pale raisi alipotengua baraza na kuunda lingine.je hamuoni ka hawa wanaweza kufanya hivyo kwa aidha kulipiza kisasi au kumkomoa rais kwa kuwatupa nje?


Vilevile ifahamike kuwa,migomo ya madakatari inasababisha vifo vya watu waso na hatia.je hamuwezi kuona kuwa hizi ni hasira za wananchi wanaopoteza ndugu zao kwa migomo ya madaktari?


Lakini pia,juzi tu tumeshuhudia askofu mmoja akitamka kuwa,ccm ijiandae kuaga ikulu mwaka 2015.je hamuwezi kuona kuwa,haya ni maandalizi ya kufikia lengo hilo la askofu hoyo?


Mwisho napenda kusema kuwa, tusiharakie kuishtumu serikali kuhusika na tukio hilo bali tuachie tume kufanya uchunguzi kwani mchawi atapatikana tu.


Naomba kuwasilisha wanajamii







naona mkuu unajitahidi kutufanya sisi ni wajinga wenzio humu jamvini.
 
Kwa kazi zinazoonekana kufanywa na unaoitwa usalama wa taifa, je ni kweli ni usalama wa taifa au wa CCM?
Majibu wadau.
 
Kwani we hujui kwamba usalama wa Taifa ulivunjwa 1076. Hamna, inabidi usukwe upya. Ukiona mtu anafikia kupeleka mswada wa FIU bungeni, huku tuna TAKAkuru, wakati hizi zinatakiwa kuwa udara tu ndani ya TISS ujue kuna matatizo makubwa sana. Huu ni usalama wa watawala.
 
Hiyo Taasisi inanuka, inahitaji kusafishwa siku nyingi sana.
 
Back
Top Bottom