Awali ya yote yatupasa kumpa pole na kumuombea apone haraka dakatari wetu huyu bwana Ulimboka na walaaniwe kwa nguvu zote wale wote waliohusika kwa namna moja ama nyingine.
Wengi wetu kwa asilimia kubwa tumekuwa na imani kuwa, utekelezaji wa jambo hilo ni njama au mkakati wa serikali kupunguza kasi ya harakati za madaktari katika kudai haki zao.
Tunapoihusisha moja kwa moja serikali kwa upande mmoja wa mbele, hebu tugeuke nyuma na kuangalia upande wa pili.
Bila shaka Dk Ulimboka alikuwa na maadui wa hatari wenye chuki binafsi naye hasa kipindi cha vugu vugu hili la migomo ya madaktari. Kuna watu waliopoteza madaraka yao matamu kutokana na kadhia hii, upo uwezekano wa kupanga njama za kulipiza kisasi.
Kutumika polisi si kitu mbele ya pesa. Ukiwa na fungu la kutosha ukitaka kuwatumia polisi njaa kwa ajili ya uhalifu unawatumia bila shida. Ikiwa wapo ambao hufanya ujambazi na kupora mali za watu, itakuwa hawa wa kukodiwa! Tugawanye fikra na mitazamo yetu, wakati tunaitupia jicho la mashaka serikali.
Tuangalie na upande wa pili, wale waliomwaga unga kutokana na harakati hizi tunawachukuliaje? Hapa mhalifu halisi anaweza kujificha chini ya kivuli cha serikali.
Mwisho napenda niwapongeza madaktari wote waliotoa kichapo kwa mtu anayedhaniwa kuwa alikuwa mmoja wa wateka nyara.
Mungu msaidie Dk Ulimboka apone haraka ili aendelee na harakati zake.