A failed assassination plot against Dr. Ulimboka...

A failed assassination plot against Dr. Ulimboka...

Pole kweli wewe, hivi unawezaje kumuhudumia mgonjwa mahututi wakati huohuo unamwambia kalete Groves,

kwa huko vijijini mama mzizi anaambiwa njoo na na mafuta ya taa ya kuchemshia maji, kuwasha taa, groves na maji yake.

hii kazi ni ngumu sana na ni hatari pia (naamini unanielewa )
Hapo unaudanganya Umma nani kakwambia MaMedical Assistant bba Manesi wamegoma huku kwetu wanachapa kz tofautisha MaDoctor na Nurse mpaka N/Auxillary ni wazalendo hasa ambao wanajua uchungu wa kifo si km hao vijana ambao wako zaidi kisiasa wanataka 3.5m tena wapo huko kwenu Muhimbili
Kwiaha yataisha na Liwalo na liwe nyongeza hiyo hakuna na isitoke
Lkn Dr Uli ugua pole
 
Itabaki siri kama ilivyokuwa kwa EDWARD MOLINGE SOKOINE, IMRAN KOMBE au MZEE JWANI MWAIKYUSA.
Pia tutasahau kama wale walimrisha sumu MWAKYEMBE.!!
 
Hii hatari sana maana nchi yetu ni ya amani lakini kuna matukio huwa yanatokea ukiyaangalia yanatia kichefuchefu, hii yote ni kutokana na nchi yetu bado watu wake wengi si waumini wa kutofautiana hoja ndio maana hata katika maisha yetu ya kwaida huwa mtu akiwa mbishi sana kwenye jamii huwa anachukuliwa kama adui badala ya kumkusanyia vielelezo ili aache kubisha vivyo hivyo kwenye serikali yetu nako ni yaleyale mtu anafanya kosa ambalo linaleta madhara kwa taifa akiambiwa wakati na yeye anajua amefanya kosa anawaona wale waliogundua uovu kama ni maadui. Kiukweli tumeshuhudia mashaidi wa kesi mbalimbali wanakufa katika mazingira ya utata wakati kesi zipo katika hatua ngumu na huwezi sema wameuliwa kwa kuwa hakuna ushahidi. Hii ni sawa na Kubenea alivyomwagiwa tindikali kutokana na kusema ukweli


Unakosea kusema nchi hii ni ya amani-LA!!!! ni nchi ya utulivu unaotokana na kukandamizwa na kunyimwa uhuru wa kutamka, tukawa waoga, uoga siyo amani kama ulivyo utulivu. Sasa ndo mwanzo wa kujenga amani-kumbuka amani haiji mpaka watu wachafuane ili wapate kuheshimika-hapo ndo amani inakuwepo nchini. Tukae mkao wa kula-wachache wetu lazima wawe mbuzi wa kafara ili watakaobaki na vizazi vijavyo wawe na amani ya kweli inayotokana na kuheshimiana na kuthaminiana
 
huyu alitambikia kuhani na kuona wagonjwa ndo dawa zake zifanye kazi si mnajua hata Kubenea alimtembelea alipounguzwa macho kwa tindikali. huyu ni bonge la mafioso.hivi anajiuliza ni kwa nini killing plot imeshindwa na huyu kiumbe bado anpumua?
 
Jamani naomba anayejua hali ya kamanda wetu Dr. Ulimboka atujuze anaendeleaje.
Samahani kwa kuwasumbua
 
huu ndo udhaifu wa jk, sikuzote mtu dhaifu huombea adui wake afe ili asiwe outsmarted
 
Yawezekana pia kuwa ili kuficha kuhusika kwa serikali katika utekelezaji wa mpango husika walikusudia kuufanya jinsi ulivyotokea ili watu wenye upeo wa kati na wa juu wafikiri kuwa serikali na wataalamu wake wa fani ya intelijensia hawawezi kufanya makosa ya kizembe kihivyo kumbe ni wao
Mazingira na mpango wa tukio haukutekelezwa kitaalamu kwa kiwango cha wale wenye kazi hiyo unaofikiria wewe. Lazima tutizame pande zote kwani mpango na njama yenyewe haikufanywa kitaalamu. Tunakumbuka wengi waliokufa katika mazingira tata mfano Kolimba, Katabalo nk. Inaonekana waliofanya tukio hili hawana uzoefu unaomaanisha wewe.
 
Wewe wapi kisukali/kisukari? sasa mtu amechukuliwa na polisi halafu unataka taarifa apelekewe polisi? alitafutwa mtu wa msaada wa kisheria na Dr.Helen Kijo Bisimba ndiyo alikuwa mtu sahihi na ndiyo maana yeye alianza kwa kutoa taarifa vituo vyote ili polisi waseme wamempeleka wapi. Duuh kweli wewe KISUKALI

Sidhani kama mpaka Dakika hii wewe na Kijosimba Mna ushahidi kuwa Polisi wamehusika. Hili Tukio ni kubwa, Baya na la Kusikitisha sasa Watu wasije na Mtandao wao wa kutaka Umaarufu kwa Gharama ya Wengine! au na wewe ni Kinyamana Eboo!!
 
Tumshukuru Mungu kwa taarifa hiyo ya maendeleo ya afya ya daktari na tuendelee kumwomba amponye. Mungu turehemu watanzania tunakoenda siko!
 
Mkuu umenena maisha magumu ni kwa kila Mtanzania...kila taaluma ina umuhimu wake.Watanzania wote tuwalaani madaktari kwa kitendo chao cha kinyama

muache kuilaani serikali, mnalaani madr. sijui akili za watu ziko wapi!
 
I dont want to believe what I am hearing about the current status of Dr. Ulimboka's Healthy!! Is he still alive???
 
Utasikia kujikosha anajidai serikali itagharamia matibabu yake apelekwe India..... hiyo ni baada ya kuona huyo bwana hakufa..... Madaktari kataeni asimwone... kwanza kwa hali yake hatakiwi kuonana na watu...wanaweza kumsababishia ugonjwa zaidi.

Very well said. Kwanini asiende kuona hao watanzania wanaokufa kwakukosa huduma bora kila siku? Yaani huyu mtu si mtu ni mnyama kabisa. He is just going there to try to clear his image kwa Wadanganyika. Mambo yakina Mwakyembe hayo... alafu atakuja kusema madaktari wanagoma alafu wakiumwa wao wanapelekwa India... Be ware!
 
Picha nzima ya suala la Dr. Ulimboka, haijakaa Ki-James Bond, ndiyo maana mimi nachelea kusema kuwa huyu jamaa kaadhibiwa na mkono wa serikali 'Professionals' kama wangekuwa wao wangemfanyia kitua mbaya ambayo asingeweza kuisimulia!

Hii kitu bila kuingilia kazi ya Polisi inaelekea imefanywa na 'Thugs' kwasababu haikufanywa na watu ambao hizo ndiyo kazi zao wengeweza kuifanya hiyo bila kuacha foot prints aina yeyote. kwahiyo tazameni upande mwingine pia!

Kama wangekuwa waliofanya hivyo ni moja ya kazi zao basi wamefanya makusidi kufikisha ujumbe kuwa usitupe mawe ukiwa ndani ya nyumba ya kioo.

Huyu Bwana samahani 'Dr' kama kweli wataalamu wangekuwa wanamuhitaji,

  • Gari analoendesha au kuendeshwa linajulikana
  • Sehemu anayopata kinywaji inajulikana
  • Sehemu anayopenda kwenda kupumzika inajulikana
  • Mahali anapokaa inajulikana

Ki-James Bond, wangesubiri joto na pressure ya mgomo ishuke, wanaenda na kilo moja ya 'Bwimbi' madawa ya kulevya wanaweka kwenye boot ya gari yake au Masters bedroom ta nyumbani kwake bila yeye kujua na baadaye linasukwa zengwe la uuzaji wa madawa ya kulevya na hatimaye anatiwa mbaroni na hapo hatakuwa na washabiki wa kumshangilia na kumtetea.

Hiki kipigo alichokipata mungu apishe mbali kiwe kilitoka sehemu nyingine lakini sitaki kuamini kuwa ni kazi ya Professionals kama watu wanavyotaka kuaamini hapa kwa Great 'Sinkers'

Pole Daktari! lakini kuna watanzania walikufa katika mgomo uliopita kwa kukosa huduma!
 
wanagoma na mwisho wa mwezi wanaenda na ATM kudraw Bank fedha zetu walipa kodi huku wagonjwa wetu wanakufa hospitali. hii ni halali? kwanini waendelee kulipwa mwezi huu? kwanini serikali haigomi kuwalipa kwa kususa kwao? hawatendi haki hata kidogo.
Si bora ya hao! Je wale wanaolala bungeni huku posho kwa siku ni Mshahara wa Mwalimu IIIA, V8 linawekwa mafuta lita sh 3000/= nk
 
hey wanajamii wengine mna chuki zisizo na misingi. U need to behave and act mature, humanly and professional. sasa asiende kumuona mgonjwa kwa nini? Hujui ukiwa mgonjwa watu kukujulia hali tu ni sababu tosha ya kupata nafuu.....maana. Raisi anakwenda pale kama binadamu yeyote. Pia msiwe na mawazo hasi kila mara na kumhusianisha Raisi na ajali aliyopata Steven. Mbona wakati mpiganaji Waziri Mwakyembe alipopatwa na janga hamkuhamasika na kuwatafuta waliosababisha? je walikua ndugu zenu?....
 
Madaktari wamkatalie, kwa sababu ya majeraha aliyonayo asije akamwambukiza magonjwa mengine kama ukimwi.
 
Unaweza kumkatalia mkuu wa nchi hasimuone mwananchi wake? sijui! Hata hivyo, huo si uamuzi wa maDaktari kumkatalia Rais kwenda kumuona Daktari mwenzao..bali ni uamuzi wa Dr Ulimboka mwenyewe na familia yake. Au Daktari mwangalizi wa Ulimboka anaweza kataa kwa misingi ya kitabibu kuwa mgonjwa wake hana hali nzuri kiasi cha kutembelewa!

Well said!
 
Back
Top Bottom