2025 kuna uwezekano Paul Makonda akachukua fomu ya Urais. Ndipo Rais Samia ataijua vizuri rangi ya Paul Makonda

Kiboko ya Jiwe

JF-Expert Member
Apr 7, 2020
12,703
36,151
Nimekaa pale nawazoom Watanzania mimi mlinzi msomi na mwenye vinasaba vya kinabii.

Hizi sifa anazozichukua huko mitaani kwenye ziara zake huyu Mheshimiwa zitamfanya 2030 aione iko mbali.

Maana kwa sasa target yake kubwa ni Urais na si cheo chochote. Aliamini 2025 angeachiwa kijiti na Magufuli lakini dili likagoma mapema tangu tu alipopigwa chini kwenye kura za maoni jimboni (Kigamboni).

Sasa baada ya kuukwaa uenezi anaitazama 2030 lakini kwa sifa anazopata mtaani hatoweza kusubiri 2030.

Mwakani 2025 anajilipua rasmi liwalo na liwe. Kama akilljilipua kuna uwezekano akaungwa mkono na wanakamati wengi hapo ndipo Watanzania wataona kasheshe.

Mimi simpendi Makonda, hata nyuzi zangu zinaonyesha hilo kwa uwazi kabisa lakini akigombea Urais nitamuunga mkono.

Kwa jinsi alivyo yule kijana ataleta maendeleo makubwa hapa nchini, naamini makandokando yake atayaacha.

Suala la Rais aliyeko madarani kupiti bila kupingwa kwenye kura za maoni huko CCM usilitafakari sana kwenye uchaguzi wao wa ndani 2025. Lolote linaweza kutokea.
 
Naona toka jamaa achaguliwe kuwa katibu mwenezi, wapinzani wake mnakosa usingizi, na kuja na vijimada vichovu vichovu vya kujikatisha tamaa na kujifariji.

Si ni nyinyi mliomba mikutano ya siasa iruhusiwe, kisha mkaanza na vimikutano vyenu vya kuokota okota watu wawili watatu kwenye mikutano, mbona sasa baada ya jamaa kuchaguliwa mikutano yenu imekufa ghafla na kuja na vimada vya kipuuzi puuzi kama hivi?
 
Kama unaweza kufikiri hivyo basi akili yako ni ndogo kuliko ya mende. Yaani hata Zerobrain Makonda anakuzidi akili
 
aliacha ukuu wa mkoa mbele ya baba yake kugombea ubunge kilichofata kaangukia wowo sio pua.leo cheo hiko tafute uraisi we embu acha kujaza server ya JF.hakitolewa unataka mbwembwe zijifiche
 
Back
Top Bottom