Kuna genge limejipanga kuharibu kwa makusudi sifa na hadhi ya Rais Samia

olimpio

JF-Expert Member
Apr 5, 2023
402
834
Kwenye Siasa , " Hakuna kinachotokea kwa bahati mbaya " everything is planned .

Think about this ,
Soko la kariakoo wafanya biashara wameandamana, mkataba wa bandari umuvujishwa kwa mbwembwe na tayari kila kona kuna watu wamepangwa kuushambulia , ghafla mkataba hauongelewi maada inageuka kua Rais hana uwezo, Rais hatoshi , etc.

I need to let you know this piece of classified information kwa kua imebidi niwamegee kidogo.

Agenda sio bandari hata kidogo , agenda ni Urais 2025. Kuna siku Chalamila akiwa Kagera aliwahi kusema kuna mawaziri wamesafiri kwenda nchi za nje kusaka fund za kuusaka uraisi, kuna watu walihisi Chalamila ameropoka.

Twende mdogo mdogo sasa, Mwezi August mwaka 2022 , waziri mmoja mwenye mafungamano na Kigogo aliunda rasmi genge la kuusaka uraisi na kila mtu kwenye taasisi nyeti serikalini za kiusalama na maamuzi magumu anajua hili ninalolisema, Rais analijua hili kundi, na ni kundi ambalo liko tayari hata kuuwa ukisimama kwenye njia yao, it is a gang within the Government.

Genge hili lina watu nyeti na viongozi waandamizi wengi ambao baadhi ni reject wa serikali iliyopo sasa.
Kama mnakumbuka, Rais samia ameanza kuwarudisha serikalini viongozi kadhaa waliowahi kuhudumu enzi za Rais Magufuli, Rais Samia hapo kabla aliaminishwa kua yeyote aliyetumika na RAIS Magufuli alikuwa anamtakia mabaya.

Till late last year Rais Samia akafanikiwa kujua Rangi za aliohisi wako naye kumbe wanatafuta kumamliza na kuchukua Urais kijanja na kwa usmart sana.

Genge hili lilifahamu Rais Samia ameshajua mipango yao , na kati ya mipango ya Rais Samia ilikuwa Berndard Membe aje awe mgombea Mwenza 2025. Genge lilichukia sana na kuona kua Membe angekuwa na smooth passage ya kuwa Rais 2030 Baada ya RAIS Samia.

Vita ikaanza Rasmi na genge hilo likaapa kumpigisha ajali kwa kila atakachofanya Rais Samia. Ni kwa sababu baadhi ya mambo ni classfied na yana NDA (Non disclosure Agreement ). Vinginevyo mkataba ambao hata sio wa milele ungewekwa hadharani. Kwanini mkataba hauwekwi hadharani wa badari?

Kampuni inayotaka kuingia ubia na Serikali ya Tanzania ina biashara sehemu zingine Duniani, kuweka wazi mkataba ambao una NDA ni kuharibu biashara yao maeneo mengine na sio ethics za biashara pia.

Genge hili baada ya kujua mkataba una NDA, wakaona Rais hawezi kuutoa hadharani, hivyo hata wakitunga duration ya mkataba hataweza kukataa wala kuutoa hadharani.

Nini kimeandaliwa Rasmi na genge hili kwa sasa. Watu hawa wakiongozwa na waziri ambaye kwa mambo yalipofika anaweza kutenguliwa rasmi, wanalipa watu kumtukana Rais ili waue brand kabisa.

Fikiria hadi Mange Kimambi amebadilika kutoka kuongelea Mkataba sasa nafanya personal attacks kwa Rais, hawaongelei tena Mkataba wala wanasheria waliohusika kunegotiate , the target ni Rais wa nchi . Mange Kimambi amelipwa kwa njia ya Bitcoin fedha zenye thamani ya 800 Million za kitanzania. From last Month na aliambiwa asubiri assignement, this is the clear assigment .

Huyu mnayemwona Kigogo kama anamtetea Rais, don't buy it , it is a set up, atapinduka soon na ataanza kumchafua Rais very soon, it is a strategic movement.

Hawa watu wako serious sana, wanalipa pesa nyingi sana kuusaka urais sio wa 2030 ni wa 2025.

Ni majangili haya, na kama hamuamini in less than a week to come anaweza kufariki mtu muhimu sana mmoja.

I'm telling you this sio kwa sababu sijui kwamba Bandari ni muhimu, sio kwa sababu nasupport waarabu wapewe bandari hapana, the agenda is not about Bandari get your third eye and see.

Tulimpoteza Rais Magufuli japokua na watu walifurahia lakini nawaambia, kama watanzania watazinunua hizi siasa zinazoendelea tutakuwa na Rais wa nchi ambaye ni Magufuli Reject Pro.

Bahati mabaya sana, baada ya miezi zaidi ya miwili watu hua wanarejea maandiko haya na kusema kumbe ilikuwa kweli.

Kwa viongozi wa Upinzani wengi wanacheza ngoma isiyowahusu wanakoleza moto usio na manufaa kwao.

Genge hili limeanza kupita kwa maaskofu na baadhi ya wanaojiita manabii kumpaka matope RAIS Samia kua anataka kuiingiza nchi kwenye OIC (Organization of islamic Countries) ili akose uungwaji mkono toka jamii ya wakristo hii sio haki, Uislamu wa Rais Samia kisiwe kigezo cha kumfitini kwa wakristo.

Genge hili linahonga hadi viongozi wa jumuia za kikistro ili waanzishe movement kulalamika Rais Samia anataka kuiuza nchi kwa jumuia ya Kiislamu, lengo wamchafue kisiasa na akose kabisa uungwaji mkono.

Nimeyasema yote haya nikiamini wanasiasa na waovu hawa muwajue na mjue laana wanayowaletea.
Chagueni na kujadiliana kwa weledi , wenzeni agenda zao sio hizo.

NOTE: Rais anamtaka Polepole arudi awe mwenezi genge liko tayari kufanya chochote pole pole asiwe karibu na Rais

Samia.jpg
 
Nimekuelewa kiasi na hii Sheria ya tiss kupitishwa haraka lengo ni rais kuwashughulikia hao wataka urais au Nia ajenda iliopita kwa wasaka urais maana ulisema jamaa mtandao wao ni mkubwa.
 
Wataje majina hao acha kuzunguka kama ukizunguka tutajua unapika majungu
 
Back
Top Bottom