johnthebaptist
JF-Expert Member
- May 27, 2014
- 82,752
- 139,557
Ukizisoma vizuri hizi nyakati utagundua hakuna fursa tena ya Upinzani mamboleo ule unaotegemea " hisani" ya ruzuku ili chama na viongozi wake waweze kuishi.
Unaweza kujiuliza kwanini maalimu Seif alialikwa Ikulu na yeye siyo kiongozi wa ACT wazalendo?
Halafu iangalie vizuri historia ya Prof Lipumba na James Mbatia katika siasa za Tanzania. Kisha jikumbushe namna Nccr mageuzi na Cuf zilivyoasisiwa na namna mzee Mapalala rip alivyokimbizwa chamani na maalimu Seif.
Yuko wapi mzee Marando wa Nccr mageuzi aliyehamia Chadema? Je baada ya bunge kuvunjwa Joseph Selasini atabakia Chadema?...... Prof Baregu je? na Prof Safari?
Kwa kifupi ni kwamba robo karne ya Upinzani mamboleo imefikia tamati, Chadema itabaki na mzee Mtei lakini Lyatonga Mrema, mzee Cheyo, mzee Shibuda wote hawa watarejea CCM where they belong.
Kisha vipimo vitamwelekea Zitto Kabwe wa ACT wazalendo kama ni mpinzani wa kizazi kipya au ndio walewale. Ikumbukwe wakati upinzani unaasisiwa Zitto alikuwa bado ni mtoto kwa mujibu wa sheria za nchi.
Nawatakia Kwaresma yenye baraka
Maendeleo hayana vyama!
Unaweza kujiuliza kwanini maalimu Seif alialikwa Ikulu na yeye siyo kiongozi wa ACT wazalendo?
Halafu iangalie vizuri historia ya Prof Lipumba na James Mbatia katika siasa za Tanzania. Kisha jikumbushe namna Nccr mageuzi na Cuf zilivyoasisiwa na namna mzee Mapalala rip alivyokimbizwa chamani na maalimu Seif.
Yuko wapi mzee Marando wa Nccr mageuzi aliyehamia Chadema? Je baada ya bunge kuvunjwa Joseph Selasini atabakia Chadema?...... Prof Baregu je? na Prof Safari?
Kwa kifupi ni kwamba robo karne ya Upinzani mamboleo imefikia tamati, Chadema itabaki na mzee Mtei lakini Lyatonga Mrema, mzee Cheyo, mzee Shibuda wote hawa watarejea CCM where they belong.
Kisha vipimo vitamwelekea Zitto Kabwe wa ACT wazalendo kama ni mpinzani wa kizazi kipya au ndio walewale. Ikumbukwe wakati upinzani unaasisiwa Zitto alikuwa bado ni mtoto kwa mujibu wa sheria za nchi.
Nawatakia Kwaresma yenye baraka
Maendeleo hayana vyama!